Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,175
- 25,446
Nawaandikia viongozi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Nawaandikia kuwaambia kuwa siku si nyingi tutawapuuza kwa kila mnalolisema au kulitenda. Hii tabia ya kukaa na mafisadi na majizi kwenye chama chenu hadi wahame au waachane na siasa ndiyo muwanyooshee vidole na kuwasema si sawa.
Uzuri wenu CCM ndiyo mnaounda Serikali. Mna kila uwezo, kama kuna nia pia, ya kuwachunguza, kuwabaini na kuwashughulikia mafisadi na majizi yote yaliyopo kwenye chama chenu. Kwakuwa mmekuwa madarakani tangu kuanzishwa kwenu mwaka 1977, hamuwezi kusema kuna mahali kuna majizi mengi kuliko nyinyi kwakuwa mko wengi.
Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wenu wa Taifa wa CCM aliingia madarakani, pamoja na sera nyinginezo, na sera ya kupambana na kuyashughulikia mafisadi na majizi yote ya hapa Tanzania. Sera yake hiyo, ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa Mahakama ya Mafisadi, iliwavutia watanzania waliokuwa wamechoshwa na ufisadi na kumchagua Magufuli kwa wingi wao.
CCM mnapaswa kumsaidia Rais Magufuli kwa matendo katika vita dhidi ya mafisadi na majizi ya mali za umma. Msaidieni Rais kuwabaini, kuwachunguza na kuwashughulikia mafisadi wote waliopo CCM hivi sasa ili kama usafi uanzie ndani ya CCM. Kungoja hadi mwanasiasa ahame CCM na nyinyi kuanza kumsema kuwa ni fisadi na mwizi ni utapeli wa hali ya juu.
CCM, kuweni serious na mambo yenu. Kuaminika kwenu kunategemea na mnayoyasimamia na kuyafanya sasa. Pia, mnapaswa kujibu kichama mapigo yote ya wanaohama bila ya kuwategemea wasomi makada na watawala kuwajibu wanaoibua maswala ya kichama zaidi. Nasema tena, mafisadi na majizi yote yaliyopo CCM yashughulikiwe sasa. Au mseme wazi sasa kuwa ndani ya CCM hakuna mafisadi au majizi.
Msipowashughulikia sasa mafisadi na majizi hadi msubiri wahame au wajiuzulu, tutawapuuza na kuwaona matapeli, walaghai na watu wa propaganda. Muda wa kuwashughulikia mafisadi na majizi ndani na nje ya CCM ni sasa katika kuunga mkono sera ya Rais wetu na mwenyekiti wenu Dr. John Pombe Magufuli.
Uzuri wenu CCM ndiyo mnaounda Serikali. Mna kila uwezo, kama kuna nia pia, ya kuwachunguza, kuwabaini na kuwashughulikia mafisadi na majizi yote yaliyopo kwenye chama chenu. Kwakuwa mmekuwa madarakani tangu kuanzishwa kwenu mwaka 1977, hamuwezi kusema kuna mahali kuna majizi mengi kuliko nyinyi kwakuwa mko wengi.
Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wenu wa Taifa wa CCM aliingia madarakani, pamoja na sera nyinginezo, na sera ya kupambana na kuyashughulikia mafisadi na majizi yote ya hapa Tanzania. Sera yake hiyo, ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa Mahakama ya Mafisadi, iliwavutia watanzania waliokuwa wamechoshwa na ufisadi na kumchagua Magufuli kwa wingi wao.
CCM mnapaswa kumsaidia Rais Magufuli kwa matendo katika vita dhidi ya mafisadi na majizi ya mali za umma. Msaidieni Rais kuwabaini, kuwachunguza na kuwashughulikia mafisadi wote waliopo CCM hivi sasa ili kama usafi uanzie ndani ya CCM. Kungoja hadi mwanasiasa ahame CCM na nyinyi kuanza kumsema kuwa ni fisadi na mwizi ni utapeli wa hali ya juu.
CCM, kuweni serious na mambo yenu. Kuaminika kwenu kunategemea na mnayoyasimamia na kuyafanya sasa. Pia, mnapaswa kujibu kichama mapigo yote ya wanaohama bila ya kuwategemea wasomi makada na watawala kuwajibu wanaoibua maswala ya kichama zaidi. Nasema tena, mafisadi na majizi yote yaliyopo CCM yashughulikiwe sasa. Au mseme wazi sasa kuwa ndani ya CCM hakuna mafisadi au majizi.
Msipowashughulikia sasa mafisadi na majizi hadi msubiri wahame au wajiuzulu, tutawapuuza na kuwaona matapeli, walaghai na watu wa propaganda. Muda wa kuwashughulikia mafisadi na majizi ndani na nje ya CCM ni sasa katika kuunga mkono sera ya Rais wetu na mwenyekiti wenu Dr. John Pombe Magufuli.