Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,725
- 18,620
Wakuu jana CCM wametoa press na kusema kuna haja ya kufufua mchakato wa Katiba mpya
Katiba mpya ambayo imekuwa kilio cha muda mrefu cha wapinzani na wataka mabadiliko nchini, inatarajiwa kukuza demokrasia, kuleta uwajibikaji, ugatuaji wa madaraka na ufanisi wa kuendesha serikali
Sasa CCM ambao walikataa katiba 2014 na kusisitiza mara kwa mara katiba haina umuhimu sababu wananchi wanachohitaji ni kula tu, ghafla wamebadilika
Nina uhakika hawana nia wala mpango wowote na katiba mpya, lakini nsiojaelewa ni karata gani wanacheza haswa
CCM ni chama kinachopenda ubwanyenye (Conservatism) na ukiritimba (monopoly) kwenye siasa mambo ambayo Katiba mpya inataka kuleta mapinduzi dhidi yake, nitatoa miofano michache kuthibitisha hayo
1. Katiba ya CCM imempa madaraka makubwa sana mwenyekiti wao ambaye ndio Rais na mtu yoyote akimkosoa ndani ya chama basi ndio mwisho wake kisiasa, mfano Ndugai alipokosoa kuhusu mikopo, kuna Baraka Shamte alimkosoa Mwinyi akafukuzwa chama
2. pia hata Bunge linavyoendeshwa kuna baadhi ya wabunge wamekuwa wanakosoa mawaziri lakini wabunge hawa wamekuwa wakitishwa kuwa wanampinga Rais,
3. CCM miaka ya hivi karibuni kupitia vyombo vya habari, wasanii, viongozi wa dini wamekuwa wakitengeneza image ya Umungu kwa Rais, mtu ambaye hana makosa, jasiri, anajua yote, mwenye nia njema kuliko wote, mwenye akili kuliko wote na kwa image hii wanaom kosoa wote wanaonekana watukutu ama waliokosa nidhamu, sasa hawa watu ndio watake katiba itakayoleta demokrasia na kupunguza nguvu ya Rais? UNLIKELY
jE MKAKATI WAO NI UPI HASWA?
Katiba mpya ambayo imekuwa kilio cha muda mrefu cha wapinzani na wataka mabadiliko nchini, inatarajiwa kukuza demokrasia, kuleta uwajibikaji, ugatuaji wa madaraka na ufanisi wa kuendesha serikali
Sasa CCM ambao walikataa katiba 2014 na kusisitiza mara kwa mara katiba haina umuhimu sababu wananchi wanachohitaji ni kula tu, ghafla wamebadilika
Nina uhakika hawana nia wala mpango wowote na katiba mpya, lakini nsiojaelewa ni karata gani wanacheza haswa
CCM ni chama kinachopenda ubwanyenye (Conservatism) na ukiritimba (monopoly) kwenye siasa mambo ambayo Katiba mpya inataka kuleta mapinduzi dhidi yake, nitatoa miofano michache kuthibitisha hayo
1. Katiba ya CCM imempa madaraka makubwa sana mwenyekiti wao ambaye ndio Rais na mtu yoyote akimkosoa ndani ya chama basi ndio mwisho wake kisiasa, mfano Ndugai alipokosoa kuhusu mikopo, kuna Baraka Shamte alimkosoa Mwinyi akafukuzwa chama
2. pia hata Bunge linavyoendeshwa kuna baadhi ya wabunge wamekuwa wanakosoa mawaziri lakini wabunge hawa wamekuwa wakitishwa kuwa wanampinga Rais,
3. CCM miaka ya hivi karibuni kupitia vyombo vya habari, wasanii, viongozi wa dini wamekuwa wakitengeneza image ya Umungu kwa Rais, mtu ambaye hana makosa, jasiri, anajua yote, mwenye nia njema kuliko wote, mwenye akili kuliko wote na kwa image hii wanaom kosoa wote wanaonekana watukutu ama waliokosa nidhamu, sasa hawa watu ndio watake katiba itakayoleta demokrasia na kupunguza nguvu ya Rais? UNLIKELY
jE MKAKATI WAO NI UPI HASWA?