mamayoyo1
JF-Expert Member
- Jul 25, 2018
- 1,011
- 1,019
Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amemtumia salamu Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) kuwa akae mkao wa kula katika Jimbo analoliongoza.
Dkt. Bashiru kuelekea uchaguzi Mkuu amesema hakuna uchawi, wizi, kupendelea huku akiwataka waache visingizio wachape kazi.
"Bwana Sugu kaa mkao wa kula nakuja kwako hakuna uchawi kuna kazi, hakuna sijui wizi sijui kupendelewa acheni visingizio," alisema Dkt, Bashiri akiwa Dodoma.
"Chapa kazi ya siasa mpate dawa yenyewe iingie mpone hiyo ndio CCM mpya lakini ni vizuri tukahamasisha Watanzania wengi kushiriki katika uchaguzi ikiwezekana wote wenye umri wa kupiga kura."