SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Chama Cha Mapinduzi kinafutilia kwa makini mienendo ya baadhi viongozi wake ambao wamekuwa wakipotosha Umma na kwenda kinyume na maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu na maadili ya Chama.
CCM inawakikishia wanachama na watanzania kuwa hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wote ambao wanatumia nafasi hiyo kusukuma ajenda zao binafsi, kwa mujibu wa Katiba, kanuni za maadili na uongozi za CCM.
Kauli hii ya CCM imetokana na kauli kinzani zinazotolewa na baadhi ya makada wake katika masuala ambayo Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT amekwishayatolea maelekezo ikiwemo suala la tozo na COVID-19.
Shaka Hamdu Shaka,
Katibu wa Halmshauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi.