Matukio mengie yametokea siku za hivi karibuni kwenye siasa za nchi yetu. Nadhani tukio kubwa ninalokumbuka ni lile la CCM kujivua gamba kwa kuwaondoa madarakani akina Yusufu MAKAMBA na kuweka damu mpya ya akina January MAKAMBA.
Je ni kweli sasa CCM siyo nyoka tena bali sasa amekuwa ni mjusi tu asiyekuwa na madhara kwa watanzania tena? Swali hilo ndio sijaweza kulijibu; na ndiyo maana naanzisha thread hii ili baada ya wiki moja niweza kufahamu kama kweli magezui yaliyofanyika ndani ya CCM ni ya kweli au ni danganya toto tu. jambo moja linalokera zaidi ni kuwa gamba lililovuliwa na CCM ni lile la ufisadi, ambalo kwa mujibu wa sheria za nchi ni kosa la jinai. Je ni kweli mafisadi waliovuliwa CCM watafikishwa kwenye vyombo vya sheria; yaani kuna anayeweza kuniaminisha kuwa Januari atamfikisha Yusufu kwenye vyombo vya sheria ili hali Januari huyo amefika hapo kupitia mgongo wa Yusufu?
Nadhani bado tunaishi na nyoka uvunguni mwetu; wakati wowote atatung'ata tu!!
Mungu katika Jina la Yesu atamlinda Nape. Hakuna atakayemgusa kwa kuwa Malaika wa Mungu aliyehai wanaomlinda ni wengi kuliko Majini yatakayotumwa na wabaya wake ili kumdhuru.
Mungu aendelee kumlinda Nape Nnauye.
yawezekana uko sahihi kwamba kilichofanyika ni maigizo tu.lakini jaribu kuelezea falsafa hii ambayo jk aliisema kabla ya mabadiliko ya kamati kuu hivi karibuni ilimaanisha nini?Hakuna gamba lolote lililovuliwa, ni maigizo tuu yaliyolenga kufanikisha harakati zao za kuteka imani ya watanzania!..
kwa hiyo walichohitaji ni 'kujisafisha' na sio kulivua gamba?ccm hawakua na GAMBA bali ule ni UKURUTU
Matukio mengie yametokea siku za hivi karibuni kwenye siasa za nchi yetu. Nadhani tukio kubwa ninalokumbuka ni lile la CCM kujivua gamba kwa kuwaondoa madarakani akina Yusufu MAKAMBA na kuweka damu mpya ya akina January MAKAMBA.
Je ni kweli sasa CCM siyo nyoka tena bali sasa amekuwa ni mjusi tu asiyekuwa na madhara kwa watanzania tena? Swali hilo ndio sijaweza kulijibu; na ndiyo maana naanzisha thread hii ili baada ya wiki moja niweza kufahamu kama kweli magezui yaliyofanyika ndani ya CCM ni ya kweli au ni danganya toto tu. jambo moja linalokera zaidi ni kuwa gamba lililovuliwa na CCM ni lile la ufisadi, ambalo kwa mujibu wa sheria za nchi ni kosa la jinai. Je ni kweli mafisadi waliovuliwa CCM watafikishwa kwenye vyombo vya sheria; yaani kuna anayeweza kuniaminisha kuwa Januari atamfikisha Yusufu kwenye vyombo vya sheria ili hali Januari huyo amefika hapo kupitia mgongo wa Yusufu?
Nadhani bado tunaishi na nyoka uvunguni mwetu; wakati wowote atatung'ata tu!!