Tetesi: CCM si wamoja, hamna siri. Kumbe kamati kuu yenu iligawanyika pakubwa kuhusu sakata la kufukuzwa Membe?

Kati ya wajumbe wote wa kamati kuu ni watu watatu tu pamoja na msemaji wao ndiyo waliounga mkono Membe kufukuzwa. Hata aliyeongoza Tume ya Maadili, yaani Mzee Philip Mangula alipinga Membe kuvuliwa uanachama wa chama hicho, imedokezwa.

Wajumbe wengi walipendekeza Benard Membe kufungiwa kufanya siasa ndani ya chama hicho kwa muda maalum kama adhabu mbadala ili kuepuka kukigawa chama.

Adhabu kama hiyo ndiyo alipewa Kinana ambaye hata hivyo haiwezi kumuathiri kwa lolote lile kwani alishaachana na mambo ya siasa. Adhabu hiyo mbadala ilipingwa kwa nguvu zote na Katibu Mkuu wa chama hicho Dr. Bashiru Ally ambaye alisimamia Membe na Kinana kufukuzwa.

Taarifa zilizovuja ndani ya kamati hiyo zinadai kuwa wajumbe wa kikao hicho waliondoka bila ya kupata muafaka wa pamoja huku wababe wanne ambao walisimamia Membe kufukuzwa wakitoka na maamuzi yao.

My take: Upo uwezekano kuwa ndani ya CCM kuna mgogoro unaoendelea licha ya wachache kutuaminisha kuwa wanachama wake ni wamoja. Tusubiri tuone watakaoanza kuunga mkono msimamo wa Membe wazi wazi.

Wazee wa kale hawajawahi kukosea. Ukiona. Mke wa jirani anafuatilia sana ya ndani mwenu ujue HATOSHEKI aliko. So tell us mkuu. Shida yako hasa nini. Tufanye yote hayo kweli. Wewe unahitaji Nini. Mana kama Ni mpinzani wa hicho chama. Bado haitakusaidia.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
C
Hapo ndo huwa naona CCM ina intelejensia ya hali ya juu. Kumwacha Membe ilikuwa hatari zaidi. Huenda Membe mwenyewe alitegemea angefungiwa ila hii ya kumfukuza ni kama imemshtua. Ndo maana kajikuta anaropoka vitu nje vya taaluma yake.
CCM hawana intelijensia yoyoye ya Hali ya juu ndugu yangu.
CCM inategemea vyombo vya Dola.TISS.
 
Bashiru atakuja kuumizwa na miamba ya CCM. Hata UDSM atafukuzwa akalime bamia. Huyu bwana anajisahau sana.

Mangula enzi za Mkapa aliwafanyia figisu wakina Boyz to Men siku wameshika madaraka walimnyoosha mpk akarudi kwao akagombania uenyekiti wa mkoa bado akachinjiwa baharini(from umakamu mwenyekiti wa CCM taifa to uenyekiti wa CCM wa mkoa na bado akaukosa) ikabidi mzee arudi kwny shughuli za kulima Nyanya mpk siku wakina JK walipomuhitaji tena kwa kazi maalumu ndipo akarudishwa.

Bashiru awe makini.
 
Kati ya wajumbe wote wa kamati kuu ni watu watatu tu pamoja na msemaji wao ndiyo waliounga mkono Membe kufukuzwa. Hata aliyeongoza Tume ya Maadili, yaani Mzee Philip Mangula alipinga Membe kuvuliwa uanachama wa chama hicho, imedokezwa.

Wajumbe wengi walipendekeza Benard Membe kufungiwa kufanya siasa ndani ya chama hicho kwa muda maalum kama adhabu mbadala ili kuepuka kukigawa chama.

Adhabu kama hiyo ndiyo alipewa Kinana ambaye hata hivyo haiwezi kumuathiri kwa lolote lile kwani alishaachana na mambo ya siasa. Adhabu hiyo mbadala ilipingwa kwa nguvu zote na Katibu Mkuu wa chama hicho Dr. Bashiru Ally ambaye alisimamia Membe na Kinana kufukuzwa.

Taarifa zilizovuja ndani ya kamati hiyo zinadai kuwa wajumbe wa kikao hicho waliondoka bila ya kupata muafaka wa pamoja huku wababe wanne ambao walisimamia Membe kufukuzwa wakitoka na maamuzi yao.

My take: Upo uwezekano kuwa ndani ya CCM kuna mgogoro unaoendelea licha ya wachache kutuaminisha kuwa wanachama wake ni wamoja. Tusubiri tuone watakaoanza kuunga mkono msimamo wa Membe wazi wazi.
Heart attack ya Mangula si bure, alishtuka misuli ikashindwa kufanya kazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili jambo sio dogo. Yaliyo tokea 2015 yanaweza kutokea 2020 kuhusu "kusukumiziwa" kwa hasira.
Mwezi July akijitokeza mtu mwenye jina fahamika ndani ya nchi hii na kuchukua fomu za kutaka kugombea anaweza "kusukumiziwa" kwa hasira kama alivyosukumiziwa Magufuli mwaka 2015.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi haiwezekani raisi kutokuwa mwenyekiti wa chama chake namaanisha mwwnyekiti awe mfano mzee wa msoga alaf meko awe kama alivyo then akimaliza na yeye anakuwa mwenyekiti then anayeendeleza gurudumu anakuwa raisi ..eet kwwnye uzo katiba zenu hamuwezi badilishaga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bashiru ananua wapinzani kwa hongo. Ni aibu kwa mhadhiri aliyepata kuheshimika Kama yeye. Ni mwalimu mzuri wa sayansi ya siasa na uongozi wa umma lakini si mzuri katika siasa
Bashiru anatumika na jiwe kusimika udikteta ndani ya chama. Bashiru ipo siku atajuta anayoyafanya ndani ya chama.

Ni aibu kwa mhadhiri aliyewahi kuheshimika siku za nyuma. Anaaibisha taaluma yake na anajiwekea alama ya kudumu atakayokufa nayo kwa majuto. Lakini majuto ni mjukuu. Pole sana kadikteta kabashiru.
 
Sasa si kafukuzwa akigawe chama sasa kama ana ubavu
Kati ya wajumbe wote wa kamati kuu ni watu watatu tu pamoja na msemaji wao ndiyo waliounga mkono Membe kufukuzwa. Hata aliyeongoza Tume ya Maadili, yaani Mzee Philip Mangula alipinga Membe kuvuliwa uanachama wa chama hicho, imedokezwa.

Wajumbe wengi walipendekeza Benard Membe kufungiwa kufanya siasa ndani ya chama hicho kwa muda maalum kama adhabu mbadala ili kuepuka kukigawa chama.

Adhabu kama hiyo ndiyo alipewa Kinana ambaye hata hivyo haiwezi kumuathiri kwa lolote lile kwani alishaachana na mambo ya siasa. Adhabu hiyo mbadala ilipingwa kwa nguvu zote na Katibu Mkuu wa chama hicho Dr. Bashiru Ally ambaye alisimamia Membe na Kinana kufukuzwa.

Taarifa zilizovuja ndani ya kamati hiyo zinadai kuwa wajumbe wa kikao hicho waliondoka bila ya kupata muafaka wa pamoja huku wababe wanne ambao walisimamia Membe kufukuzwa wakitoka na maamuzi yao.

My take: Upo uwezekano kuwa ndani ya CCM kuna mgogoro unaoendelea licha ya wachache kutuaminisha kuwa wanachama wake ni wamoja. Tusubiri tuone watakaoanza kuunga mkono msimamo wa Membe wazi wazi.
 
Ila wangemuacha na mwisho wangemkata kama Lowasa mwishoni Ila mm naona kuna vita ccm asilia na wahamiaji na asilia ni wengi na kiongozi wao ni membe naye wamemkata kichwa je wafuasi wake wanasubiri bunge livunje ili wasikose potepote wahamiaji kiongozi wao Rais magufuli,Bashiru,Polepole
 
48 Reactions
Reply
Back
Top Bottom