CCM Temeke ndani ya Kashfa nzito

Taarifa zinazojiri mtandaoni sasa ni tuhuma za ubadhirifu uliofanywa na Mweyekiti wa CCM Wilaya ya Temeke bibie Almishi Hassal, ambaye anatuhumiwa kuunda vikundi hewa vya wanawake na vijana kisha kufanikisha uchotwaji wa zaidi ya Tshs milioni 300 za Halmashauri ya Temeke zilizopaswa kukopeshwa Wanawake, Vijana na Walemavu.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, Almish anatumia madaraka yake kuwatishia watendaji wa Halmashauri wanaofuatilia marejesho kutoka kwa vikundi hivyo hewa.

Sambamba na taarifa hizo, huyu Mwenyekiti wa Wilaya pia alisimama kidete kumtetea yule Mwenyekiti wa Mtaa wa moja ya Mitaa ya Kata ya Toangoma aliyetuhumiwa wizi wa Tshs milion 12 ambapo hadi leo kesi ipo mahakama ya Temeke ikipigwa danadana ili kumlinda mwenyekiti yule mwizi.

Pia hata wananchi wa mtaa ule walipopeleka pendekezo na saini zao kumkataa Mwenyekiti wa Mtaa kwa sababu ana tuhuma zingine za wizi wa milion zaidi ya 20 za wananchi alitumia madaraka yake kuzuia Wilaya kutimiza wajibu wake kwa wananchi hao.

Chanzo.
DarMpya BlogView attachment 2116089
CCM na ufisadi ni sawa na nzi na kinyesi
 
Nadhani huu uchunguzi wa kuwabaini hawa ungefanyika nchi nzima kata kwa kata, mtaa kwa mtaa. Viongozi wengi wanaishi kama mchwa mnakula kweli kweli. Kupata mkopo wa vikundi ni kero unazungushwa kweli. Mara mnaambiwa mwandike Katiba, mkiandika na kuleta inakataliwa baadae mnauziwa na wao hao hao CCM kata Tshs 30000/= mpaka 50000/= . Ili ipitishwe na afisa maendeleo. Huu ni wizi mkubwa kwa vikundi vya watu masikini
Huko kunaitwa kuingia kuingia kwenye 18 za wanachukua chako mapema(ccm)
 
Back
Top Bottom