CCM wanasababisha umasikini kwa makusudi

Kessy Wa Kilimanjaro

JF-Expert Member
Jan 23, 2016
327
208
Tangia uhuru wa Tanzania tumepewa msaada wa zaidi ya mabilioni ya dolla za kimarekani ili kujenga nchi yetu. Je hiyo hela imeenda kwenye kujenga barabara ambazo magari yanaanguka kwenye mashimo kila siku, au kwenye kununua madawati ambayo yanakosekana, au hiyo hela imeenda kwenye kununua vitanda muimbili, au imeenda kwenye kukuza elimu ambayo kwenye kusoma tuko namba 82 kati ya 112, au hiyo hela imeenda kwenye kusaidia vijiji ambavyo bado vinaishi kwenye nyumba za matope.

Lakini ambacho kinashangaza ni kwamba bado hawa wanasiasa na viongozi wana hamu ya kupendekeza sera ambazo zinazidi kuwafukuza wafanya biashara, kufanya uwekezaji wa wamaskini kwenye biashara uwe mgumu, kuongeza kodi, kuongeza wizara, kuongeza sheria kwenye uwekezaji, kuongeza leseni zinazohitajika kuanzisha biashara, kuongeza vikwazo kwenye mabenki na maisha ya watu binafsi.

hivi kweli hawa viongozi wetu wanajidai kama hawajui madhara ya wanachofanya?

Ukweli ni kwamba wanajua na wanafanya maksudi. Sababu ni kwamba wanapenda urahisi wa hela za misaada. Hela za misaada zinakuja pale kukiwa na shida. Sasa fikiria, hawa viongozi wangetumia mbinu ambazo wanajua zinaleta mazao na zimeonyesha kuleta maendeleo kwenye nchi zingine, na wangejenga uchumi kwenye kiwango cha kupunguza umaskini mpaka wale wanaotuma misaada wakaona hamna haja tena, si watakuwa wanajiharibia utajiri wao wenyewe. Misaada ingeanza kupungua na wao wangeshindwa kuiiba na kuificha kwenye account swiss bank account zao. Kama hamniamini waulizeni viongozi wenu kwanini tusiache kuchukua misaada utaona watakavyo badilika sura kama umewatukana.
 
Du hata mfuasi mmoja wa CCM hajaja? Itakuwa sina umaarufu au JF inaificha uzi wangu kutoonekana.
Umesema kweli Kessy.
Wadanganyika ni kondoo..hawahoji, hawadadisi. CCM imeshawafanya wadanganyika kuwa ni kichwa cha mwendawazimu.
Nimesoma sehemu nyingi, msajili wa vyama vya siasa anashauriwa akifute hiki chama cha kuwagawia umasikini wadanganyika lakini inaonekana ana masilahi binafsi na hana huruma na walalahoi milioni 40+.

Nchi inafanya usanii na igizo la uchaguzi ili kumsimika madarakani mccm mmoja ili aje awatumbue na awahadae wadanganyika kwa kauli mbiu zilizopakwa asali.

Wakishakupokezana kijiti kama wanavyosema wenyewe, wanasema bila kuona aibu, kazeni mikanda, wakisoma hiyo wanayoiita bajeti, wanataka fedha yote ya mlalahio aitoe sadaka kupitia kodi.

Wewe unasema misaada, ninachojua mimi kama wanapewa misaada ya bure basi deni la Taifa linaongezeka maradufu. Hakuna cha maana kinachoonekana wanafanya, wanachojua ni kuongeza ugumu wa maisha tu kwa wadanganyika na walalahoi.

Hawa wanaojitwalia madaraka ya kuongoza nchi hii sijui kama wanaamini uwepo wa Mungu. Wanawezaje kuwafanya watu wanaowaongoza( wanaowatawala) wawe mafukara na masikini duni kabisa wakati nchi imejaa rasilimali na mali ghafi. Viongozi wa nchi hii wana roho mbaya kweli, wanajali matumbo yao tu.

Na ukondoo wetu ndio unawapa kiburi watawala.
 
Mi sijawaji kusikia Ukawa wahamasishe wananchi walime ili wajipatie chakula, au kuhamasisha wananchi kufanya shughuri za kuongeza kipato ili wajikwamue kimaisha. Kila kukicha ni kuhamasisha migomo na maandamano, je maandamano yanaondoa umaskini? Mi naona ingekuwa kweli Ukawa wanapenda watanzania waondokane na umaskini wangehimiza watu wafanye shughuri za maendeleo majimboni kwao ili kuondoa umaskini, ifike wakati sasa tufanye siasa zenye tija kwa wananchi, si siasa hizi za sungura na fisi
 
Mi sijawaji kusikia Ukawa wahamasishe wananchi walime ili wajipatie chakula, au kuhamasisha wananchi kufanya shughuri za kuongeza kipato ili wajikwamue kimaisha. Kila kukicha ni kuhamasisha migomo na maandamano, je maandamano yanaondoa umaskini? Mi naona ingekuwa kweli Ukawa wanapenda watanzania waondokane na umaskini wangehimiza watu wafanye shughuri za maendeleo majimboni kwao ili kuondoa umaskini, ifike wakati sasa tufanye siasa zenye tija kwa wananchi, si siasa hizi za sungura na fisi
Unajua maana ya UKAWA?
UKAWA ni nani?
Msajili wa vyama vya siasa amesajili UKAWA?
UKAWA imeundwa lini?
CCM je iliundwa lini?
CCM inajitawalisha nchi hii tangia lini? 1977 -2016?
 
Mi sijawaji kusikia Ukawa wahamasishe wananchi walime ili wajipatie chakula, au kuhamasisha wananchi kufanya shughuri za kuongeza kipato ili wajikwamue kimaisha. Kila kukicha ni kuhamasisha migomo na maandamano, je maandamano yanaondoa umaskini? Mi naona ingekuwa kweli Ukawa wanapenda watanzania waondokane na umaskini wangehimiza watu wafanye shughuri za maendeleo majimboni kwao ili kuondoa umaskini, ifike wakati sasa tufanye siasa zenye tija kwa wananchi, si siasa hizi za sungura na fisi
Link Duru za siasa: Ndani ya Bunge
 
Mi sijawaji kusikia Ukawa wahamasishe wananchi walime ili wajipatie chakula, au kuhamasisha wananchi kufanya shughuri za kuongeza kipato ili wajikwamue kimaisha. Kila kukicha ni kuhamasisha migomo na maandamano, je maandamano yanaondoa umaskini? Mi naona ingekuwa kweli Ukawa wanapenda watanzania waondokane na umaskini wangehimiza watu wafanye shughuri za maendeleo majimboni kwao ili kuondoa umaskini, ifike wakati sasa tufanye siasa zenye tija kwa wananchi, si siasa hizi za sungura na fisi
Mbona ccm miaka 50 umasikini umewashinda? Acha ukawa wauseme ukweli.
 
Umesema kweli Kessy.
Wadanganyika ni kondoo..hawahoji, hawadadisi. CCM imeshawafanya wadanganyika kuwa ni kichwa cha mwendawazimu.
Nimesoma sehemu nyingi, msajili wa vyama vya siasa anashauriwa akifute hiki chama cha kuwagawia umasikini wadanganyika lakini inaonekana ana masilahi binafsi na hana huruma na walalahoi milioni 40+.

Nchi inafanya usanii na igizo la uchaguzi ili kumsimika madarakani mccm mmoja ili aje awatumbue na awahadae wadanganyika kwa kauli mbiu zilizopakwa asali.

Wakishakupokezana kijiti kama wanavyosema wenyewe, wanasema bila kuona aibu, kazeni mikanda, wakisoma hiyo wanayoiita bajeti, wanataka fedha yote ya mlalahio aitoe sadaka kupitia kodi.

Wewe unasema misaada, ninachojua mimi kama wanapewa misaada ya bure basi deni la Taifa linaongezeka maradufu. Hakuna cha maana kinachoonekana wanafanya, wanachojua ni kuongeza ugumu wa maisha tu kwa wadanganyika na walalahoi.

Hawa wanaojitwalia madaraka ya kuongoza nchi hii sijui kama wanaamini uwepo wa Mungu. Wanawezaje kuwafanya watu wanaowaongoza( wanaowatawala) wawe mafukara na masikini duni kabisa wakati nchi imejaa rasilimali na mali ghafi. Viongozi wa nchi hii wana roho mbaya kweli, wanajali matumbo yao tu.

Na ukondoo wetu ndio unawapa kiburi watawala.
Nchi haitajengwa na viongozi uchwara.
Nchi haitajengwa na sera uchwara za uchumi,
Nchi haitajengwa na siasa uchwara,
Nchi haitajengwa na watu wasiopenda demokrasia.
 
Umesema kweli Kessy.
Wadanganyika ni kondoo..hawahoji, hawadadisi. CCM imeshawafanya wadanganyika kuwa ni kichwa cha mwendawazimu.
Nimesoma sehemu nyingi, msajili wa vyama vya siasa anashauriwa akifute hiki chama cha kuwagawia umasikini wadanganyika lakini inaonekana ana masilahi binafsi na hana huruma na walalahoi milioni 40+.

Nchi inafanya usanii na igizo la uchaguzi ili kumsimika madarakani mccm mmoja ili aje awatumbue na awahadae wadanganyika kwa kauli mbiu zilizopakwa asali.

Wakishakupokezana kijiti kama wanavyosema wenyewe, wanasema bila kuona aibu, kazeni mikanda, wakisoma hiyo wanayoiita bajeti, wanataka fedha yote ya mlalahio aitoe sadaka kupitia kodi.

Wewe unasema misaada, ninachojua mimi kama wanapewa misaada ya bure basi deni la Taifa linaongezeka maradufu. Hakuna cha maana kinachoonekana wanafanya, wanachojua ni kuongeza ugumu wa maisha tu kwa wadanganyika na walalahoi.

Hawa wanaojitwalia madaraka ya kuongoza nchi hii sijui kama wanaamini uwepo wa Mungu. Wanawezaje kuwafanya watu wanaowaongoza( wanaowatawala) wawe mafukara na masikini duni kabisa wakati nchi imejaa rasilimali na mali ghafi. Viongozi wa nchi hii wana roho mbaya kweli, wanajali matumbo yao tu.

Na ukondoo wetu ndio unawapa kiburi watawala.

Ukondoo unaishaga kondoo akiona majani yameisha. Kondoo atamkimbia mchungaji wake ili ale. Huo mda unakuja we ngoja.
Cha kwanza kilikua upungufu wa sukari kama utani vile. Cha pili bidhaa bandarini kupungua. Cha tatu biashara na mabenki yanakufa. Cha nne mikopo ikipotea kwenye sekta ya kilimo, ukame utafwata. Cha tano inflation na hela itakua kama ya zimbabwe. Hapo ndipo kondoo watageuka kuwa mbuzi.
 
Mi sijawaji kusikia Ukawa wahamasishe wananchi walime ili wajipatie chakula, au kuhamasisha wananchi kufanya shughuri za kuongeza kipato ili wajikwamue kimaisha. Kila kukicha ni kuhamasisha migomo na maandamano, je maandamano yanaondoa umaskini? Mi naona ingekuwa kweli Ukawa wanapenda watanzania waondokane na umaskini wangehimiza watu wafanye shughuri za maendeleo majimboni kwao ili kuondoa umaskini, ifike wakati sasa tufanye siasa zenye tija kwa wananchi, si siasa hizi za sungura na fisi

sasa ndiyo nikwambie watu wanataka kufanya hizo shughuri hata sasa tunavyoongea. Lakini hao watu hawana mapato wala hela au mali ya kuwawezesha kuchukulia mikopo. Juu ya hayo kuanzisha hizo biashara wanazotaka kuanzisha wanahitaji kupitia usajiri wa kupata leseni chungu mzima ambao mtu wakawaida han uwezo huo. Juu ya hilo wanahitaji kulipa kodi zilizoongezwa mpaka mtu hapati faida wala hela ya kukuza biashara. Alafu akiangalia serikali yake inamwambia wanataka kujenga viwanda. Ivi kweli huo siyo uovu jamani?

Na haijalishi Iwe CCM au UKAWA mimi naona wote tu ni sawa kwasababu wote ni wanasiasa wa kiafrika na kama wanasiasa wa kiafrika wanachotaka ni kitu kile kile.
 
Tatizo CCM wanajifanya wanakurupuka sasa hv baada ya kupata mtikisiko wa Chama katika uchunguzi uliopita.
Sasa wanataka kutekeleza mambo mengi makubwa ambayo walitakiwa kuyafanya mapema.
Sasa presha zao zinakuja kutuumiza sisi wananchi ambao hatuna makosa.
Wao ndio walio sababisha sisi kuwa katika hali mbaya Inabidi wawajibike kwa uzembe huu.
 
Kama chadema wanapotumia mabilioni kuandamana nchi nzima ,lkn wakiambiwa jengeni ofisi ya chama, wanasema hatuna hela.!!!
 
Chadema hawa dola wewe una dola watu wako masikini wa kutupwa miaka 50 ya Uhuru aibu kubwa hata Mh.Rais amesema nchi ni Tajiri mbona watu wake masikini?
 
UKAWA mbona hamuhamasishi maendeleo?? Kila siku kuandamana tu!!

Cha kwanza unawajumlisha wote waliopo ukawa na unafikiri kwamba wote hawahamasishi maendeleo. Hilo unajuaje. Hivi hata watu waliopo ukawa unajuaje ni wangapi? Je unaweza kutaja hata vyama vyote vya ukawa? Come on man be realistic.
 
Tatizo CCM wanajifanya wanakurupuka sasa hv baada ya kupata mtikisiko wa Chama katika uchunguzi uliopita.
Sasa wanataka kutekeleza mambo mengi makubwa ambayo walitakiwa kuyafanya mapema.
Sasa presha zao zinakuja kutuumiza sisi wananchi ambao hatuna makosa.
Wao ndio walio sababisha sisi kuwa katika hali mbaya Inabidi wawajibike kwa uzembe huu.

yani ndo wanafanya damage control sasahivi. Wameona approve yao imeshuka na nchi haiwataki tena na hata kura zenyewe sijui wamezipataje hayo anajua mungu lakini kama wameiba ushindi basi wanajidanganya wenyewe kama wanafikiri huo ni ubabe. Miaka 55 ya CHAMA CHA MAFISADI
 
Ndg yangu lupyee wote ni wana CCM, lkn mambo mengine yanatuangusha. Hata ofis yetu ya Lumumba tunayolingia hatukujenga km CCM, bali tulirithi. Kumbuka pale ilikua kitivo cha Sheria cha UDSM. Hawa wapinzani wakichachama sisi hatuna ofisi wala viwanja vya michezo
 
Chadema hawa dola wewe una dola watu wako masikini wa kutupwa miaka 50 ya Uhuru aibu kubwa hata Mh.Rais amesema nchi ni Tajiri mbona watu wake masikini?

Nchi siyo tajiri. Nini kinaifanya nchi iwe inaitwa tajiri. Hivi ni kuwa na madini, au gesi, au mabwawa, au wanyama au ardhi au hali ya hewa nzuri? Mbona hivyo vyote south Korea hawana na Uchumi wao ni mara mia kupita wetu, shule zao ni mara elfu kupita zetu na hali ya maisha hata hauwezi kuifananisha na nchi yetu. Lakini ukiangalia kwenye business freedom yao wamepata ranking nzuri in asia na unimployment yao iko kwenye 3.5% na kodi zao ziko chini.

Msijidanganye nchi hiko tajiri. Utajiri unatokana na wananchi na uhuru na uwezo wao ziyo vijiwe vilivyoko kwenye udongo au mafuta na gesi iliyoko kwenye ardhi.
 
Back
Top Bottom