Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,082
- 33,567
Ukisoma kwenye mitandao ya kijamii na kusikiliza matamko ya baadhi ya viongozi wa CCM, unaona kabisa kwamba baadhi ya wanachama wa CCM wamekereka sana na Lissu kuwa hai na kuwa na akili timamu baada ya lile shambulio la Dodoma.
Lissu kuitwa "Msaliti" na wana CCM ilishazoeleka lakini sasa wana CCM wanataka kuitumia Tanzania kama kichaka cha kuelezea hisia zao dhidi ya Lissu. Ukiangalia kwa makini wana CCM wanaona Lissu ni mtu anayetakiwa kuadabishwa zaidi ya kushitakiwa.
Lengo la wana CCM hao (Siyo CCM) ni nini hasa. Jee kuna baadhi yao wanajua ni kina nani walihusika na shambulio la Lissu hivyo wana hofu iko siku Lissu atawataja watu hao na kuwaumbua hadharani?
Ukiona kauli zinazotoka kwa wana CCM walioko Bungeni, Baadhi ya wakuu wa mikoa, baadhi ya mawaziri, baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM na kina pangu pakavu tia mchuzi waliomo CCM, jambo moja la dhahiri kabisa ni kwamba kwa kauli zao inawezekana wanataka kumdhuru Lissu kutokana na misimamo yake!
Lissu kuitwa "Msaliti" na wana CCM ilishazoeleka lakini sasa wana CCM wanataka kuitumia Tanzania kama kichaka cha kuelezea hisia zao dhidi ya Lissu. Ukiangalia kwa makini wana CCM wanaona Lissu ni mtu anayetakiwa kuadabishwa zaidi ya kushitakiwa.
Lengo la wana CCM hao (Siyo CCM) ni nini hasa. Jee kuna baadhi yao wanajua ni kina nani walihusika na shambulio la Lissu hivyo wana hofu iko siku Lissu atawataja watu hao na kuwaumbua hadharani?
Ukiona kauli zinazotoka kwa wana CCM walioko Bungeni, Baadhi ya wakuu wa mikoa, baadhi ya mawaziri, baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM na kina pangu pakavu tia mchuzi waliomo CCM, jambo moja la dhahiri kabisa ni kwamba kwa kauli zao inawezekana wanataka kumdhuru Lissu kutokana na misimamo yake!