Ndekirhepva
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 371
- 44
Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa CHADEMA wameandaa vijana mia mbili, ambao wametafutiwa fulana za CCM wazivae kesho katika mkutano wao jangwani lakini pia wamewafanyia semina vijana hao ili waseme kuwa ni wana-CCM ambao wataikana CCM hapo kesho katika viwanja vya jangwani.
Ni mkakati wa kilaghai kwa wananchi wa kujionesha kuwa wanakubalika kwa kuwarubuni baadhi ya watu ambao ni watu wao na kuwatumia kama wanaCCM wanaoikana CCM. Ili kuitangaza kauli mbiu yao ya vua gamba vaa gwandwa
Sehemu waliyofanyia semina hiyo imejulikana ni sinza, na mtu aliyewapatia jezi hizo pia amejulikana na hivi sasa yupo jengo la umoja wa vijana akihojiwa na kupewa stahiki nyinginezo. Wameumbuka...!
mbona huja mshtua mjomba wako mukama akawaumbue na hizo dekio zenu za kijni na njano??????
sanasana mnaivunjia heshima rangi ya kijani kwa vile sasa hivi imekua ya kuzaraulika tu ilihali inawakilisha kitu fulani katika bendera ya taifa letu hili lililojaa vibaka wa posta hadi wa magogoni...shame on you