Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Katika kipindi cha Miezi Miwili hapa tanzania Vyama vikubwa vya Siasa hapa Tanzania CHADEMA na CCM vimefanya harakati zenye lengo la kuwaambia wananchi ni kwa nini waungwe mkono wao na si mwingine.
Katika kufanya Hivyo CHADEMA ilifanya Maandamano ya Amani na kufanya Mikutano ya hadhara ikiwa na lengo la kuwaonesha wananchi ni kwa nini basi Chenyewe kinapswa kupewa Dola na si CCM. Kama lengo kuu la chama cha Upinzani kinachojitayarisha kuchukua Nchi, CHADEMA kimeendeleza harakati za kuwafanya Wananchi Waichukie CCM ambayo ndiyo inayounda Serikali iliyoko Madarakani. Kwa kweli CHADEMA kama chama cha Upinzani kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuleta Chuki ya Wananchi dhidi ya Serikali. Kwa hilo nawapongeza CHADEMA kama chama cha siasa, kwa sababu bila ya kuwafanya Wananchi waichukie Serikali iliyoko Madarakani huwezi Kuchukua Dola.
CCM katika kile kinachoonekana ni Kujaribu kupambana na Nguvu ya CHADEMA kilifanya kile walichokiita " Kujivua Gamba" na wamezunguka sehemu mbali mbali kuwaelezea Wananchi juu ya kile walichokiita "Dhana" ya kujivua Gamba. Tuliona kule Songea CCM walifanya Mkutano siku moja kabla ya CHADEMA hawajafanya wao ( Picha za Mikitano hiyo ya CCM zimekuwa ni Siri kubwa). Katika Mikutano hiyo CCM walitumia Mbinu zile zile zilizotumiwa na CHADEMA katika kujipatia Umaarufu miongoni mwa wananchi. Tuliona CCM wakimtuhumu Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Slaa kwa kile walichokiita " Siri' ya Mshahara wa dr. Slaa na Ufisadi wa Mbowe. Baada ya Mikutano hiyo ya Kuelezea "Dhana" ya kujivua Gamba nilitarajia yafuatayo na Tuhuma za Ufisadi dhidi ya Viongozi wa Ngazi za juu wa CHADEMA
1: Wananchi kumzomea Dr. Slaa kila apitapo
2: Wananchi Kumzomea Freeman Mbowe kwa Ufisadi wake
3: Wananchi kuyakataa Maandamao ya CHADEMA
Naomba niwaalike watetezi wa CCM na "Dhana" ya kujivua Gamba waje hapa jamvini na Kutupa Tathmini juu ya Mwitikio wa Wananchi juu ya "Kujivua Gamba". Watuwekee Picha za Mikutano waliyofanya CCM Songea, Singida na Kwingine
Katika kufanya Hivyo CHADEMA ilifanya Maandamano ya Amani na kufanya Mikutano ya hadhara ikiwa na lengo la kuwaonesha wananchi ni kwa nini basi Chenyewe kinapswa kupewa Dola na si CCM. Kama lengo kuu la chama cha Upinzani kinachojitayarisha kuchukua Nchi, CHADEMA kimeendeleza harakati za kuwafanya Wananchi Waichukie CCM ambayo ndiyo inayounda Serikali iliyoko Madarakani. Kwa kweli CHADEMA kama chama cha Upinzani kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuleta Chuki ya Wananchi dhidi ya Serikali. Kwa hilo nawapongeza CHADEMA kama chama cha siasa, kwa sababu bila ya kuwafanya Wananchi waichukie Serikali iliyoko Madarakani huwezi Kuchukua Dola.
CCM katika kile kinachoonekana ni Kujaribu kupambana na Nguvu ya CHADEMA kilifanya kile walichokiita " Kujivua Gamba" na wamezunguka sehemu mbali mbali kuwaelezea Wananchi juu ya kile walichokiita "Dhana" ya kujivua Gamba. Tuliona kule Songea CCM walifanya Mkutano siku moja kabla ya CHADEMA hawajafanya wao ( Picha za Mikitano hiyo ya CCM zimekuwa ni Siri kubwa). Katika Mikutano hiyo CCM walitumia Mbinu zile zile zilizotumiwa na CHADEMA katika kujipatia Umaarufu miongoni mwa wananchi. Tuliona CCM wakimtuhumu Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr. Slaa kwa kile walichokiita " Siri' ya Mshahara wa dr. Slaa na Ufisadi wa Mbowe. Baada ya Mikutano hiyo ya Kuelezea "Dhana" ya kujivua Gamba nilitarajia yafuatayo na Tuhuma za Ufisadi dhidi ya Viongozi wa Ngazi za juu wa CHADEMA
1: Wananchi kumzomea Dr. Slaa kila apitapo
2: Wananchi Kumzomea Freeman Mbowe kwa Ufisadi wake
3: Wananchi kuyakataa Maandamao ya CHADEMA
Naomba niwaalike watetezi wa CCM na "Dhana" ya kujivua Gamba waje hapa jamvini na Kutupa Tathmini juu ya Mwitikio wa Wananchi juu ya "Kujivua Gamba". Watuwekee Picha za Mikutano waliyofanya CCM Songea, Singida na Kwingine