KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 537
Kampeni chafu imeanzishwa na chama cha mafisadi kuhakikisha kuwa Chadema na wagombea wake hawashidi katika uchaguzi wa mwaka huu. Kampeni hii imeanza baada ya kuona kuwa upepo unawaendea vibaya CCM na wagombea wake katika majimbo mbalimbali ha[pa nchini. Kampeni chafu inayofanywa na CCM ni ya kubandika mapicha ya wagombea wao juu ya wagombea wa Chadema. Hili linafanyika kuhakikisha kuwa wananchi wananyimwa haki ya kuwafahamu vilivyo wagembea makini wa chama cha chadema ili wa CCM ndo wajulikane. Ushahidi wa jambo hili utaupata eneo la stendi ya utawala chuo kikuu cha Dar es salaam ambako CCM wamedandika picha ya kikwete na Ng'umbi ya ya picha za Dr. Slaa na Mnyika. CCM wanataka kuhakikisha wanaibomolea mbali ngome ya chadema baada ya hatua ya awali ya kuhakikisha idadi kubwa ya wanafunzi wa UDSM hawapigi kula katika vituo vyao kwa kuwa watakuwa likizo wakati wa uchaguzi.
Imeandaliwa na Kidundulima
Imeandaliwa na Kidundulima