CCM tusibeze uchaguzi mkuu wa 2020

mkafrend

JF-Expert Member
May 12, 2014
3,047
1,503
Wanaccm wenzangu, salaam!
Naomba nianze kwa kuwakumbusha kwamba ktk uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 chama cha CCM kilipata kura takribani 8 million huku CDM ikipata kura 6milioni.
Mabadiriko ya kura pamoja na kuwepo makundi ndani ya CCM lakini pia kwa CDM waliweza kuliteka kundi lika la vijana 18+.

Sasa uchaguzi ujao iwapo CCM hatutawekeza vizuri, basi mtaji wa CDM huenda ukawa ongezeko la vijana wenye sifa za kuchaguwa ambao kwa mwaka 2015 hawakuweza. Vijana hao ni:-
1. Waliokuwa na miaka 17 kwa 2015,
2. Waliokuwa na miaka 16 kwa 2015,
3. Waliokuwa na miaka 15 kwa 2015,
4. Waliokuwa na miaka 14 kwa 2015,
5. Waliokuwa na miaka 13 kwa 2015.

Jumla ya vijana hawa kwa idadi hadi Oktoba mwaka 2020 watakuwa 7,130,991. Hivyo, CCM tukiwaandaa kwa mfumo wa nyuma basi hata goli la mkono halitawezekana. Hii ni analysis tu - ikiwa mtu ana maoni basi ayawasilishe kwa njia ya kidiplomasia na yasiwe matusi.

MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU WABARIKI WANANCHI WOTE
MUNGU WABARIKI VIONGOZI WETU
 
Shida yako ni gani mkigoda nec homeport. Acha yule akitaka dau kuubwa
 
Shida yako ni gani mkigoda nec homeport. Acha yule akitaka dau kuubwa
Alipambana kule na chiza cjui akashindwa mara mbili kwenye kura za maoni nazan anajiandaa kuhama chama
 
Chama cha CCM wana mtaji mkubwa sana, mtaji wa Tume ya uchaguzi, hawahangaiki na vimtaji ulivyovisema hivyo.
 
Na hawa wote wanaandaliwa na walimu wa shule za kata ambao kwa sasa wanasumbuliwa hadi kudekishwa madarasa mbele ya wanafunzi wao
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom