CCM tusijisahau na kujisahaulisha kuhusu Ilani yetu na ahadi tulizozitoa kwa wapigakura mwaka 2015. Muda unataradadi!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Najua kuwa kwasasa wanaCCM wenzangu wengi wanaamini kuwa katika mazingira ya kisiasa ya sasa CCM haipitiki kiuchaguzi. Makada wenzangu wengi wanaamini kuwa hakuna chama chochote cha upinzani au mpinzani binafsi atakayeweza kuishinda CCM kwenye uchaguzi mdogo au hata mkuu wa mwaka 2020. Tunaamini kuwa CCM iko sahihi kwa kila jambo na ushindi ni lazima.

Kwangu mimi kama kada kindakindaki na mwanasiasa mkongwe chamani na nchini, siamini hivyo. Siamini kuwa mwaka 2020 lazima CCM ishinde. Kama kada niliyepikwa chamani tangu miaka ya themanini, naamini kuwa siasa ni kama upepo na uelekeo wake. Siasa hubadilika bila kutoa tahadhari. Namini kuwa mwaka 2020 ni mbali sana katika mabadiliko ya upepo wa kisiasa lakini ni karibu sana katika kujiandaa kujibu hoja.

Hapa kati kunaweza hata kukatokea chama kipya cha kisiasa. Tena kwa kumegeka hata kwa CCM yetu. Hapa kati, panaweza kujitokeza sera au muuzasera mahiri kuliko mshairi na kuwafunika wote waliotangulia. Hapa kati, panaweza kuibuka kashfa au chuki kwa walio na uhakika wa kuchaguliwa na hatimaye kukataliwa kwelikweli. Hapa kati, panaweza kutokea 'wasaidizi wa ushindi' wa CCM wakabadilika. Wakawa wavivu na wenye wivu.

Kinga pekee kisiasa, ili kuwa na uhakika wa kushinda tena, ni kutekeleza Ilani na ahdi za wagombea wetu wa mwaka 2015. Tutakachopaswa kuonesha mwaka 2020 ni utekelezaji wa Ilani na ahadi zetu kwa wananchi. Si vinginevyo. Wananchi wanatupima CCM kwa Ilani yetu ile ya mwaka 2015 kabla ya kutuamini tena kwa Ilani ya mwaka 2020. Watataka kuyaona mazuri yetu kupitia utekelezaji wa Ilani yetu. Utekelezaji wa Ilani na hadi ni kila kitu.

Kutegemea Tume ya Uchaguzi, Polisi na mfumo kuturejesha madarakani kumepitwa na wakati. Kila kada, katika nafasi yake na mahali alipo, asimamie utekelezaji wa Ilani na hadi zetu za 2015. Kuamini kuwa wapinzani wameishiwa nguvu ni kujihatarisha sana kisiasa. Ni kujiweka rehani. Ni kujipalia makaa ya moto. CCM haina haja ya kutegemea Tume kushinda. Haina haja kutegemea Polisi kushinda. Haina haja ya kutegemea mfumo kushinda. Inapaswa kujiandaa kama chama. Muda unayoyoma.

Ukonga na Monduli 'tutashinda' lakini chamoto tutakiona!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Umewaasa makada wenzio wa chama kongwe na chovu vema kabisa. Tatizo Ni kwamba wameshazoea mbeleko ya NEC na polisi na wasipoachiwa kujitegemea mapema, 2020 itabidi waendelee kuitegemea mbeleko. Kama watakuelewa basi kuanzia kwenye chaguzi ndogo zijazo polisi wafanye kazi yao kwa weledi na vivyo hivyo NEC; vinginevyo CCM ya kubebwa tu hadi 2020 na kuendelea!
 
Mzee Tupatupa, sikujua kama kuna mtu mwenye asiye mnafiki kama ww bado yumo ccm. Mengi uliyoandika ni kweli kabisa. Ila kuna maeneo machache huelewi, au umedanganya, nayo ni haya hapa:

1). Ilani haiwezi kuwasaidia chochote. Umma ushachoka sana na hicho chama, na ndo maana maeneo mengi ya nchi hawawezi kushinda kwa uchaguzi huru.
2). Viongozi wa juu wa hicho chama (hata wastaafu wao) wana madhambi mengi mno, so hawawezi kuruhusu utawala mwingine.. Ndo maana hata kule znz walimtumia jecha "kurekebisha" mambo.
3). ...duh, ngoja kwnz niweke akiba ya maneno
 
CCM haiwezi shinda Monduli wala Ukonga
Itapokonya kwa kutumia NEC ya Ikulu
NEC inayopewa maelezo na CCM
 
Najua kuwa kwasasa wanaCCM wenzangu wengi wanaamini kuwa katika mazingira ya kisiasa ya sasa CCM haipitiki kiuchaguzi. Makada wenzangu wengi wanaamini kuwa hakuna chama chochote cha upinzani au mpinzani binafsi atakayeweza kuishinda CCM kwenye uchaguzi mdogo au hata mkuu wa mwaka 2020. Tunaamini kuwa CCM iko sahihi kwa kila jambo na ushindi ni lazima.

Kwangu mimi kama kada kindakindaki na mwanasiasa mkongwe chamani na nchini, siamini hivyo. Siamini kuwa mwaka 2020 lazima CCM ishinde. Kama kada niliyepikwa chamani tangu miaka ya themanini, naamini kuwa siasa ni kama upepo na uelekeo wake. Siasa hubadilika bila kutoa tahadhari. Namini kuwa mwaka 2020 ni mbali sana katika mabadiliko ya upepo wa kisiasa lakini ni karibu sana katika kujiandaa kujibu hoja.

Hapa kati kunaweza hata kukatokea chama kipya cha kisiasa. Tena kwa kumegeka hata kwa CCM yetu. Hapa kati, panaweza kujitokeza sera au muuzasera mahiri kuliko mshairi na kuwafunika wote waliotangulia. Hapa kati, panaweza kuibuka kashfa au chuki kwa walio na uhakika wa kuchaguliwa na hatimaye kukataliwa kwelikweli. Hapa kati, panaweza kutokea 'wasaidizi wa ushindi' wa CCM wakabadilika. Wakawa wavivu na wenye wivu.

Kinga pekee kisiasa, ili kuwa na uhakika wa kushinda tena, ni kutekeleza Ilani na ahdi za wagombea wetu wa mwaka 2015. Tutakachopaswa kuonesha mwaka 2020 ni utekelezaji wa Ilani na ahadi zetu kwa wananchi. Si vinginevyo. Wananchi wanatupima CCM kwa Ilani yetu ile ya mwaka 2015 kabla ya kutuamini tena kwa Ilani ya mwaka 2020. Watataka kuyaona mazuri yetu kupitia utekelezaji wa Ilani yetu. Utekelezaji wa Ilani na hadi ni kila kitu.

Kutegemea Tume ya Uchaguzi, Polisi na mfumo kuturejesha madarakani kumepitwa na wakati. Kila kada, katika nafasi yake na mahali alipo, asimamie utekelezaji wa Ilani na hadi zetu za 2015. Kuamini kuwa wapinzani wameishiwa nguvu ni kujihatarisha sana kisiasa. Ni kujiweka rehani. Ni kujipalia makaa ya moto. CCM haina haja ya kutegemea Tume kushinda. Haina haja kutegemea Polisi kushinda. Haina haja ya kutegemea mfumo kushinda. Inapaswa kujiandaa kama chama. Muda unayoyoma.

Ukonga na Monduli 'tutashinda' lakini chamoto tutakiona!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Tatizo walio wengi wanasahau hayo kwa kujipima kwa ushindi wa baadhi ta kata
 
Tshirts, kanga, fulana, jezi za mpira, kuwaalika wasanii waje kutumbuiza kwenye maeneo yetu, vitamaliza tatizo. Usihofu kada.

Na hata kura zisipotosha, zitatosheshwa.
 
Million 50 kila kijiji zitatolewa ama hazitolewi?? Kwani walipo ahidi hawakujua kuwa wanatakiwa pia kusimamia ujenzi wa shule, zahanati, barabara nk? Ahadi ni deni na dawa ya deni ni kulipa kinyume na hapo ni ulaghai, uwongo, utapeli na maneno mengine yanayofanana na hayo!
 
Si mtatumia Geshi ndio maana hamna wasiwasi? Polish si wapo kuhakikisha kura zinatosha kama mlivyofanya kwenye chaguzi za marudio. mf. Buyungu?
 
Hata mimi ningekuwa chama tawala nisingekubali kuachia madaraka wakati jeshi,bunge, ikulu,tume ya uchaguzi viko chini yangu
 
Back
Top Bottom