CCM wakiandamana watakuwa wanahalisha Uchakachuaji

mzozaji

JF-Expert Member
Jul 28, 2010
255
13
Kuna tetesi kuwa washabiki na wanachama wa CCM wanapanga kuandamana kulaani wabunge wa CHADEMA kutoka Bungeni wakati Mwenyekiti wao alipokuwa anahutubia. Hii inaonyesha wazi kuwa sasa imefikia hatua watu wanataka kukwepa hoja ya msingi ambayo ni uchakachuaji wa matokeo ya Uraisi na kutaka wanaolaani mtindo mzima wa uchakachuaji waonekane 'wabaya' wakati ni sehemu ya Demokrasia kupinga matokeo yale. Nadhani watakuwa na busara zaidi kama wakijibu hoja ya msingi kuliko kukoleza mambo kwa kuzusha mengine zaidi.
 
UKIONA TWIGA ANAANZA KULA MAJANI YA CHINI UJUE JUU YA MTI KUMETANDA JOKA KUBWA

Nakuambia WANADEMOKRASIA na WANADIPLOMASIA ambao siku zote wana ufuhamu mkubwa na mambo mengi mno duniani, WANAELEWA FIKA MAANA YA UJUMBE waliutuma wana-CHADEMA kule Dodoma. Na kwa kitendo hicho, utawala DHALIMU utaanza kumomonyoka kama nyumba ya karata. Mtu kashikwa pabaya hapa!!!

Itakua ni kosa kubwa CCM kwenda Barabarani kwa siku yoyote ile. Kwani, wakitangulia huko barabarani kwenda kudai HAKI huko, basi ninauhakika kwamba CHADEMA na wale wapiga kura 15 milioni ndio haswa WATAMALIZIA KABISA picha zima. Kamanda Kombe, tayarisha vijana zaidi na barabara zote ziwe wazi kupitika na WADAI HAKI tu.

Ila, kwa UTULIVU mkubwa ambao Wa-Tanzania wameonyesha na kuendelea na michakato mbali mbali za kuleta MABADILIKO ya kweli TAnzania mpaka sasa inatoa TASWIRA zifyatazo:


1. Wameamua kuwapa WALIOWAPOKONYA HAKI yao Adhabu isiyokifani Kisaokolojia akilini. Hii na silaha hatari mno wailoutumia wananchi.


2. Wanatuma pia UJUMBE MZITO kimataifa ya kwamba nyuma ya UKIMYA WAO HUU, licha ya rais kupatikana kwa kura CHINI ya ROBO ya wote waliojiandikisha kufanya hivyo, kwamba Jumuiya ya Kimataifa ITUMIE AKILI kubanini kwamba kuna UDIKTETA wa ajabu uliofichama ndani ya NEMBO ya AMANI tuliyonayo Tanzania kwa miaka mingi sasa LAKINI BILA HAKI YA KUTOFAUTIANA na uongozi kwenye FIKRA na MAONI. Na Kwamba, wengi sasa tu (hadi wa ngazi za Maprofesa) WAMEPOTEZWA KIMYA KIMYA GIZANI kwa kuthubutu kufanya hivyo.


3. Pia, kwa ukimya huu Wa-Tanzania wameamua KUMNYIMA KAKA MBABE fursa ya kutumia DOLA kuwarudi.
 
Waache waandamane,Lakini wajue kuwa wananchi wanaelewa nini kilitokea katika uchaguzi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom