CCM wajikoroga tena, wanatambua uwepo wa Tanganyika kwenye sherehe tu siyo kikatiba!

Makala Jr

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
3,395
1,110
Katika kile ambacho Mwanafalsafa Andrew Carnegie anakitambua kama, "Uncontrolled desire for something for nothing" viongozi wa Chama Cha Mapinduzi akiwemo Mwenyekiti wake kitaifa Mhe.Dr.Jakaya Kikwete wameonesha kukosa mantiki ya msimamo wao kuhusu haja ya kutambua kikatiba uwepo wa Tanganyika iliyoungana na Zanzibar mnamo mwaka tar.26.04.1964.

CCM ndicho chama pekee kilichoshindwa kutoa mwelekeo sahihi kuhusu aina ya muungano unaotakiwa kwa sasa na haja ya uwazi wa mambo yahusuyo Tanganyika.

CCM wamekuwa mstari wa mbele katika sherehe mathalani kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika ambayo wanapinga uwepo wake kinyume na ilivyopendekezwa na tume ya uundaji wa katiba mpya chini ya Mzee Sinde J.Warioba.

Mara kadhaa viongozi wa CCM akiwemo Mzee Abdallah Bulendo wamemkashifu Mzee Warioba kwa kukubali muungano wa serikali tatu ikiwamo Tanganyika.

Hoja ipo wazi, bajeti ya sherehe ya uhuru iligharamiwa na nani hali Tanganyika haina serikali?
 
Vituko vyao eti wanasema uhuru wa Tanzania Bara does it make any sense historia ni historia tu waache wazimu waseme uhuru wa Tanganyika
 
Ngalele Fijo; Bila shaka wamepoteza mwelekeo, watuambie ni lini wabunge/mawaziri walikaa kujadili na kupitisha bajeti ya maendeleo kwa masuala yale yasiyo ya muungano kwa ajili ya Tanganyika?
 
Last edited by a moderator:
NI ujinga kwamba unaweza ua Tanganyika ukweli ni kwamba historia huwa haifi wakubaliane na ukweli Tanganyika will ever ring into our minds the only option is to deal with it , The Great Tanganyika
 
Nilimsikia katika hutoba JK anavyobabaika!...Uhuru wa Tanzania, Uhuru wa Tanzania Bara, Uhuru wa Tanganyika?
 
Tanganyika ikiitwa Tanzania Bara huwa najisikia kichefuchefu kabisa.
 
Subirini rasimu ya katiba itoke, watanyoosha maelezo, wamemkolimba dr.mvungi akajipongeza walidhani wamemaliza kazi.Tanganyika lazima si ombi tena
 
Ujinga tu hapo no sense kwa magamba mana hawajitambui kabisa, kiongozi mkubwa yule jamaa hata historia ya nchi haijui itakuweje watoto wetu wapate elimu stahili kama mpitia midahalo ya elimu ni yeye boga wetu!
 
SMU; Bila shaka alikuchukiza sana Mhe.Rais Kikwete kwa kushindwa kutamka "Uhuru wa Tanganyika" bila kigugumizi. By the way, kusema Tanzania bara ina maana visiwa kama Nansio,Ukerewe,Makobe n.k ni provinces za Zanzibar?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: SMU
SMU; Bila shaka alikuchukiza sana Mhe.Rais Kikwete kwa kushindwa kutamka "Uhuru wa Tanganyika" bila kigugumizi. By the way, kusema Tanzania bara ina maana visiwa kama Nansio,Ukerewe,Makobe n.k ni provinces za Zanzibar?
Mkuu, kwa kweli wanakera. Yaani unaweza kufikiri kutamka neno "Tanganyika" mbele za watu ni kukosa maadili (ni matusi)!
 
Nilimsikia katika hutoba JK anavyobabaika!...Uhuru wa Tanzania, Uhuru wa Tanzania Bara, Uhuru wa Tanganyika?

huyu JK majanga matupu .sijui hata tulitoka naye wapi ...aghhhh
 
Baba Gaude; Si kwamba anasimamia sera za chama chake japokuwa alikiuka pale aliporuhusu mjadala wa katiba mpya jambo ambalo halikuwahi kuwa sera ya CCM!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom