Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
CCM wanaswa wakinunua shahada - Tanzania Daima
Wakutwa nazo 180
WAKATI juhudi za kuliokoa Jimbo la Bukombe ambalo liko katika hatihati za kunyakuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) zikipamba moto, viongozi wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa wakinunua shahada kutoka kwa wapiga kura.
Habari kutoka Bukombe ambazo zimethibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Selemani Nyakipande, zinasema viongozi hao ni Juma Mhoja na Shadrack Paul, ambao ni makatibu wa Tawi la Ushirombo na Msonga.
Alisema viongozi hao walikamatwa katika Kijiji cha Msonga, Kata ya Runzewe, wakiwa tayari wamenunua shahada 185 za kupigia kura kutoka kwa wananchi ambao walikuwa wanarubuniwa na baadhi ya makada wa CCM ambao wako katika mkakati wa kuliokoa jimbo hilo.
Viongozi hao walikuwa wakinunua shahada hizo kwa bei kati ya sh 2,000 na 5,000 huku lengo kuu likionekana kuwalenga zaidi wafuasi wa CHADEMA ili kudhoofisha nguvu iliyopo.
Kamanda Nyakipande alisema polisi inaendelea kuwafanyia uchunguzi watuhumiwa hao kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kwa madai kuwa tukio hilo linaingiliana na Sheria ya Gharama za uchaguzi.
Hali ya kisiasa katika jimbo hilo ni tete kutokana na upinzani mkali uliopo kati ya CCM na CHADEMA, sababu kubwa ni kutokana na kuwapo makundi, baada ya kura za maoni zilizoibua malalamiko mengi.
Huko Zanzibar, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Sophia Simba, amewakoromea wanachama wa CCM wanaoendeleza makundi kutokana na chuki za kuanguka kwenye uchaguzi kuwa ni washamba wa siasa.
Hayo ameyaeleza alipokuwa akizungumza na wanachama wa umoja huo, Tawi la CCM Kizimbani katika Jimbo la Dole, Wilaya ya Magharibi Unguja, akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ushindi kwa CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Aliwataka wanachama wa CCM kuvunja kambi zao na kujenga umoja ili kuhakikisha chama hicho kinaibuka na ushindi mkubwa Tanzania Bara na Zanzibar katika ngazi zote, kuanzia urais hadi udiwani.
Alisema UWT taifa tayari imeshajipanga katika mikoa, wilaya, majimbo hadi katika wadi zote na wanachama wa CCM wahakikishe ushindi katika ngazi zote.
Alisema baada ya kumalizika kura ya maoni na wagombea kupatikana, pande zilizokuwa zikipingana zilitakiwa zivunje kambi, lakini kuna baadhi ya wanachama hadi sasa wanaendeleza tofauti zao kwa kukosa ukomavu wa kisiasa.
Alisema wapo wagombea walioshindwa kwa kura nyingi katika mchakato wa kura za maoni, ambao hadi sasa wanakataa kuwaunga mkono wale walioibuka washindi.
Alisema ni kitendo cha kusikiktisha kuona wanachama hao wanatumia hata udini na ukabila, vitendo ambavyo ni sumu katika kudumisha umoja wa kitaifa ulioasisiwa na marehemu Mwalimu Julius Nyerere na mzee Abeid Aman Karume.
Aliwataka wagombea waliopitishwa kuwania nafasi mbalimbali wajenge ushirikiano wa karibu na wenzao ambao walianguka na kuhakikisha chama hicho kinafikia malengo yake.
CCM inatupeleka wapi ? Piga, ua na galagaza, ushindi ni lazima yasema CCM !
Tanzania kweli twahitaji ukombozi