kaking81
New Member
- Feb 12, 2019
- 2
- 7
WANARUDISHA BUNGE LIVE KWA MBINDE
CHAMA cha Mapinduzi na Serikali yao hivi sasa wako kwenye Mvutano mkali kwa kipindi cha Wiki nzima na zaidi, kuhusiana na uamuzi wa kurejesha "Bunge Live" kwa Wananchi.
Viongozi wa CCM wanatoa hoja Vikaoni kwamba; Wabunge wake hawaonekani kwa Wananchi na wanaenda mbali zaidi wanaitetea hoja yao wakisema, Mitaani hakukaliki kutokana na hasira walizonazo Wananchi maana huko Mitaani Wananchi wanaamini kuwa, Serikali ya CCM ndio imewanyima haki hiyo na sasa hivi Nchi nzima Wananchi wanaijadili vibaya sana CCM kuhusiana na suala hili la Bunge kutokuwa Mubashara.
Hao Viongozi wa CCM wanaohudhuria Vikao hivi vizito vinavyofanyikia kwenye lile Jengo lenu wanazitetea hoja hizi kwa kueleza wazi kuwa, hoja ya gharama za uendeshaji" wa Bunge Live kuwa kubwa kama ilivyotolewa wakati wa kufuta utaratibu huo, imewaelemea katika kuitolea ufafanuzi mbele za Wananchi na wanaisihi Serikali iurejeshe ule utaratibu wa mwanzo kwa kile wanachosema kuwa, itakuwa ni ahueni nyingine kwa CCM kuelekea Chaguzi zijazo.
Kwa sasa, hoja ya Bunge Live ni miongoni mwa hoja nzito zinazowasumbua sana CCM na Serikali yao juu ya namna gani wataweza kujinasua, ukiliachilia mbali suala la Tundu Lissu aliyeumizwa vibaya na ameamua kuieleza Dunia 'jinsi' alivyokosa Ushirikiano wa Serikali ya Chama hicho pamoja na kwamba ni Mbunge mwenye Stahiki za Kibunge na alikuwa Rais wa Chama cha Mawakili TLS.
Kuhusiana na hoja hii ya Bunge Live, Serikali kwa upande wao, wanapata kigugumizi sana kuwa wazi juu ya nini wafanye kutokana na kwamba, "Mkuu" wenu bado haridhiki maana shida yake kubwa, hataki Wabunge wa Upinzani waonekane kwa Wananchi, anahisi Wananchi wakiona hoja zao (akina Lema, Bulaya, Heche, Msigwa, Zitto, Mdee, Mnyika na wengine) zitakuwa sumu ya kumharibia Kura za 2020 maana akili yake yote ni jinsi gani ataweza kurudi tena humo Magogoni 2020.
Baadhi ya Watu wa Serikali wanaohudhuria Vikao hivyo wanasema, baadhi ya Wabunge wa Chama chao wanahoji vitu vya ajabu wakiwa Bungeni, hivyo inaweza kuendelea kuwa fedheha kwa Chama hicho kama Wananchi wakiwatazama Mubashara. Mmoja wa Maofisa wa Serikali alitolea Mfano wa Mbunge mmoja Mwanamke kupitia CCM aliyehoji kwa nini Wanaume wasianze kukaguliwa getini kama wametaahiriwa kabla hawajaingia ndani ya Bunge.
Kinachopangwa sasa kuhusiana na suala hili la Bunge Live, ni kuanza kuratibu Propaganda ya kuonyesha kwamba, kuna Watu wanamuomba Rais aingilie kati suala hilo (subirini muone kama hawataahirisha) kisha utaitishwa Mkutano wa wadau wa habari pamoja na Wananchi kama ilivyofanyika kwenye suala la Kikokotoo cha 25% ili Rais akatoe kauli ya kuliomba Bunge kurejesha Bunge Live kwa niaba ya Wananchi.
Baada ya hapo; wadau wote pamoja na Wananchi, imepangwa kuwa; yafanyike Maandamano kila kona ya Nchi kwa ajili ya kumpongeza "Rais" kwa kuliomba Bunge kurejesha Bunge Live la Wananchi na Movie iishie hapo, tusubiri nyingine.
Hizi ndizo Siasa za Matukio. Yaani ni zile Siasa za kutengeneza tatizo mbele za Watu unaowaongoza kisha unarudi tena wewe huyo huyo kulitatua kwa mbinu zile zile ulizopita wakati wa kulianzisha na hao Watu wapige Makofi na kukushangilia tena huku wakikuita Shujaa, Jembe, Mpiganaji ama hata Mtetezi wa Wanyonge.
Kwa mujibu wa taarifa za Vikao hivyo, mambo mengine yanayowasumbulia CCM na Serikali yao akili kuelekea Chaguzi zinazofuata ni pamoja na haya; Mauaji ya Raia wasio na hatia kila wakati na kusiwepo na upelelezi wa kueleweka, kupotea ama kupotezwa kwa Raia, Wanaharakati, Wanahabari, Wanasiasa, Wafanyabiashara n.k. Uchumi wa Nchi kuendelea kudorora Siku hadi Siku.
Suala la Korosho za Watu wa kusini, Kunyimwa Misaada na Mataifa makubwa ya Dunia. Deni la Taifa kuongezeka kwa Kasi ya ajabu kutoka Trillioni 30 hadi Trillioni 60 na zaidi zinazodaiwa sasa.
Mambo mengine ambayo ni tatizo la sasa kwa CCM ni haya; Huduma hovyo ya Maji Vijijini na Mijini, Ahadi ya Millioni 50 kila Kijiji na Kukosekana kwa Ajira.
Francis M. Garatwa,
Diwani na Mwenyekiti wa Chadema Serengeti.
CHAMA cha Mapinduzi na Serikali yao hivi sasa wako kwenye Mvutano mkali kwa kipindi cha Wiki nzima na zaidi, kuhusiana na uamuzi wa kurejesha "Bunge Live" kwa Wananchi.
Viongozi wa CCM wanatoa hoja Vikaoni kwamba; Wabunge wake hawaonekani kwa Wananchi na wanaenda mbali zaidi wanaitetea hoja yao wakisema, Mitaani hakukaliki kutokana na hasira walizonazo Wananchi maana huko Mitaani Wananchi wanaamini kuwa, Serikali ya CCM ndio imewanyima haki hiyo na sasa hivi Nchi nzima Wananchi wanaijadili vibaya sana CCM kuhusiana na suala hili la Bunge kutokuwa Mubashara.
Hao Viongozi wa CCM wanaohudhuria Vikao hivi vizito vinavyofanyikia kwenye lile Jengo lenu wanazitetea hoja hizi kwa kueleza wazi kuwa, hoja ya gharama za uendeshaji" wa Bunge Live kuwa kubwa kama ilivyotolewa wakati wa kufuta utaratibu huo, imewaelemea katika kuitolea ufafanuzi mbele za Wananchi na wanaisihi Serikali iurejeshe ule utaratibu wa mwanzo kwa kile wanachosema kuwa, itakuwa ni ahueni nyingine kwa CCM kuelekea Chaguzi zijazo.
Kwa sasa, hoja ya Bunge Live ni miongoni mwa hoja nzito zinazowasumbua sana CCM na Serikali yao juu ya namna gani wataweza kujinasua, ukiliachilia mbali suala la Tundu Lissu aliyeumizwa vibaya na ameamua kuieleza Dunia 'jinsi' alivyokosa Ushirikiano wa Serikali ya Chama hicho pamoja na kwamba ni Mbunge mwenye Stahiki za Kibunge na alikuwa Rais wa Chama cha Mawakili TLS.
Kuhusiana na hoja hii ya Bunge Live, Serikali kwa upande wao, wanapata kigugumizi sana kuwa wazi juu ya nini wafanye kutokana na kwamba, "Mkuu" wenu bado haridhiki maana shida yake kubwa, hataki Wabunge wa Upinzani waonekane kwa Wananchi, anahisi Wananchi wakiona hoja zao (akina Lema, Bulaya, Heche, Msigwa, Zitto, Mdee, Mnyika na wengine) zitakuwa sumu ya kumharibia Kura za 2020 maana akili yake yote ni jinsi gani ataweza kurudi tena humo Magogoni 2020.
Baadhi ya Watu wa Serikali wanaohudhuria Vikao hivyo wanasema, baadhi ya Wabunge wa Chama chao wanahoji vitu vya ajabu wakiwa Bungeni, hivyo inaweza kuendelea kuwa fedheha kwa Chama hicho kama Wananchi wakiwatazama Mubashara. Mmoja wa Maofisa wa Serikali alitolea Mfano wa Mbunge mmoja Mwanamke kupitia CCM aliyehoji kwa nini Wanaume wasianze kukaguliwa getini kama wametaahiriwa kabla hawajaingia ndani ya Bunge.
Kinachopangwa sasa kuhusiana na suala hili la Bunge Live, ni kuanza kuratibu Propaganda ya kuonyesha kwamba, kuna Watu wanamuomba Rais aingilie kati suala hilo (subirini muone kama hawataahirisha) kisha utaitishwa Mkutano wa wadau wa habari pamoja na Wananchi kama ilivyofanyika kwenye suala la Kikokotoo cha 25% ili Rais akatoe kauli ya kuliomba Bunge kurejesha Bunge Live kwa niaba ya Wananchi.
Baada ya hapo; wadau wote pamoja na Wananchi, imepangwa kuwa; yafanyike Maandamano kila kona ya Nchi kwa ajili ya kumpongeza "Rais" kwa kuliomba Bunge kurejesha Bunge Live la Wananchi na Movie iishie hapo, tusubiri nyingine.
Hizi ndizo Siasa za Matukio. Yaani ni zile Siasa za kutengeneza tatizo mbele za Watu unaowaongoza kisha unarudi tena wewe huyo huyo kulitatua kwa mbinu zile zile ulizopita wakati wa kulianzisha na hao Watu wapige Makofi na kukushangilia tena huku wakikuita Shujaa, Jembe, Mpiganaji ama hata Mtetezi wa Wanyonge.
Kwa mujibu wa taarifa za Vikao hivyo, mambo mengine yanayowasumbulia CCM na Serikali yao akili kuelekea Chaguzi zinazofuata ni pamoja na haya; Mauaji ya Raia wasio na hatia kila wakati na kusiwepo na upelelezi wa kueleweka, kupotea ama kupotezwa kwa Raia, Wanaharakati, Wanahabari, Wanasiasa, Wafanyabiashara n.k. Uchumi wa Nchi kuendelea kudorora Siku hadi Siku.
Suala la Korosho za Watu wa kusini, Kunyimwa Misaada na Mataifa makubwa ya Dunia. Deni la Taifa kuongezeka kwa Kasi ya ajabu kutoka Trillioni 30 hadi Trillioni 60 na zaidi zinazodaiwa sasa.
Mambo mengine ambayo ni tatizo la sasa kwa CCM ni haya; Huduma hovyo ya Maji Vijijini na Mijini, Ahadi ya Millioni 50 kila Kijiji na Kukosekana kwa Ajira.
Francis M. Garatwa,
Diwani na Mwenyekiti wa Chadema Serengeti.