VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Raha ya ushindi ni kunoga kwake. Raha ya uchaguzi ni kushinda halafu kutamba kama mwenye magamba membamba. Kunyakua kiti cha Urais; viti vya Ubunge na Udiwani kufuatiwe na 'utamu' wa kidemokrasia.
Kati ya mihimili ya dola iliyopo: Serikali, Bunge na Mahakama, Bunge ndiyo uwanja wa kisiasa hasa. Ndipo mshindi wa uchaguzi mkuu anapojitamba na kuonekana akitamba. Anatamba kwa wingi wake; hoja zake na mbwembwe zake nyinginezo.
Bunge hili ni tofauti. Wananchi hawaamini hata lilivyopatikana (wanatilia shaka uhalali wa kura na mchakato wa kuwapata Wabunge). Uwiano uliopo kati ya CCM na vyama vya upinzani Bungeni unatunyima kama chama kutamba na kufurahia ushindi wetu uchaguzini. Tutambe nini ikiwa Bunge 'zima' ni CCM watupu?
Watanzania walio wengi kwasasa hawalifuatilii Bunge kwenye vikao vyake na mijadala yake. Wamelipuuza na kulipotezea. Wanawatazama Wabunge kama wanavyowatazama wajumbe wa NEC au KK ya CCM wanapokutana hukohuko Dodoma. Hakika, Bunge hili ni kama kikao cha CCM.
Ushindi wetu wa 2020 haunogi kabisa. Tumepata lakini tumekwama. Tunatokaje hapo?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Kati ya mihimili ya dola iliyopo: Serikali, Bunge na Mahakama, Bunge ndiyo uwanja wa kisiasa hasa. Ndipo mshindi wa uchaguzi mkuu anapojitamba na kuonekana akitamba. Anatamba kwa wingi wake; hoja zake na mbwembwe zake nyinginezo.
Bunge hili ni tofauti. Wananchi hawaamini hata lilivyopatikana (wanatilia shaka uhalali wa kura na mchakato wa kuwapata Wabunge). Uwiano uliopo kati ya CCM na vyama vya upinzani Bungeni unatunyima kama chama kutamba na kufurahia ushindi wetu uchaguzini. Tutambe nini ikiwa Bunge 'zima' ni CCM watupu?
Watanzania walio wengi kwasasa hawalifuatilii Bunge kwenye vikao vyake na mijadala yake. Wamelipuuza na kulipotezea. Wanawatazama Wabunge kama wanavyowatazama wajumbe wa NEC au KK ya CCM wanapokutana hukohuko Dodoma. Hakika, Bunge hili ni kama kikao cha CCM.
Ushindi wetu wa 2020 haunogi kabisa. Tumepata lakini tumekwama. Tunatokaje hapo?
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam