Kwa kweli namna katiba inavyovurugwa ni wazi kabisa Chama cha Mapinduzi kimeshaivuruga nchi na sasa, na sasa kila mmoja anaongoza kivyakevyake, msemo wa Kiswahili maarufu ule usemao mwenye nguvu mpishe, ndio tunaokwenda nao sio tena kufuata ule msemo wa Uongozi ni dhamana.
Mnavuruga Katiba ya nchi halafu mnaonekana hamjali kabisa, mnaonyesha kiburi waziwazi.
Mtiririko huu unaanthiri nyanja zote za utendaji kazi serikalini maana mahakama haki itapotea watafanya na kuamua wanavyotaka, polisi nao watafanya wanavyotaka kwani CCM hawezi kuwakemea tena polisi sababu polisi ndio walinzi wa masanduku ya kura za wizi na walazimishaji wa kuwaondoa mawakala, majeshi watafanya wanavyotaka maana na wao ndio wanaolinda misafara ya viongozi wa serikali ya CCM na unaweza kuona muendelezo huo kama hayo ya mabenki kuchotwa hela yote ni mataputapu yanayosababishwa na uvunjwaji wa katiba. Spika wa bunge naye anafanya anavyotaka kila kitu kinaonekana kimevugwa.
Huwa nikikaa nawaza na kujisemea pamoja na kujiuliza. Je, Tanzania tunaelekea kuwa kama zile nchi zenye mapigano yasiokwisha kwa kweli ninakuwa na masuali mengi ya kuona tunaondoka taratibu kwenye lile hekalu la amani na utulivu.
Kuna tabu gani ya kufuata Katiba na kila mmoja akafanya wajibu wake kutoka katika miongozo iliyomo ndani ya Katiba na yakitokea malalamiko wananchi wanalalamika Katiba imevunjwa ni wajibu wa serikali kujitokeza haraka kuivunja hoja hio kwa miongozo inayoeleweka na sio majibu ya papo kwa papo.
Kuna watu wanasema Rais Samia amevunja au anavunja katika kwani mawaziri waliopo hawakula kiapo kwake yeye ni Rais mpya kama atateua wapya au walewale basi awatayarishie siku awaapishe.
Kama Tanzania tuiweke kwenye umbo la meli basi naona kama kamba ya nanga inaelekea kukatika.
Mnavuruga Katiba ya nchi halafu mnaonekana hamjali kabisa, mnaonyesha kiburi waziwazi.
Mtiririko huu unaanthiri nyanja zote za utendaji kazi serikalini maana mahakama haki itapotea watafanya na kuamua wanavyotaka, polisi nao watafanya wanavyotaka kwani CCM hawezi kuwakemea tena polisi sababu polisi ndio walinzi wa masanduku ya kura za wizi na walazimishaji wa kuwaondoa mawakala, majeshi watafanya wanavyotaka maana na wao ndio wanaolinda misafara ya viongozi wa serikali ya CCM na unaweza kuona muendelezo huo kama hayo ya mabenki kuchotwa hela yote ni mataputapu yanayosababishwa na uvunjwaji wa katiba. Spika wa bunge naye anafanya anavyotaka kila kitu kinaonekana kimevugwa.
Huwa nikikaa nawaza na kujisemea pamoja na kujiuliza. Je, Tanzania tunaelekea kuwa kama zile nchi zenye mapigano yasiokwisha kwa kweli ninakuwa na masuali mengi ya kuona tunaondoka taratibu kwenye lile hekalu la amani na utulivu.
Kuna tabu gani ya kufuata Katiba na kila mmoja akafanya wajibu wake kutoka katika miongozo iliyomo ndani ya Katiba na yakitokea malalamiko wananchi wanalalamika Katiba imevunjwa ni wajibu wa serikali kujitokeza haraka kuivunja hoja hio kwa miongozo inayoeleweka na sio majibu ya papo kwa papo.
Kuna watu wanasema Rais Samia amevunja au anavunja katika kwani mawaziri waliopo hawakula kiapo kwake yeye ni Rais mpya kama atateua wapya au walewale basi awatayarishie siku awaapishe.
Kama Tanzania tuiweke kwenye umbo la meli basi naona kama kamba ya nanga inaelekea kukatika.