Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Kundya ataka Nape,wenzake wapigwe 'stop'
KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza,Rajabu Kundya, amesema ziara zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Nape Nnauye na wenzake katika mikoa mbalimbali nchini, zinapingana na taratibu za CCM.
Kundya pia amesema kitendo cha viongozi hao kuwataja majina baadhi ya wanachama wanaotuhumiwa kwa mambo mbalimbali kinaleta mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hicho kinachotawala.
Katika zira hizo mikoani, Nape amekuwa akifuatana na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na wengine kadhaa.Akizungumza katika mahojiano maalum jana katibu huyo wa CCM wa Mkoa wa Mwanza, alisema ingawa ziara kama hizo zingeweza kusaidia kuimarisha chama, lakini kutaja majina ya watu na kuwashutumu si sehemu ya kuimarisha chama bali kukibomoa.
"Kama kuna mtu ambaye wanadhani ana tatizo kubwa ndani ya chama, utaratibu upo na wala si busara kumtaja katika mikutano ya hadhara, hili ni la kulisemea ndani ya vikao," alisema Kundya.Alisema taratibu za kusema zipo na zinatoa nafasi kwa mwananchama yeyote kuzungumza na hata kuwasema wenzake kupitia njia za vika ndani ya chama.
Mtendaji huyo alisema kinachokifanywa na Nape na wenzake hasa kuwasema hadharani viongozi wanaotakiwa kujivua magamba, ni kukiuka taratibu. Alisema hata hiyo jambo hilo analiacha mikononi mwa chama, ili kiangalie namna ya kuwazuia viongozi hao ili wasiendelee kuvunja taratibu.
Kwa kauli hiyo katibu huyo atakuwa anaungana na wenyeviti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja na Mkoa wa Dar es salaam John Guninita waliojitokeza kuwakosoa makada hao wa CCM.
Mwananchi
KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza,Rajabu Kundya, amesema ziara zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Nape Nnauye na wenzake katika mikoa mbalimbali nchini, zinapingana na taratibu za CCM.
Kundya pia amesema kitendo cha viongozi hao kuwataja majina baadhi ya wanachama wanaotuhumiwa kwa mambo mbalimbali kinaleta mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hicho kinachotawala.
Katika zira hizo mikoani, Nape amekuwa akifuatana na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Lazaro Nyalandu, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na wengine kadhaa.Akizungumza katika mahojiano maalum jana katibu huyo wa CCM wa Mkoa wa Mwanza, alisema ingawa ziara kama hizo zingeweza kusaidia kuimarisha chama, lakini kutaja majina ya watu na kuwashutumu si sehemu ya kuimarisha chama bali kukibomoa.
"Kama kuna mtu ambaye wanadhani ana tatizo kubwa ndani ya chama, utaratibu upo na wala si busara kumtaja katika mikutano ya hadhara, hili ni la kulisemea ndani ya vikao," alisema Kundya.Alisema taratibu za kusema zipo na zinatoa nafasi kwa mwananchama yeyote kuzungumza na hata kuwasema wenzake kupitia njia za vika ndani ya chama.
Mtendaji huyo alisema kinachokifanywa na Nape na wenzake hasa kuwasema hadharani viongozi wanaotakiwa kujivua magamba, ni kukiuka taratibu. Alisema hata hiyo jambo hilo analiacha mikononi mwa chama, ili kiangalie namna ya kuwazuia viongozi hao ili wasiendelee kuvunja taratibu.
Kwa kauli hiyo katibu huyo atakuwa anaungana na wenyeviti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja na Mkoa wa Dar es salaam John Guninita waliojitokeza kuwakosoa makada hao wa CCM.
Mwananchi