Ufunuo wa Yohana
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 319
- 70
ANGALIA JINSI MUNISHI ANAVYOPAMBANA NA CCM!!
"CCM Wakiniua, Mnizike Kenya." Asema Munishi. "Siyo kwamba nimebadili uraia, wala sitarajii kufanya hivyo.Mimi bado ni Mtanzania. Sikuchagua kuzaliwa Tanzania, lakini nitachagua pa kuzikwa.Serikali za CCM zimenifanya nisiwe na mahali ninapoweza kupaita nyumbani ndani ya nchi yangu. Kosa langu ni kusema CCM sera zake zimeiharibu Tanzania, na hawafai kuwa madarakani.Makachero wa Tanzania wamekuwa wakitumia kila mbinu chafu kuwasumbua na hata kuwaua wote walio na uhusiano wa karibu na Munishi. Ajabu ni kwamba Munishi mwenyewe akienda Tanzania wanafuatilia nyendo zake bila kutishia kumuua. Akiwa Kenya ambako ndipo sanaa yake ilimpatia uwezo wa kununua nusu ekari ambapo amejenga nyumba ya mabati kujisitiri na jamii yake, bado makachero hawaishi kumvamia kama majambazi, na kutishia kumuua. Munishi akiwaeleza wanahabari kwamba wavamizi walidai kutumwa, wao wanaandika kwamba ni majambazi wa kawaida. Walijuaje kama ni majambazi wa kawaida? Tena wangejuaje kwamba siyo majambazi wa kawaida? Basi kwa nini waandike ni majambazi wa kawaida? Mbaya zaidi wanasema Munishi ndiye aliyewaambia wakati sivyo. Mtu akikuuliza je! unaona waliokuvamia kama ni washindani wako kibiashara? Na jibu likawa ni vigumu kujua kwa hakika wavamizi wangu ni kina nani, Lakini walidai kutumwa na watu ambao hawakuwataja. Je hapo utakuwa umesema kwamba majambazi hawakuwa washindani wangu kibiashara bali ni wa kawaida? NATION wanapaswa mara moja kumjibu Munishi kwani mahojiano aliyanakili kwenye simu yake
Serikali ya Mkapa Tanzania inaamini kwamba Munishi na nyimbo zake ni mwanzo wa kuvurugika kwa amani Tanzania. Kinyume chake ndio sahihi. Amani ilivurugika pale Mkapa alipowaamuru Polisi wawaue Wazanzibari zaidi ya 70 kwa sababu za kisiasa. Majeshi Tanzania walikasirishwa sana na jambo hilo,na walikuwa tayari kuipindua serikali ya Mkapa. Munishi akaimba wimbo "MPENDE ADUI YAKO", Mkapa badala ajue kwamba wimbo huo ulikuwa ukimsaidia yeye ili serikali yake isipinduliwe na kisha afunguliwe mashitaka ya kuwaua raia wasio na hatia, Aliupiga marufuku wimbo huo na kuamuru polisi wamsake Munishi. Iko siku Mkapa atamkumbuka Munishi. Ngoja kipindi chake cha urais kimalizike, na tunaomba kimalizike salama, halafu Mkapa awe raia wa kawaida. Kombe aliyemwamuru amsake Munishi, ndiye atakayeamriwa amtie Mkapa mbaroni ili ajibu mashitaka ya kuua na kupora mali ya umma pamoja na kuiuza nchi kwa makaburu
"CCM Wakiniua, Mnizike Kenya." Asema Munishi. "Siyo kwamba nimebadili uraia, wala sitarajii kufanya hivyo.Mimi bado ni Mtanzania. Sikuchagua kuzaliwa Tanzania, lakini nitachagua pa kuzikwa.Serikali za CCM zimenifanya nisiwe na mahali ninapoweza kupaita nyumbani ndani ya nchi yangu. Kosa langu ni kusema CCM sera zake zimeiharibu Tanzania, na hawafai kuwa madarakani.Makachero wa Tanzania wamekuwa wakitumia kila mbinu chafu kuwasumbua na hata kuwaua wote walio na uhusiano wa karibu na Munishi. Ajabu ni kwamba Munishi mwenyewe akienda Tanzania wanafuatilia nyendo zake bila kutishia kumuua. Akiwa Kenya ambako ndipo sanaa yake ilimpatia uwezo wa kununua nusu ekari ambapo amejenga nyumba ya mabati kujisitiri na jamii yake, bado makachero hawaishi kumvamia kama majambazi, na kutishia kumuua. Munishi akiwaeleza wanahabari kwamba wavamizi walidai kutumwa, wao wanaandika kwamba ni majambazi wa kawaida. Walijuaje kama ni majambazi wa kawaida? Tena wangejuaje kwamba siyo majambazi wa kawaida? Basi kwa nini waandike ni majambazi wa kawaida? Mbaya zaidi wanasema Munishi ndiye aliyewaambia wakati sivyo. Mtu akikuuliza je! unaona waliokuvamia kama ni washindani wako kibiashara? Na jibu likawa ni vigumu kujua kwa hakika wavamizi wangu ni kina nani, Lakini walidai kutumwa na watu ambao hawakuwataja. Je hapo utakuwa umesema kwamba majambazi hawakuwa washindani wangu kibiashara bali ni wa kawaida? NATION wanapaswa mara moja kumjibu Munishi kwani mahojiano aliyanakili kwenye simu yake
Serikali ya Mkapa Tanzania inaamini kwamba Munishi na nyimbo zake ni mwanzo wa kuvurugika kwa amani Tanzania. Kinyume chake ndio sahihi. Amani ilivurugika pale Mkapa alipowaamuru Polisi wawaue Wazanzibari zaidi ya 70 kwa sababu za kisiasa. Majeshi Tanzania walikasirishwa sana na jambo hilo,na walikuwa tayari kuipindua serikali ya Mkapa. Munishi akaimba wimbo "MPENDE ADUI YAKO", Mkapa badala ajue kwamba wimbo huo ulikuwa ukimsaidia yeye ili serikali yake isipinduliwe na kisha afunguliwe mashitaka ya kuwaua raia wasio na hatia, Aliupiga marufuku wimbo huo na kuamuru polisi wamsake Munishi. Iko siku Mkapa atamkumbuka Munishi. Ngoja kipindi chake cha urais kimalizike, na tunaomba kimalizike salama, halafu Mkapa awe raia wa kawaida. Kombe aliyemwamuru amsake Munishi, ndiye atakayeamriwa amtie Mkapa mbaroni ili ajibu mashitaka ya kuua na kupora mali ya umma pamoja na kuiuza nchi kwa makaburu