CCM sasa yapoteza mwelekeo baada ya agizo la JK la kutotegemea polisi kuidhibiti Chadema

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233



Hii ni dhahiri sasa baada ya tukio lile la Mgololo Iringa ambapo polisi walipofikia siku zao 40 – baada kujikuta wanaaibika katika jitihada zao za kuitumikia CCM kwa lengo la kuionyesha CDM kuwa ni chama cha vurugu.

Baada ya hilo tukio ambalo mbali na kuiabisha polisi, bali pia serikali ya CCM lilimpelekea JK kuagiza/kutoa angalizo k,wa makada wa chama chake kwamba waache kutegemea polisi katika kudhibiti makada wa CDM na hoja zao na badala yake wajibu hoja zao.

Kujibu hoja za msingi za makada wa CDM imekuwa kazi ngumu kwa watu kama Nape hadi kufikia sasa anaaingiza mambo mengine yasiyohusu eti Slaa bado ana kadi ya CCM.
 
Nape amekosa hoja,eti anakimbilia kutafuta kadi za zamani kama Rupia..yake ya CCJ ameiweka wapi? Anafaidi mafao ya mzee wake coz watoto wa vigogo wanafaidi Gambani.
 
Mbona hoja zinajibiwa humu? wewe unataka kila hoja hata ya kipuuzi zijibiwe? huko kupoteza muda bora kuwaacha wakiumana mara Jimbo la Kawe linatafutiwa Mgombea Mwingine badala ya halima Mdee mara Nape katangaza Dr Slaa ana kadi ya CCM bado Lazima uangalie ni wapi panaswihi sio kila Hoja unachangia ili ttu uonekane ww ni shabiki MAGWANDA au MAGAMBA Post km hii https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-wageuka;-ccm-juu-chadema-hakieleweki-3.html Mchangiaji MAFILILI anaulizwa wewe ni Chama gani? au mtu anatoka povu asisikie CDM imesemwa au Matusi km UHARO
quote_icon.png
By Ellyson
Bado hujajibu ulivyoulizwa wewe ni mfuasi wa chama gani? Au ukilipwa 2 hivyo viposho vya mlo mmoja unaridhika nakuja kumwaga uharo humu?
 
Last edited by a moderator:
Mie nilijua tu hili litatokea -- CCM walibweteka sana chini ya mwavuli wa polisi. nami nadhani kuanzia sasa polisi hawatakuwa wanafanya mambo yao hayo ya kijinga ya eti kuonesha umma kuwa CDM ni chama cha vurugu.

nashauri kuanzia sasa polisi waelekeze nguvu zao kuwashughulikia wezi wa mali na rasilimali za umma ambao wamo kibao ndani ya CCM na serikali yake.
 
akuna kinachoweza kudhibiti nguvu ya umaa, ccm muda umefika sasa yapasa kua chama cha upinzani:majani7:
 
Mwelekeo upi acheni za mfa maji nyie hamlali jinamizi la ccm kiboko eee
 
Nasikia baadhi ya vigogo na makada wa CCM wamehuzunishwa sana na kauli hiyo,ya JK kuhusu mbeleko ya polisi kutowabeba.
 
Nape amekosa hoja,eti anakimbilia kutafuta kadi za zamani kama Rupia..yake ya CCJ ameiweka wapi? Anafaidi mafao ya mzee wake coz watoto wa vigogo wanafaidi Gambani.

WANA CCM WENYE BUSARA NA AKILI LZM WANAMUONA NNAPE KAMA JANGA JINGINE LA KUWADHOOFISHIA CHAMA KM ILVOKUA KWA MKAMA MAANA ANAROPOKA SANA, TENA ANAROPOKA UJINGA, MF. KUDAI KADI TOKA KWA DR SLAA NI UJINGA KWANI ALVOKUWA MBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA NI WAZI UKO MAGAMBANI ALIKUA AMEAMA, NA SJUI WATAMSAFISHAJE BWANA JANGILI KINANA, TNASUBILI MAJIBU JUU YA MELI YAKE ILOKAMATIWA HONGKONG NA PEMBE ZA NDOVU, KAGASHEKI TNATAKA MAJIBU JUU YA UYU JANGILI WA KISOMALi
 
Vipi Kamuhanda,Senso,Mwema,Chagonja?hawajaumbuka na kiherehere cha kujipendekeza kwa Magamba?JK kiboko amewatoa nishai kiaina sana amewazunguka na kuwaonyesha kuwa wanaharibu demokrasia na siasa za vyama,acha vyama vijibizane kwa sera na mikutano,wao walinde amani tu!sio kuzuia mikutano
 
Kwa mtazamo wangu naiona Jk ameagiza hivyo kwa sababu yeye has nothing to lose kwani anamaliza baada ya miaka 3, na yampate ajaye.

Hivi EL akishika nchi kwa mfano, ataruhusu tena kamchezo ka kutumia polisi kuudhibiti upinzani?
 
Kwa mtazamo wangu naiona Jk ameagiza hivyo kwa sababu yeye has nothing to lose kwani anamaliza baada ya miaka 3, na yampate ajaye.

Hivi EL akishika nchi kwa mfano, ataruhusu tena kamchezo ka kutumia polisi kuudhibiti upinzani?

Be careful! Kwa nini unatoa assumption, enormous assumption - kwamba CCM hakitakuwa chama cha upinzani ifikapo January 2016?
 
Aibu kubwa sana kwa jeshi la polisi , wamejipendekeza weee ! halafu wameumbuka , unajua KIKWETE hakukusudia kuweka wazi hilo jambo ! Bali wachunguzi wanadai lilimtoka kwa bahati mbaya tu ( presha ya kofia mbili ) , kweli mungu si Athumani kwani hamfichi mnafiki ! Kama mimi ningekuwa IGP ningejiuzulu kwa ajili ya heshima yangu , na kwa taarifa tu ni kwamba rushwa imebainika na kila mtu nchi hii , silaha pekee iliyotegemewa ilikuwa polisi na TISS ( kuteka , kunyanyasa , kushughulikia , kuua n.k ) ,bila hivyo hakuna CCM .
 
Kwa mtazamo wangu naiona Jk ameagiza hivyo kwa sababu yeye has nothing to lose kwani anamaliza baada ya miaka 3, na yampate ajaye.

Hivi EL akishika nchi kwa mfano, ataruhusu tena kamchezo ka kutumia polisi kuudhibiti upinzani?

Hivi bado kuna mbumbumbu humu JF wanaamini Edward Lowasa , yule aliyepangisha jengo la Uvccm kwa miaka 99 na MHUSIKA mkuu wa RICHMOND aliyeng'oka kwa aibu na majonzi makubwa , anaweza kuwa rais wa nchi kweli !
 
CCM hakiwezi fare play hilo lipo wazi kama sio kubebwa na USALAMA WA TAIFA leo tungekuwa tunaongea story nyingine, hiki chama kimechoka, kama ni timu ya mpira basi haina first eleven, hembu cheki kinavyobadili wachezaji (Mawaziri, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu wa chama) kila uchwao, lakini wapi safu ya ushambuliaji (MAWAZIRI) ni butu, viungo wachezeshaji (NAPE,MUKAMA na wenzake) hao ndio wamechoka kabisa, sijui hawa walioingizwa dakika za mwisho (KINANA,MANGULA NA WENZAKE) Kocha wao (MH.RAIS) naye mbinu zimemuishia washabiki (WANACHAMA) wamebaki kusema anaangushwa na wachezaji, kama sio waamuzi (TUME YA UCHAGUZI) CCM ingeshindwa vibaya katika mechi iliyopita (UCHAGUZI 2010).

Kuna mshambuliaji wao mmoja yupo nje ya uwanja (LOWASA) huyu inasemekana ni majeruhi ana kadi nyekundu lakini pia nasikia haivi na kocha baadhi ya washabiki wanasema pengine asingecheza rafu akatolewa nje kwa kadi nyekundu angeweza kuisaidia timu yake, sijui itakuwaje katika mechi ijayo kwani nasikia kocha anamaliza muda wake na bado hajapata kikosi cha kwanza.
 
CCM hakiwezi fare play hilo lipo wazi kama sio kubebwa na USALAMA WA TAIFA leo tungekuwa tunaongea story nyingine, hiki chama kimechoka, kama ni timu ya mpira basi haina first eleven, hembu cheki kinavyobadili wachezaji (Mawaziri, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu wa chama) kila uchwao, lakini wapi safu ya ushambuliaji (MAWAZIRI) ni butu, viungo wachezeshaji (NAPE,MUKAMA na wenzake) hao ndio wamechoka kabisa, sijui hawa walioingizwa dakika za mwisho (KINANA,MANGULA NA WENZAKE) Kocha wao (MH.RAIS) naye mbinu zimemuishia washabiki (WANACHAMA) wamebaki kusema anaangushwa na wachezaji, kama sio waamuzi (TUME YA UCHAGUZI) CCM ingeshindwa vibaya katika mechi iliyopita (UCHAGUZI 2010). Kuna mshambuliaji wao mmoja yupo nje ya uwanja (LOWASA) huyu inasemekana ni majeruhi ana kadi nyekundu lakini pia nasikia haivi na kocha baadhi ya washabiki wanasema pengine asingecheza rafu akatolewa nje kwa kadi nyekundu angeweza kuisaidia timu yake, sijui itakuwaje katika mechi ijayo kwani nasikia kocha anamaliza muda wake na bado hajapata kikosi cha kwanza.

Nakuunga mkono kwa usemayo, ni kweli tupu.
 
CCM hakiwezi fare play hilo lipo wazi kama sio kubebwa na USALAMA WA TAIFA leo tungekuwa tunaongea story nyingine, hiki chama kimechoka, kama ni timu ya mpira basi haina first eleven, hembu cheki kinavyobadili wachezaji (Mawaziri, wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa, makatibu wakuu wa chama) kila uchwao, lakini wapi safu ya ushambuliaji (MAWAZIRI) ni butu, viungo wachezeshaji (NAPE,MUKAMA na wenzake) hao ndio wamechoka kabisa, sijui hawa walioingizwa dakika za mwisho (KINANA,MANGULA NA WENZAKE) Kocha wao (MH.RAIS) naye mbinu zimemuishia washabiki (WANACHAMA) wamebaki kusema anaangushwa na wachezaji, kama sio waamuzi (TUME YA UCHAGUZI) CCM ingeshindwa vibaya katika mechi iliyopita (UCHAGUZI 2010).

Kuna mshambuliaji wao mmoja yupo nje ya uwanja (LOWASA) huyu inasemekana ni majeruhi ana kadi nyekundu lakini pia nasikia haivi na kocha baadhi ya washabiki wanasema pengine asingecheza rafu akatolewa nje kwa kadi nyekundu angeweza kuisaidia timu yake, sijui itakuwaje katika mechi ijayo kwani nasikia kocha anamaliza muda wake na bado hajapata kikosi cha kwanza.

kaka umetisha kama ukoma!
 
Inawezekana polisi wama-lie low kwa muda tu. Upepo ukitulia wataanza kufanza mambo yao kama kawaida.
 
Inawezekana polisi wama-lie low kwa muda tu. Upepo ukitulia wataanza kufanza mambo yao kama kawaida.

Inawezekana, lakini CDM wamepata nguvu mpya inayotambuliwa hata na JK. Kitu ambacho huwa nafikiria ni kwamba iwapo wapinzani watatwaa nchi, hawa mapoliccm, hususan viongozi wao wataweka sura zao wapi/ namaananisha wary kama akina Chagonja, Kamuhanda, Kova, Shilogile na wengineo.
 
Back
Top Bottom