OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,943
- 428
Mchakato wa kuwapata mameya,manaibu mameya na wenyeviti wa Halmashauri nchini kupitia CCM ,Unaendelea kukipasua chama hicho baada ya diwani mwingine wa chama hicho kujiuzulu wadhifa huo
Aliyejiuzulu jana ni diwani wa kata ya nyamtinga ,Okea Ogigo ,wilaya ya Rorya Mkoani Mara akiungana na wengine wawili waliojiuzulu juzi ,Ongujo Wakibara wa kata ya Mkoma ,na Lukio Ambogo wa kata ya Nyaongo
Pamoja na madiwani hao,wanaopinga uamuzi ya kuenguliwa kwa baadhi ya majina kuwania uenyekiti wa halmashauri uliofanywa na fisadi Yusuph Makamba na Pius Msekwa dhidi ya msimamo wa wilaya ,pia yumo mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Rorya ,Leonard Yoda
Akizungumza na wananchi wa kata ya Mkoma Shirati Yoda alisema kuwa haoni sababu ya kuendelea kukiongoza chama wakati maamuzi ya vikao havizingatiwi na uongozi wa juu wa chama ,Mwenyekiti huyo anayeachia ngazi ,Yoda alisema kuwa uongozi wa mkoa na kamati ya siasa chini ya uenyekiti wa makongoro nyerere na katibu wake Ndekubali Ndengaso,walipitisha majina mawili Lukio Ambogo na Okea Ogigo ambao hawakuwa na Makundi na hawakuwa na kashfa ya Rushwa kipindi cha Uchaguzi Mkuu 2010
Katibu wa kata ya Mkoma Juma Ombata naye Ametangaza Kujiuzulu
Aliyejiuzulu jana ni diwani wa kata ya nyamtinga ,Okea Ogigo ,wilaya ya Rorya Mkoani Mara akiungana na wengine wawili waliojiuzulu juzi ,Ongujo Wakibara wa kata ya Mkoma ,na Lukio Ambogo wa kata ya Nyaongo
Pamoja na madiwani hao,wanaopinga uamuzi ya kuenguliwa kwa baadhi ya majina kuwania uenyekiti wa halmashauri uliofanywa na fisadi Yusuph Makamba na Pius Msekwa dhidi ya msimamo wa wilaya ,pia yumo mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Rorya ,Leonard Yoda
Akizungumza na wananchi wa kata ya Mkoma Shirati Yoda alisema kuwa haoni sababu ya kuendelea kukiongoza chama wakati maamuzi ya vikao havizingatiwi na uongozi wa juu wa chama ,Mwenyekiti huyo anayeachia ngazi ,Yoda alisema kuwa uongozi wa mkoa na kamati ya siasa chini ya uenyekiti wa makongoro nyerere na katibu wake Ndekubali Ndengaso,walipitisha majina mawili Lukio Ambogo na Okea Ogigo ambao hawakuwa na Makundi na hawakuwa na kashfa ya Rushwa kipindi cha Uchaguzi Mkuu 2010
Katibu wa kata ya Mkoma Juma Ombata naye Ametangaza Kujiuzulu