CCM wanauwana ....

Hasara

Senior Member
Dec 29, 2006
138
9
CCM wanauwana ....
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ahamua kumaliza ruswa katika nafasi ya umakamu wa mwenyekiti wa CCM kwa kumteuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, baada ya kugundua waliyo mzunguka walikuwa na ajenda ya siri, walifanya kampeni kubwa yeye akiwa safarini,walitumia resource nyingi za taifa kujinadi,

Baada ya muungwana kujua hilo haya ndiyo mawazo na uwamuzi wake
na wengine walituma wabunge sehemu mbali mbali kuwafanyia kampeni wengine hadi kupatwa na mauti,

waliyo jinadi sana na kumuogopesha muungwana ni waziri wake mkuu,

Baada ya uchaguzi huu ndiyo kila kiongozi atajua nini cha kufanya na JK ni nani wake basi hapo ndipo tutaona vilio vya wakubwa...subirini

wengi wametumia mamilioni ya pesa alafu unakuja kuweka mgombea pekee?

maana ya mmgombea pekee ni nini?
naomba kutoa hoja
 
CCM wanauwana ....
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ahamua kumaliza ruswa katika nafasi ya umakamu wa mwenyekiti wa CCM kwa kumteuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, baada ya kugundua waliyo mzunguka walikuwa na ajenda ya siri, walifanya kampeni kubwa yeye akiwa safarini,walitumia resource nyingi za taifa kujinadi,

Baada ya muungwana kujua hilo haya ndiyo mawazo na uwamuzi wake
na wengine walituma wabunge sehemu mbali mbali kuwafanyia kampeni wengine hadi kupatwa na mauti,

waliyo jinadi sana na kumuogopesha muungwana ni waziri wake mkuu,

Baada ya uchaguzi huu ndiyo kila kiongozi atajua nini cha kufanya na JK ni nani wake basi hapo ndipo tutaona vilio vya wakubwa...subirini

wengi wametumia mamilioni ya pesa alafu unakuja kuweka mgombea pekee?

maana ya mmgombea pekee ni nini?
naomba kutoa hoja


Wana CCM njooni mumjibu Hasara hapa.
 
Dua,

Usimsikilize Hasara. Ni kweli aliyosema, ila sio kweli kuwa EL alitaka u makamu. Hell NO, ni uongo , kuna waliotaka hiyo nafasi, nitaelezea mengi nikirudi kutoka Dodoma na nikiwa nimefanikiwa hazima yangu ya kilichonileta Dodoma!

Wale wa Dar tunaofahamiana mnaweza kuandaa party tu..., haina haja ya kungoja mpaka kesho. mambo juu ya msitari!
 
Dua,

Kwa ufupi Mtandao umepigwa chini vibaya sana, Yaani Muungwana ameprove kuwa Kiongozi wa kweli. Waliitaka nafasi ya umakamu WAMEIKOSA! Check NEC watakavyoanguka.

Mungu mbariki Muungwana Mungu ibariki Tanzania.

Jamani narudi ndani. I love JF
 
FD,
Hao mtandao ni akina nani ikiwa JK yupo nje. Mimi nilidhani Mtandao ni wafuasi wa JK mwenyewe kumbe inavyoonyesha kuna mgawanyiko kati ya JK na EL...
Na kama ndivyo basi kwa nini asianze na kumsimamisha EL moja kwa moja kwani waziuri mkuu sio nafasi inayochaguliwa na wananchi. Ni yeye mwenyewe, kuondoa mzizi wa fitna ni kumwondoa EL ktk nafasi ya Waziri mkuu lakini kuacha mzizi huo, mvua itanyesha na mti utastawi kwa uwezo wake Mungu.
 
Dua,

Yaani Muungwana ameprove kuwa Kiongozi wa kweli.

Ushupavu wake utaonekana kwa kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi na nchi na wala sio hayo maigizo ya hapo Kizota. Mwambie akae chini afikiri namna ya kutokomeza lindi la umaskini, atumie urais wake kutomeza ufisadi, achape kazi, atulie, aache kuzurura na kuwagawaiwa wazungu vipanda vya ardhi yetu. Tunamtakia kila la heri akifanya hivi.
 
FD

Hicho ni kipi hasa kilicho kupeleka Dodoma, maana umekuwa ukirudia kila mara "kilichonileta" hapo Dodoma au ndio U- NEC mkuu.

Haya basi mimi nakuombea kila la kheri ufanikishe azma yako hiyo..
 
Dua,

Usimsikilize Hasara. Ni kweli aliyosema, ila sio kweli kuwa EL alitaka u makamu. Hell NO, ni uongo , kuna waliotaka hiyo nafasi, nitaelezea mengi nikirudi kutoka Dodoma na nikiwa nimefanikiwa hazima yangu ya kilichonileta Dodoma!

Wale wa Dar tunaofahamiana mnaweza kuandaa party tu..., haina haja ya kungoja mpaka kesho. mambo juu ya msitari!

FD pamoja na kuwa ww ni mwanachama wa sisiemu, je na ww ni mgombea katika uchaguzi huu? Naona unawaambia jamaa zako waanda aherehe. Tudokeze kidogo basi.
 
CCM wanauwana ....
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ahamua kumaliza ruswa katika nafasi ya umakamu wa mwenyekiti wa CCM kwa kumteuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, baada ya kugundua waliyo mzunguka walikuwa na ajenda ya siri, walifanya kampeni kubwa yeye akiwa safarini,walitumia resource nyingi za taifa kujinadi,

Baada ya muungwana kujua hilo haya ndiyo mawazo na uwamuzi wake
na wengine walituma wabunge sehemu mbali mbali kuwafanyia kampeni wengine hadi kupatwa na mauti,

waliyo jinadi sana na kumuogopesha muungwana ni waziri wake mkuu,

Baada ya uchaguzi huu ndiyo kila kiongozi atajua nini cha kufanya na JK ni nani wake basi hapo ndipo tutaona vilio vya wakubwa...subirini

wengi wametumia mamilioni ya pesa alafu unakuja kuweka mgombea pekee?

maana ya mmgombea pekee ni nini?
naomba kutoa hoja

haya maneno yametoka wapi ?
 
FD

Hicho ni kipi hasa kilicho kupeleka Dodoma, maana umekuwa ukirudia kila mara "kilichonileta" hapo Dodoma au ndio U- NEC mkuu.

Haya basi mimi nakuombea kila la kheri ufanikishe azma yako hiyo..

Masatu, kama umemsoma vizuri apo juu, FD anawataka wale wa dar wanaomfahamu waandae party manakeinaelekea atapata kile 'alichofuata' apo dodoma

Sisi tusiokufahamu tutashirikije FD au ndo unatutosa mkuu?
 
Mimi nili joke, inawezekana kuna ukweli. haya Fd ninakutakia kila la heri, huenda ukawa chachu ya mabadiliko kwenye chama chenu.
 
Masatu, kama umemsoma vizuri apo juu, FD anawataka wale wa dar wanaomfahamu waandae party manakeinaelekea atapata kile 'alichofuata' apo dodoma

Sisi tusiokufahamu tutashirikije FD au ndo unatutosa mkuu?

Nakulilia TZ hata mimi nina wasiwasi FD akipata kilichompeleka Dodoma huenda hata kwenye "cocktail" hatuto pata mwaliko!

Taarifa zilizojiri ni kuwa Mswahili nae ameonekana akivinjari maeneo ya Kizota huenda nae akaramba dume....

Chelea chelea utakuta mwana si wako..
 
Nilisema Watanzania tumepata Raisi ambae hajawahi kupatikana,na pia nilisema kuhusiana na mitandao au vigogo waliokuwa wanachumia matumbo yao tu,hawa walikuwa ni wengi na wameshaota mizizi na kuota kwa sura nyingi kila kona ya Tanzania ,kupambana nao ni kazi ngumu na ni hatari ila JK ameliona na anakwenda nalo taratibu sana bila ya kumwaga unga.Tulieni anawajua ni nani wapenda maendeleo kwa nchi na wananchi na ni nani ni walaji au makupe.
 
Sisi tulio wahi kuendesha malori mabovu aina ya BEDFORD, kama yale ya kusombea mkaa,tunajua namna ya kuya treat pale gear namba 1 ikishindwa kuingia na wakati huohuo lori liko katikati ya kilima.

Gear # 1 ikigoma kuingia hapo maisha yako na ya abiria wengine ndani ya Lori yamo mikononi mwa utingo.
Utingo anakaa standby muda wote akisikiliza change down ya Gia.

Unapangua gia namba 4 na kurushia namba 3 unaweka moto chini lori linajibu mapigo.
Unapangua gia namba 3 na kubandika gia namba 2 unaweka moto chini mpaka kwenye bati lori linalalamika kishenzi lakini haliendi kokote.
Unapiga moyo konde unapangua gia namba 2 unaitafuta 1 na moja inakutafuta wewe Toba!.

Unaita kwa sauti kuu ya mayowe ya shetani kubanwa mkia na mlango.

Haya! haya! mwanangu kula Rec!

Kama paka, mwizi utingo huyoo! anaruka na kigogo chake begani, na wakati huo huo gia Box inalalamika Giiiiiiiiieeeei!

Utingo kwa Timing ya hali ya juu kabisa anasubiri lori lisimame kabla halijaanza kurudi kinyume nyume utingo anabandika kigogo, lori hata kama limebeba dunia yote linasimama pale pale, na lori linasimama wote mnaangau kicheko.

Tumewahi kujaribu Semi trailer kubwa za zaidi ya tani 100, kwa perfect timing zinasisima bila wasi. Siyo kwa vigogo viwili, kimoja tu.

MH Kikwete ametumia principle ya lori bovu mlimani kumlamba kete Edward Lowassa.

Good Move.
 
tena hata usinikumbushe malori babu, maana hata mie nimepush sana mzee, maeneo ya mpwapwa, mafinga, shinyanga, dodom, singida kote huko miaka ya 80 nikitafuta afueni ya maisha !
 
Dua,

Kwa ufupi Mtandao umepigwa chini vibaya sana, Yaani Muungwana ameprove kuwa Kiongozi wa kweli. Waliitaka nafasi ya umakamu WAMEIKOSA! Check NEC watakavyoanguka.

Mungu mbariki Muungwana Mungu ibariki Tanzania.

Jamani narudi ndani. I love JF


Mungu ambariki Muungwana kwa kipi hasa alichokifanya kwa Watanzania!? kusaini mikataba mibovu, kukumbatia mafisadi, wala rushwa na viongozi wanaopenda kujilimbikizia mali, haya kweli yanastahili kuombewa mungu ambariki!!!? :confused:
 
Mkuu
Ushupavu wake utaonekana kwa kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi na nchi na wala sio hayo maigizo ya hapo Kizota. Mwambie akae chini afikiri namna ya kutokomeza lindi la umaskini, atumie urais wake kutomeza ufisadi, achape kazi, atulie, aache kuzurura na kuwagawaiwa wazungu vipanda vya ardhi yetu. Tunamtakia kila la heri akifanya hivi.
Mkuu enzi zako ulikuwa mtu na nusu sijui nn kimekukuta
 
Back
Top Bottom