brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,876
- 7,366
Katika hali isiyokuwa ya kawaida chama cha mapinduzi kimekuwa kinakosa watu katika kampeni zake kuelekea uchaguzi wa selikari za mitaa, katika mji wa Ifakara wagombea wa CCM wamekuwa wakizomewa katika mitaa mbalimbali, diwani wa ifakara mjini kupitia chadema amekuwa na wafuasi wengi baada ya kufanikiwa kufuta michango mingi isiyokuwa na tija na kupelekea watu wengi kujitokeza kwenye kampeni za UKAWA.
Katika tarafa ya Mang'ula ambapo ndio ngome kuu ya CCM hali ni tete pia baada ya jana tarehe 4/5/2014 chama cha mapinduzi kulazimika kumaliza kampeni zake mapema majira ya saa kumi jioni baada ya wagombea kujikuta wapo wenyewe huku wananchi wakisusa kwenda kuwasikiliza huku ukizuka mzozo wa wenyewe kwa wenyewe kwa kushindwa kuwahamasisha wananchi, huku baadhi ya wagombea wakilalamika kwa kuhukumiwa kwa makosa ambayo hawajayafanya wao.
Mbunge wa jimbo la kilombero mh. Abdul mtegeta kupitia ccm ameitwa haraka ili kuokoa jahazi.
Katika tarafa ya Mang'ula ambapo ndio ngome kuu ya CCM hali ni tete pia baada ya jana tarehe 4/5/2014 chama cha mapinduzi kulazimika kumaliza kampeni zake mapema majira ya saa kumi jioni baada ya wagombea kujikuta wapo wenyewe huku wananchi wakisusa kwenda kuwasikiliza huku ukizuka mzozo wa wenyewe kwa wenyewe kwa kushindwa kuwahamasisha wananchi, huku baadhi ya wagombea wakilalamika kwa kuhukumiwa kwa makosa ambayo hawajayafanya wao.
Mbunge wa jimbo la kilombero mh. Abdul mtegeta kupitia ccm ameitwa haraka ili kuokoa jahazi.