CCM WANATAKA TUMSUSIE POMBE MLEVI KWA FAIDA YA NANI?(Makala Dira Jumatatu)

KAMBOTA

Senior Member
Mar 21, 2011
176
103
nape-mjumbe.jpg
Na Nova Kambota,

Pengine hakuna ubishi kuwa katika historia ya CCM kuanzia kuasisiwa
kwake haijapata kuyumba kama sasa tena waziwazi kiasi kwamba wadadisi
washaanza kuhoji kuwa CCM inaenda orijojo au inakufa kabisa? na
wengine washaanza kutabiri kuwa CCM ipo mbioni kugeuka chama cha
upinzani.
Nashawishika kuamini kuwa CCM inazidi kubomoka kwa kasi ya ajabu ,
imani yangu hii inapewa nguvu na udhaifu mkubwa unaoendelea kuonyeshwa
na viongozi wapya wa CCM ikiwa ni muda mfupi tu tangu wapewe uongozi
huo.
Mara baada ya kile kilichoitwa "operation vua gamba" kuzinduliwa
rasmi kule Dodoma kama kawaida ya CCM walianza kujitapa kuwa huo ni
uamuzi mgumu lakini wenye kuhoji wakauliza mgumu kivipi?, kwa mbwembwe
kubwa tena bila kuombwa kina Mukama, Nappe na Chiligati wakaanza
kueneza tambo zao kuwa mafisadi watashughulikiwa kikwelikweli, wenye
kuhoji wakauliza tena CCM imeanza lini kuchukia ufisadi?
Kwa sauti ya kikada kina Nappe wakazidi kutamba kuwa CCM imeamua
kujivua gamba huku vyanzo mbalimbali vikidai kuwa miongoni mwa watu
waliotajwa kuwa magamba ni pamoja na Rostam Aziz, Edward Lowassa na
Andrew Chenge hivyo ni lazima wajiondoe wenyewe kwenye nafasi za
uongozi ama sivyo ndani ya siku tisini watatemwa! ilitia hamasa sana.
Lakini kabla hata ya siku thelathini kuisha tayari viongozi hao
wapya wa CCM wameanza kukana maneno yao,hivi karibuni Nappe Nauye
sambamba na Wilson Mukama walikana waziwazi kupeana siku tisini badala
yake wakadai siku miaishirini kabla hili halijaisha wakaibuka na hoja
kuwa mpaka kikao kifuatacho kisha wakabuni falsafa ya aina yake kuwa
mtu akioga basi ni mwili mzima sio viungo vichache tu,hwaeleweki!
Sasa katika sintofahamu hii inayonogeshwa utamu na hao watuhumiwa
wa ufisadi ambao tayari kuna taarifa kuwa wanaweza kumwaga mtama
kwenye kuku wengi kisha mambo yakazidi kuchacha. Hali hii ya
watuhumiwa wa ufisadi kutishia uhai wa chama imefanya kasi ya kina
Nappe kupungua tena ni wazi kuwa badala ya chama kuwayumbisha hao
watuhumiwa wa ufisadi sasa ni dhahiri kuwa CCM ndiyo inayumba na
kuyumbishwa sana na maamuzi legelege.
Udhaifu huu wa kimaamuzi umefanya viongozi wapya wa CCM kukimbia
baadhi ya maswali au kuwakimbia waandishi wa habari, kila mwenye macho
aliona jinsi Nappe Nauye au Mukama walivyojitokeza wiki iliyopita
kufafanua kuwa wanahabari wanapotosha kuandika kuwa watuhumiwa wa
ufisadi wamepewa siku 90, naam! hakuna ubishi kuwa Nappe na Mukama
wanazungumza kwa woga tena wanatetemeka hata ukiangalia nyuso zao sasa
utaona zile tambo zao zimekwisha kabisa, walipima kina cha maji sasa
wameona sio saizi yao!
Moja ya maswali yanayowachachafya viongozi hawa wa ccm ni lini
barua za kuwatimua mafisadi zitaandikwa? na nani atazisaini? kwa maana
tayari kuna taarifa kuwa kila mtu anaogopa kuzisaini mara zipo kwa
Nape, mara zipo mezani kwa Msekwa, baadaye zipo kwa Mukama na sasa
zinadaiwa zipo kwa mwenyekiti wa chama lakini swali ni lilelile nani
atathubutu kuzisaini?
Wenye kuona mbali washaanza kuhoji kwanini CCM inahofu sana
kutekeleza maazimio yake? inamwogopa nani? kwani kwanini wananchi
wanaichukia CCM? jibu ni rahisi tu kwasababu inalea mafisadi na
ufisadi, suluhisho la tatizo ni nini? jibu pia ni rahisi alihitaji
tuwe na PHD ni kuwa CCM iwatimue mafisadi wote pasipo huruma wala
ngojangoja, sasa hizi porojo za mara waandishi wanapotosha, ooh sio
siku 90 bali 120, mara jamani mbona mnatuchimba sana? tuacheni tujenge
chama chetu zinatoka wapi?
Mbona wakati ule kina Nappe walijiapiza kuwashughulikia mafisadi
bila huruma? sasa mbona huruma imekuwa kubwa sana tena ya siku 120?
kwanini? na huu mchezo wa kukimbia maswali na hoja za msingi umeanza
lini? nani kawaambia kuwa watanzania wana haja na propaganda zao?
wanataka tuwaachie chama chao, inachekesha sana! kwani mtanzania gani
mjinga ambaye atamsusia mlevi pombe akidhani amemkomoa? bilashaka
hakuna!
CCM hatuwezi kuiacha hata kidogo kwasababu ni chama tawala na
udhaifu wake unayumbisha nchi yetu pia kamwe kwa ulevi wao wasitegemee
tutawaachia pombe, wakinywa je? lazima tuendelee kuhoji udhaifu huu wa
CCM au ndio wanataka tuanze kuamini kuwa CCM imefichwa kwenye kwapa
za mafisadi? lakini kusuasua huku labda CCM wameanza kubaini kuwa
dhana ya ufisadi ndani ya CCM sio jambo la watu watatu bali ni mfumo
rasmi ambao labda umecheklewa tu kutangazwa, Tungoje tuone!
Nova Kambota ni mwandishi kijana wa Makala , ni mchambuzi na mtafiti
wa maswala ya kisiasa pia ni mwanaharakati wa vijana anapatikana kwa
anwani ya barua pepe; novakambota@gmail.com au tembelea blog yake ;
www.novatzdream.blogspot.com
Au mpigie kwa namba 0717-709618 au 0766-730256.
 
Huo usanii wa ccm siye tuliushitukia mapema na kukataa single yao ya kusaula magamba.
 
Wacha chama cha MAGAMBA kiende tu. Hakuna marefu yasiyo na mwisho.
 
Hahahaha... propaganda hizo ni "NGUVU YA SODA" hakuna jipya hapo kila mtu anataka kuonekana yeye ni bora kuanzia Mukama na wenzake wote hakuna atakaye nyooshea mafisadi kidole.

Waendelee na nguvu ya soda yao waone moto wa NGUVU YA UMA inavyofanya kazi!
Mapambano ndio kwanza yameanza..... mziki mnene unakuja lazima Magamba yangooke tu!!!!!!!!!!!!!:peace:
 
Kusubiri siku 90 ziishe ni zaidi ya kungoja tamthilia ya isidingo the need iishe.Huu ni mchezo wa kuigiza tu hamna chochote.
 
wenye akili zetu tulijua right from the day 1 kwamba ulikuwa ni mchezo wa kuigiza. Rebranding si strategy katika vyama vya kisiasa, sasa sijui nani kawaloga CCM wakai-apply!!! Kwa ufupi ni kwamba bila ufisadi (wa fedha za umma na kura) hakuna CCM so nani atakubali kujinyima ulaji CCM??? watawapata hao hao mabwege, wavivu wa ku-reason, rahisi kununulika (fulana, t-shirt, kofia, kilemba, kitenge na 5,000/-) sio mtu kama mimi!!!
 
View attachment 29772
Na Nova Kambota,

Pengine hakuna ubishi kuwa katika historia ya CCM kuanzia kuasisiwa
kwake haijapata kuyumba kama sasa tena waziwazi kiasi kwamba wadadisi
washaanza kuhoji kuwa CCM inaenda orijojo au inakufa kabisa? na
wengine washaanza kutabiri kuwa CCM ipo mbioni kugeuka chama cha
upinzani.
Nashawishika kuamini kuwa CCM inazidi kubomoka kwa kasi ya ajabu ,
imani yangu hii inapewa nguvu na udhaifu mkubwa unaoendelea kuonyeshwa
na viongozi wapya wa CCM ikiwa ni muda mfupi tu tangu wapewe uongozi
huo.
Mara baada ya kile kilichoitwa "operation vua gamba" kuzinduliwa
rasmi kule Dodoma kama kawaida ya CCM walianza kujitapa kuwa huo ni
uamuzi mgumu lakini wenye kuhoji wakauliza mgumu kivipi?, kwa mbwembwe
kubwa tena bila kuombwa kina Mukama, Nappe na Chiligati wakaanza
kueneza tambo zao kuwa mafisadi watashughulikiwa kikwelikweli, wenye
kuhoji wakauliza tena CCM imeanza lini kuchukia ufisadi?
Kwa sauti ya kikada kina Nappe wakazidi kutamba kuwa CCM imeamua
kujivua gamba huku vyanzo mbalimbali vikidai kuwa miongoni mwa watu
waliotajwa kuwa magamba ni pamoja na Rostam Aziz, Edward Lowassa na
Andrew Chenge hivyo ni lazima wajiondoe wenyewe kwenye nafasi za
uongozi ama sivyo ndani ya siku tisini watatemwa! ilitia hamasa sana.
Lakini kabla hata ya siku thelathini kuisha tayari viongozi hao
wapya wa CCM wameanza kukana maneno yao,hivi karibuni Nappe Nauye
sambamba na Wilson Mukama walikana waziwazi kupeana siku tisini badala
yake wakadai siku miaishirini kabla hili halijaisha wakaibuka na hoja
kuwa mpaka kikao kifuatacho kisha wakabuni falsafa ya aina yake kuwa
mtu akioga basi ni mwili mzima sio viungo vichache tu,hwaeleweki!
Sasa katika sintofahamu hii inayonogeshwa utamu na hao watuhumiwa
wa ufisadi ambao tayari kuna taarifa kuwa wanaweza kumwaga mtama
kwenye kuku wengi kisha mambo yakazidi kuchacha. Hali hii ya
watuhumiwa wa ufisadi kutishia uhai wa chama imefanya kasi ya kina
Nappe kupungua tena ni wazi kuwa badala ya chama kuwayumbisha hao
watuhumiwa wa ufisadi sasa ni dhahiri kuwa CCM ndiyo inayumba na
kuyumbishwa sana na maamuzi legelege.
Udhaifu huu wa kimaamuzi umefanya viongozi wapya wa CCM kukimbia
baadhi ya maswali au kuwakimbia waandishi wa habari, kila mwenye macho
aliona jinsi Nappe Nauye au Mukama walivyojitokeza wiki iliyopita
kufafanua kuwa wanahabari wanapotosha kuandika kuwa watuhumiwa wa
ufisadi wamepewa siku 90, naam! hakuna ubishi kuwa Nappe na Mukama
wanazungumza kwa woga tena wanatetemeka hata ukiangalia nyuso zao sasa
utaona zile tambo zao zimekwisha kabisa, walipima kina cha maji sasa
wameona sio saizi yao!
Moja ya maswali yanayowachachafya viongozi hawa wa ccm ni lini
barua za kuwatimua mafisadi zitaandikwa? na nani atazisaini? kwa maana
tayari kuna taarifa kuwa kila mtu anaogopa kuzisaini mara zipo kwa
Nape, mara zipo mezani kwa Msekwa, baadaye zipo kwa Mukama na sasa
zinadaiwa zipo kwa mwenyekiti wa chama lakini swali ni lilelile nani
atathubutu kuzisaini?
Wenye kuona mbali washaanza kuhoji kwanini CCM inahofu sana
kutekeleza maazimio yake? inamwogopa nani? kwani kwanini wananchi
wanaichukia CCM? jibu ni rahisi tu kwasababu inalea mafisadi na
ufisadi, suluhisho la tatizo ni nini? jibu pia ni rahisi alihitaji
tuwe na PHD ni kuwa CCM iwatimue mafisadi wote pasipo huruma wala
ngojangoja, sasa hizi porojo za mara waandishi wanapotosha, ooh sio
siku 90 bali 120, mara jamani mbona mnatuchimba sana? tuacheni tujenge
chama chetu zinatoka wapi?
Mbona wakati ule kina Nappe walijiapiza kuwashughulikia mafisadi
bila huruma? sasa mbona huruma imekuwa kubwa sana tena ya siku 120?
kwanini? na huu mchezo wa kukimbia maswali na hoja za msingi umeanza
lini? nani kawaambia kuwa watanzania wana haja na propaganda zao?
wanataka tuwaachie chama chao, inachekesha sana! kwani mtanzania gani
mjinga ambaye atamsusia mlevi pombe akidhani amemkomoa? bilashaka
hakuna!
CCM hatuwezi kuiacha hata kidogo kwasababu ni chama tawala na
udhaifu wake unayumbisha nchi yetu pia kamwe kwa ulevi wao wasitegemee
tutawaachia pombe, wakinywa je? lazima tuendelee kuhoji udhaifu huu wa
CCM au ndio wanataka tuanze kuamini kuwa CCM imefichwa kwenye kwapa
za mafisadi?
lakini kusuasua huku labda CCM wameanza kubaini kuwa
dhana ya ufisadi ndani ya CCM sio jambo la watu watatu bali ni mfumo
rasmi ambao labda umecheklewa tu kutangazwa, Tungoje tuone!
Nova Kambota ni mwandishi kijana wa Makala , ni mchambuzi na mtafiti
wa maswala ya kisiasa pia ni mwanaharakati wa vijana anapatikana kwa
anwani ya barua pepe; novakambota@gmail.com au tembelea blog yake ;
www.novatzdream.blogspot.com
Au mpigie kwa namba 0717-709618 au 0766-730256.
Hapo umenena Mkuu. Hatuwezi kuiacha kuisema ccm kwa vile ndiyo ni chama tawala na kimeshikilia maisha ya Watanzania mikononi. Je! Utampa dereva aliyelewa chakari bus lenye abiria? La hasha. Kutokemea ulevi wake ni janga kwa abiria wote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom