KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 537
katika hali inayoonyesha kuwa kuingia kwa Dr. Slaa katika uchaguzi wa mwaka huu ni pigo kubwa kwa CCM na Kikwete, CCM wanahaha kutafuta ushindi ambao wanadhani unaweza kuwaponyoka wakati wowote. Hali hiyo imedhihirishwa na matumizi ya mabilioni ya fedha kwa ajili ya kampeni. Hivi sasa CCM wanabandika mabango ya mgombea wao kila baada ya mita mia moja nchi nzima kuhakikisha kuwa mgombea wao anatambulishwa kwa watanzania pamoja na kuwa watanzania wanamfahamu fika kwa muda wa miaka mitano aliowatumbukiza kwenye hali ngumu ya maisha. Jana nimewakuta mafundi wakiangaika wakiendelea kusimika bill boards na kubandika picha za mgombea wa CCM kwenye barabara ya sam Nujoma. Barabara imechafuka picha za Kikwete na CCM yake.
DR. Slaa kaza buti CCM wageuke wapinzani kuanzia November
DR. Slaa kaza buti CCM wageuke wapinzani kuanzia November