cdm mna michezo ya kitoto sana, kuanzia juzi mlikuwa mnatafuta nguo za ccm sasa jana mmezipata leo mmewavalisha wahuni wenu na kuwapachika kwenye kundi la ccm na kuwatuma wafanye fujo ili tu ionekane ccm wabaya
Wakuu sasa labda haya ni maagizo au ni kitu gani, subjected to debate. Leo kulikuwa na mikutano miwili ya uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo Kata ya Msalato, Manispaa ya Dodoma, nje kidogo ya mjii.
CHADEMA walikuwa wanazindulia katika eneo la Msalato Bibo, karibu na Shule ya Sekondari Msalato, vipaji maalum. CCM wao walikuwa wanafanyia uzinduzi wao katika eneo la Msalato Gulioni, ni eneo ambalo liko karibu na barabara.
Msafara wa CHADEMA umefika eneo hilo majira ya saa 9. Kama ilivyo ada ya wageni wakifika mahali, viongozi wa kitaifa walikuwa wanakwenda kuweka saini katika kitabu cha wageni kwenye Ofisi ya Kata ya Msalato. Ili ufike mjini iliko ofisi hiyo ni lazima upite eneo la gulio, walipokuwa CCM.
Kufumba na kufumbua, wakati msafara ukipita maeneo hayo, ukiongozwa na watu wa pikipiki takribani 40+, hee mara mawe yakaanzwa kurushwa upande wa msafara wa CHADEMA kutoka kwa wafuasi wa CCM ambao wengi wao walikuwa wamesombwa kwa magari kutoka mjini.
Kama hiyo ya kuponda mawe msafara wa CHADEMA haitoshi, sasa wakaamua kwenda hatua nyingi zaidi mbele, wakamkamata mwandishi wa habari Danson Kaijage. Wakaanza kumshuhushia kipondo kikali. Wakitaka kumyang'anya kamera, wachukue picha alizopiga wakati wanawashambulia CHADEMA.
Kariibu wote waliokuwa wakimshambulia Kaijage anawafahamu. Salama yake ilikuwa ni kuwasili kwa polisi eneo hilo, ambao hata hivyo walichlewa sana kufika eneo la mkutano kufanya kazi yao ya ulinzi. Polisi walishindwa ku-guarantee usalama na kuzuia yaliyotokea leo.
Nitakuja kumalziia kuelezea namna ambavyo CCM walisomba watu kutoka mjini, mgeni rasmi akaonekana akija eneo la mkutano lakini akakutwa watu hawajasombwa vya kutosha hivyo akalazimika kurudi tena mjini mpaka watu wajae, kisha akarudi tena baadae kufanya uzinduzi.
Unajua mgeni rasmi alikuwa nani?
Wakuu sasa labda haya ni maagizo au ni kitu gani, subjected to debate. Leo kulikuwa na mikutano miwili ya uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo Kata ya Msalato, Manispaa ya Dodoma, nje kidogo ya mjii.
CHADEMA walikuwa wanazindulia katika eneo la Msalato Bibo, karibu na Shule ya Sekondari Msalato, vipaji maalum. CCM wao walikuwa wanafanyia uzinduzi wao katika eneo la Msalato Gulioni, ni eneo ambalo liko karibu na barabara.
Msafara wa CHADEMA umefika eneo hilo majira ya saa 9. Kama ilivyo ada ya wageni wakifika mahali, viongozi wa kitaifa walikuwa wanakwenda kuweka saini katika kitabu cha wageni kwenye Ofisi ya Kata ya Msalato. Ili ufike mjini iliko ofisi hiyo ni lazima upite eneo la gulio, walipokuwa CCM.
Kufumba na kufumbua, wakati msafara ukipita maeneo hayo, ukiongozwa na watu wa pikipiki takribani 40+, hee mara mawe yakaanzwa kurushwa upande wa msafara wa CHADEMA kutoka kwa wafuasi wa CCM ambao wengi wao walikuwa wamesombwa kwa magari kutoka mjini.
Kama hiyo ya kuponda mawe msafara wa CHADEMA haitoshi, sasa wakaamua kwenda hatua nyingi zaidi mbele, wakamkamata mwandishi wa habari Danson Kaijage. Wakaanza kumshuhushia kipondo kikali. Wakitaka kumyang'anya kamera, wachukue picha alizopiga wakati wanawashambulia CHADEMA.
Kariibu wote waliokuwa wakimshambulia Kaijage anawafahamu. Salama yake ilikuwa ni kuwasili kwa polisi eneo hilo, ambao hata hivyo walichlewa sana kufika eneo la mkutano kufanya kazi yao ya ulinzi. Polisi walishindwa ku-guarantee usalama na kuzuia yaliyotokea leo.
Nitakuja kumalziia kuelezea namna ambavyo CCM walisomba watu kutoka mjini, mgeni rasmi akaonekana akija eneo la mkutano lakini akakutwa watu hawajasombwa vya kutosha hivyo akalazimika kurudi tena mjini mpaka watu wajae, kisha akarudi tena baadae kufanya uzinduzi.
Unajua mgeni rasmi alikuwa nani?
Isije ikawa ni vichaa walisombwa kutoka milembe,sidhani kama kuna mtanganyika mwenye akili timamu anaye weza kuwapiga chadema mawe.chunguzeni kwa makini mtagundua nani walisombwa.