Nimetumia muda mwingi kutafakari hali ya kisiasa inavyoenedea hapa nchini.
Napenda niweke wazi kabisa mimi ni mwana CCM na ni mwanachama hai maana hata kadi yangu imelipiwa ada hadi mwaka 2014. Katika hali ya kutafakari nimepata kuona kuwa sijambo la kuficha tena na katika hili CCM inaelewa wazi kuwa upepo wa kisiasa kwake hauendi vizuri na chama kinachoelekea kuchukua nafasi yake ni CHADEMA. Nitakuwa mnafiki sana iwapo nitashindwa kukiri ukweli huu kuwa hoja za kitaifa zinazotolewa na CHADEMA, hasa matatizo yanayoikabili nchi yakihusishwa na CCM ni ukweli mtupu.
CCM imeruhusu ufisadi kuwa utamadunu wake, watu wanakwapua raslimali za nchi huku umma wa watanzania ukiteseka katika hili CCM ielewe wazi kuwa watu hawako tayari kuona jambo hili linaendelea. Nimekuwa nikihudhuria vikao mbalimbali vya chama moja kati ya ajenda ambayo sasa inaelekea kuwa ya kudumu ni juu ya kwanini CCM imepoteza mvuto kwa watu.
Roho yangu huwa inaniuma maana swali hili majibu yake tunayo lakini tunajidai kupapaza kama vile hatuoni. Najua kuwa it is too late kwa CCM sasa hivi kujisafisha, la maana ni kuandaa exit plan chama kingine kitawale nchi kwa mfumo ulio wa kidemokrasia badala ya kuwa na kushikiana mitutu kwa ukaidi tu. Sasa hali mefukia katika climax, chama kimeanza kutumia vyombo vya dola ku-suprees demokrasia hadi kusababisha mauaji, hasa hili ndilo limekoleza chumvi kwa wanachi kuichukia CCM, hata mie nimesikia uchungu mwingi kiasi cha kuona kuwa nashiriki katika utendaji dhambi iwapo nitaendelea kuiunga Mkono CCM.
Eee, Mungu naomba unisamehe maana najiona msaliti wa umma kwa kendelea kuwa mwana CCM.
Najua wapo wanazi wasiopenda ukweli wanaweza kusema najifanya kuwa mwana-CCM wakati ni mwanachama wa chama kingine hasa CHADEMA inayotisha kwa jinsi inavyokubalika kama moto kwenye kichaka kikavu. Napenda niwahakikishie mie ni mwana-CCM wakati ukifika nitajitambulisha.
Wana JF hebu angalieni hili, daima ukiona timu inacheza defensive game ujue mambo yameiendea kombo, timu inayojiamini upeleka mashambulizi mbele huku ikijilinda isifungwe. Hii ndiyo hali iliyonayo CCM, kwa wakati huu haina hoja yoyote ya kupeleka maashambulizi mbele, bali imabaki kueleza oho! CHADMEA hao ni wapuuzi, hata wao wakipewa nchi watafanya hayo hayo, tusikubali kurubuniwa n.k Hoja za nguvu ziko wapi CCM? Sikubaliani na hali hii na wito kwa wana- CCM wenzangu, taabu na shida haziangalii unavaa rangi gani, dhiki na tabu zinatukumba wote hivyo kutokubali ukweli huo ni ujinga na uzandiki.
Hivi CCM, jiulize Mtoto wa Kikwete RZ1 kapata mtaji wapi wa kuweka vituo vya mafuta nchi nzima na malori lukuki?Lakini Jua watanzania wanaona! Najihisi uchungu sana hasa ninapoona wanachi vijijini wanashinda porini kwa kujificha ili wasitkamatwe kwa kutolipa michango ya ujenzi wa sekondari ya Kata, huku wapo watu wanao jichotea mabilioni ya Hela ambayo yangetosha kujenga vishule vyote vya Kata bila kudai senti kwa mwnanchi.
TUMECHOKA, TAFADHALI ENDELEZA MASHAMBULIZI MTUKOMBOE, HUKU MKIJIHADHALI MSIJE MKASAMBARATISHWA kwa mbinu za vyombo vya CCM.
Napenda niweke wazi kabisa mimi ni mwana CCM na ni mwanachama hai maana hata kadi yangu imelipiwa ada hadi mwaka 2014. Katika hali ya kutafakari nimepata kuona kuwa sijambo la kuficha tena na katika hili CCM inaelewa wazi kuwa upepo wa kisiasa kwake hauendi vizuri na chama kinachoelekea kuchukua nafasi yake ni CHADEMA. Nitakuwa mnafiki sana iwapo nitashindwa kukiri ukweli huu kuwa hoja za kitaifa zinazotolewa na CHADEMA, hasa matatizo yanayoikabili nchi yakihusishwa na CCM ni ukweli mtupu.
CCM imeruhusu ufisadi kuwa utamadunu wake, watu wanakwapua raslimali za nchi huku umma wa watanzania ukiteseka katika hili CCM ielewe wazi kuwa watu hawako tayari kuona jambo hili linaendelea. Nimekuwa nikihudhuria vikao mbalimbali vya chama moja kati ya ajenda ambayo sasa inaelekea kuwa ya kudumu ni juu ya kwanini CCM imepoteza mvuto kwa watu.
Roho yangu huwa inaniuma maana swali hili majibu yake tunayo lakini tunajidai kupapaza kama vile hatuoni. Najua kuwa it is too late kwa CCM sasa hivi kujisafisha, la maana ni kuandaa exit plan chama kingine kitawale nchi kwa mfumo ulio wa kidemokrasia badala ya kuwa na kushikiana mitutu kwa ukaidi tu. Sasa hali mefukia katika climax, chama kimeanza kutumia vyombo vya dola ku-suprees demokrasia hadi kusababisha mauaji, hasa hili ndilo limekoleza chumvi kwa wanachi kuichukia CCM, hata mie nimesikia uchungu mwingi kiasi cha kuona kuwa nashiriki katika utendaji dhambi iwapo nitaendelea kuiunga Mkono CCM.
Eee, Mungu naomba unisamehe maana najiona msaliti wa umma kwa kendelea kuwa mwana CCM.
Najua wapo wanazi wasiopenda ukweli wanaweza kusema najifanya kuwa mwana-CCM wakati ni mwanachama wa chama kingine hasa CHADEMA inayotisha kwa jinsi inavyokubalika kama moto kwenye kichaka kikavu. Napenda niwahakikishie mie ni mwana-CCM wakati ukifika nitajitambulisha.
Wana JF hebu angalieni hili, daima ukiona timu inacheza defensive game ujue mambo yameiendea kombo, timu inayojiamini upeleka mashambulizi mbele huku ikijilinda isifungwe. Hii ndiyo hali iliyonayo CCM, kwa wakati huu haina hoja yoyote ya kupeleka maashambulizi mbele, bali imabaki kueleza oho! CHADMEA hao ni wapuuzi, hata wao wakipewa nchi watafanya hayo hayo, tusikubali kurubuniwa n.k Hoja za nguvu ziko wapi CCM? Sikubaliani na hali hii na wito kwa wana- CCM wenzangu, taabu na shida haziangalii unavaa rangi gani, dhiki na tabu zinatukumba wote hivyo kutokubali ukweli huo ni ujinga na uzandiki.
Hivi CCM, jiulize Mtoto wa Kikwete RZ1 kapata mtaji wapi wa kuweka vituo vya mafuta nchi nzima na malori lukuki?Lakini Jua watanzania wanaona! Najihisi uchungu sana hasa ninapoona wanachi vijijini wanashinda porini kwa kujificha ili wasitkamatwe kwa kutolipa michango ya ujenzi wa sekondari ya Kata, huku wapo watu wanao jichotea mabilioni ya Hela ambayo yangetosha kujenga vishule vyote vya Kata bila kudai senti kwa mwnanchi.
TUMECHOKA, TAFADHALI ENDELEZA MASHAMBULIZI MTUKOMBOE, HUKU MKIJIHADHALI MSIJE MKASAMBARATISHWA kwa mbinu za vyombo vya CCM.