CCM sasa wamtumia Warioba kuimaliza CHADEMA?

Joblube

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
369
151
Nimesoma habari ya Jaji Warioba katika gazeti la Raia Mwema la leo, nikagundua kuwa CCM bado inafikiri kuwa Watanzania kuwa ni wajinga kiasi hicho, wanachofikiri wao ni kuwa bado kuna watu wanaweza kufikiri vizuri kwa ajili ya watu wengine.

Kingine nilichogundua ni kuwa CCM wanaweweseka, na CCM ndio itakayoleta vurugu nchi hii kwa kuwa haiko tayari kushindwa kidemokrasia yamejidhihirisha katika mazungumzo hayo ya Jaji Warioba.

Lingine nililojifunza ni kuwa CCM sasa wanatumia mbinu zozote zile zidi ya CHADEMA kuwa kuwa haiwezi tena kushindana na CHADEMA kisera imebakia kuropoka, sasa wamebuni mbinu za kuwatumia watu maarufu kama Warioba kujifanya wanazunguzia mustakabali wa nchi bila upendeleo huku wakiingiza maoni ya kuiponda CHADEMA.

Warioba anasema Chadema kule igunga wasifikiri wanapanda chati ile inaweza kuwa nguvu ya soda halafu anaingiza propaganda za CCM za udini na kuwa CHADEMA si chama cha watu.

Tumuulize Warioba atupe data zinazoonyesha kuwa kule si kupanda chati bali ni nguvu za soda si kuzungumza kisiasa na kinadharia. Wengine sisi si wanasiasa tunataka analysis and fact.

Angalizo kwa CHADEMA ni kuwa kuna nguvu iliyo nyuma ya pazia ya kuiangamiza ambayo ni kubwa sana, sasa hivi wanawatumia wakongwe hao wameanza na Warioba, atafuata Salim, gazeti la Raia Mwema limeshachukuliwa! Kumbuka Warioba na Jenerali na Mkapa walikuwa marafiki wakubwa sana kabla ya wawili wao hawajagombana.

Mimi nimefanya kazi kwa Jenerali Ulimwengu wakati wanaanzisha gazeti la Mtanzania nawafahamu vizuri.

Watanzania tusikubali kuruhusu watu kufikiri kwa niaba yetu, CCM hawako tayari kuona chama kingine kwa kuwa wanaogopa utawala mwingine kwa kuwa wanajua katika CCM hakuna aliyemsafi kamili. Watajifanya kujikosoa wenyewe ili wabaki madarakani ili kulinda madhambi yao. Tuendelee kupambana mapaka ukombozi kamili upatikane.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Mkuu mabadiliko yanatokea sasa hivi nchini na nchi zingine ni ya lazima kutokea kutokana na mwamko wa watu kila kona.

Teknolojia ya habari imesaidia sana watu kuelewa nini pumba na nini mchele, kinachotakiwa ni hao ndugu zetu wa kijijini kupata ujumbe na kuwatoa uoga.

Serikali saizi inaishi wa kuvitisho, watu wengi huko vijijini mfano Ukenyenge kijijini kwangu wanamwamko, hawadanganyiki.

CCM waendelee kutumia vitisho ila the changes are non-stoppable. Mabadiliko yatatokea nchi zote jirani, Tanzania watayazuia na nini? Kwa mikwara, No no no way! Kwa risasi? No no no no! kwa kuchakachua kura?

Tusubiri watu watakaoandikishwa; safari hii ni mguu kwa mguu hakuna mtu kuibiwa.
 
Kila anayejaribu kushauri, kuonya, kukemea baadhi ya mapungufu ya CHADEMA mtasema anatumiwa na CCM. Hivi kama mtu au chama unakipenda utakaa kimya tu na kukisifia hata kama unaona kinakoelekea siko? Sasa hivi Jaji Warioba anajaribu kuwa juu kidogo ya siasa za vyama. Jana alivikosoa vyama vyote ikiwemo CCM yake. Wewe umeyaona maoni haya ya CHADEMA tu. Kwa namna ulivyoleta, utaungwa mkono sana tu humu JF. Umeongea lugha ya wengi humu.
 
Kushindana kwa sera. Sera zipi? Ninachojua ni kwamba Chadema wamaekuwa tu wakosoaji bila kueleza ni kipi walichoandaa ambacho watawaletea wananchi iwapo wataingia madarakani. Ni kulia lia na kulalamika wakati kwenye majimbo wanayoyaongoza hali ni hoi bin taabani na wala huoni kama kuna kitu kinachoweza kuipambanua Chadema na CCM na kuwapa watu matumaini kwamba chama hicho ni mbadala wa CCM.
 
Huyu fisadi mzee naye anatafuta pa kufia, anafikiri tumesahau ile ishu yake ya Mwananchi Gold? Akafie mbali huyo kikongwe.
 
Yeye Warioba amelifanyia nini taifa hili hadi atuchagulie chama. Ameshiriki katika ufisadi wa madini, ni fisadi tu kama mafisadi wengine. Hana mashiko katika jamii na alipewa madaraka na Mwalimu kwa vile wanatokea njia moja, sio objectively. Ni mmoja wa viongozi wanaodaiwa na nchi hii kwa umaskini huu tulionao na miaka 50 ya uhuru. Hakuna atakayejali kauli zake zaidi ya sisi vijana kujiuliza huyu mzee atakufa lini atuachie nchi yetu aliyoinyonya enzi za uhai wake?
 
Nimesoma habari ya Jaji Warioba katika gazeti la Raia Mwema la leo, nikagundua kuwa CCM bado inafikiri kuwa Watanzania kuwa ni wajinga kiasi hicho, wanachofikiri wao ni kuwa bado kuna watu wanaweza kufikiri vizuri kwa ajili ya watu wengine.

Kingine nilichogundua ni kuwa CCM wanaweweseka, na CCM ndio itakayoleta vurugu nchi hii kwa kuwa haiko tayari kushindwa kidemokrasia yamejidhihirisha katika mazungumzo hayo ya Jaji Warioba.

Lingine nililojifunza ni kuwa CCM sasa wanatumia mbinu zozote zile zidi ya CHADEMA kuwa kuwa haiwezi tena kushindana na CHADEMA kisera imebakia kuropoka, sasa wamebuni mbinu za kuwatumia watu maarufu kama Warioba kujifanya wanazunguzia mustakabali wa nchi bila upendeleo huku wakiingiza maoni ya kuiponda CHADEMA.

Warioba anasema Chadema kule igunga wasifikiri wanapanda chati ile inaweza kuwa nguvu ya soda halafu anaingiza propaganda za CCM za udini na kuwa CHADEMA si chama cha watu.

Tumuulize Warioba atupe data zinazoonyesha kuwa kule si kupanda chati bali ni nguvu za soda si kuzungumza kisiasa na kinadharia. Wengine sisi si wanasiasa tunataka analysis and fact.

Angalizo kwa CHADEMA ni kuwa kuna nguvu iliyo nyuma ya pazia ya kuiangamiza ambayo ni kubwa sana, sasa hivi wanawatumia wakongwe hao wameanza na Warioba, atafuata Salim, gazeti la Raia Mwema limeshachukuliwa! Kumbuka Warioba na Jenerali na Mkapa walikuwa marafiki wakubwa sana kabla ya wawili wao hawajagombana.

Mimi nimefanya kazi kwa Jenerali Ulimwengu wakati wanaanzisha gazeti la Mtanzania nawafahamu vizuri.

Watanzania tusikubali kuruhusu watu kufikiri kwa niaba yetu, CCM hawako tayari kuona chama kingine kwa kuwa wanaogopa utawala mwingine kwa kuwa wanajua katika CCM hakuna aliyemsafi kamili. Watajifanya kujikosoa wenyewe ili wabaki madarakani ili kulinda madhambi yao. Tuendelee kupambana mapaka ukombozi kamili upatikane.

Mungu ibariki Tanzania.

Poti anaota kuwa Waziri Mkuu tena kama Machina anavyoota kuwa Rais.
 
Kila anayejaribu kushauri, kuonya, kukemea baadhi ya mapungufu ya CHADEMA mtasema anatumiwa na CCM. Hivi kama mtu au chama unakipenda utakaa kimya tu na kukisifia hata kama unaona kinakoelekea siko? Sasa hivi Jaji Warioba anajaribu kuwa juu kidogo ya siasa za vyama. Jana alivikosoa vyama vyote ikiwemo CCM yake. Wewe umeyaona maoni haya ya CHADEMA tu. Kwa namna ulivyoleta, utaungwa mkono sana tu humu JF. Umeongea lugha ya wengi humu.
Ni kweli kabisa mkuu. KInachotuumiza watanzania hivi sasa ni kuzama zaidi kwenye siasa za vyama. Mbaya zaidi, hata humo kwenye siasa za vyama tunaangalia mambo kwa ushabiki kuliko dhamira ya kusaidia kulikwamua taifa. Ni wakati sasa tukaibuka juu ya siasa za vyama na kuiangalia Tanzania kama Taifa, hasa wakati huu tunapoadhimisha miaka 50 baada ya Uhuru
 
Kushindana kwa sera. Sera zipi? Ninachojua ni kwamba Chadema wamaekuwa tu wakosoaji bila kueleza ni kipi walichoandaa ambacho watawaletea wananchi iwapo wataingia madarakani. Ni kulia lia na kulalamika wakati kwenye majimbo wanayoyaongoza hali ni hoi bin taabani na wala huoni kama kuna kitu kinachoweza kuipambanua Chadema na CCM na kuwapa watu matumaini kwamba chama hicho ni mbadala wa CCM.

Kama wananchi wanalia na kulalamika unategemea wanasiasa wanaowapresent wafanyeje? wachekecheke.
Wakati wa Kampeni DR SLAA alisema hana mpango wa kubadilisha sheria hata moja atakachokifanya
ni kuzisimamia kwa uadilifu mkubwa sheria zilizopo. bado hapo hauoni utafauti wa kisera na serikali ya
Jakaya ambayo haiko tayari kusimamia sheria zaidi ya kutuongoza kuzivunja?

well, Hakuna mtu anategemea tutakuwa na chama perfect kama vile kimeteremshwa kutoka mbinguni.
CHADEMA wanaweaknesses zao, tuzipima na za CCM ni sawa na kulinganisha harufu ya mavi na ua rose.
why do you insist comparing these two, by the way, hata tukikomaa kuisafisha CHADEMA mpaka ikawa
nyeupe kama saruji haitotuletea unafuu kwenye maisha yetu immedietly, haitazuia vifo vya mama wajawazito
na vichanga vyao kwa kukosekana huduma bora za uzazi wa afya as soon as possible, haitashusha bei ya
sukari, mkate wala unga, haitaleta solution ya kupunguza ajali za barabarani za kimfumo.

Its just different, tunategemea katika kuikosoa CCM, ijirekebishe na hivyo kufungua milango ya kuboresha
maisha yetu, surprisingly this does not happen. so what do we do? remove them.

Hatutaki kuwa confused na agenda za kutuelekeza kufikiria wala kujishughulisha na issues ambazo
hazina manufaa kwenye maisha yetu, tumekuwa conviced kwamba kuiondoa CCM madarakani
ndio solution.
 
Walioba hana legacy yoyote,na yeye ni gamba tu.mbona ni mweyekiti wa council pale udsm na kuna madudu mengi yanafanyika tu chini yake.TUPA KULE
 
Nimesoma habari ya Jaji Warioba katika gazeti la Raia Mwema la leo, nikagundua kuwa CCM bado inafikiri kuwa Watanzania kuwa ni wajinga kiasi hicho, wanachofikiri wao ni kuwa bado kuna watu wanaweza kufikiri vizuri kwa ajili ya watu wengine.

Kingine nilichogundua ni kuwa CCM wanaweweseka, na CCM ndio itakayoleta vurugu nchi hii kwa kuwa haiko tayari kushindwa kidemokrasia yamejidhihirisha katika mazungumzo hayo ya Jaji Warioba.

Lingine nililojifunza ni kuwa CCM sasa wanatumia mbinu zozote zile zidi ya CHADEMA kuwa kuwa haiwezi tena kushindana na CHADEMA kisera imebakia kuropoka, sasa wamebuni mbinu za kuwatumia watu maarufu kama Warioba kujifanya wanazunguzia mustakabali wa nchi bila upendeleo huku wakiingiza maoni ya kuiponda CHADEMA.

Warioba anasema Chadema kule igunga wasifikiri wanapanda chati ile inaweza kuwa nguvu ya soda halafu anaingiza propaganda za CCM za udini na kuwa CHADEMA si chama cha watu.

Tumuulize Warioba atupe data zinazoonyesha kuwa kule si kupanda chati bali ni nguvu za soda si kuzungumza kisiasa na kinadharia. Wengine sisi si wanasiasa tunataka analysis and fact.

Angalizo kwa CHADEMA ni kuwa kuna nguvu iliyo nyuma ya pazia ya kuiangamiza ambayo ni kubwa sana, sasa hivi wanawatumia wakongwe hao wameanza na Warioba, atafuata Salim, gazeti la Raia Mwema limeshachukuliwa! Kumbuka Warioba na Jenerali na Mkapa walikuwa marafiki wakubwa sana kabla ya wawili wao hawajagombana.

Mimi nimefanya kazi kwa Jenerali Ulimwengu wakati wanaanzisha gazeti la Mtanzania nawafahamu vizuri.

Watanzania tusikubali kuruhusu watu kufikiri kwa niaba yetu, CCM hawako tayari kuona chama kingine kwa kuwa wanaogopa utawala mwingine kwa kuwa wanajua katika CCM hakuna aliyemsafi kamili. Watajifanya kujikosoa wenyewe ili wabaki madarakani ili kulinda madhambi yao. Tuendelee kupambana mapaka ukombozi kamili upatikane.

Mungu ibariki Tanzania.

kwa kufungamana na CCM gazeti la raia mwena ndo linakufa, Ulimwengu hajajifunza kikichomfanya akaikimbia habari corp.
 
Kila anayejaribu kushauri, kuonya, kukemea baadhi ya mapungufu ya CHADEMA mtasema anatumiwa na CCM. Hivi kama mtu au chama unakipenda utakaa kimya tu na kukisifia hata kama unaona kinakoelekea siko? Sasa hivi Jaji Warioba anajaribu kuwa juu kidogo ya siasa za vyama. Jana alivikosoa vyama vyote ikiwemo CCM yake. Wewe umeyaona maoni haya ya CHADEMA tu. Kwa namna ulivyoleta, utaungwa mkono sana tu humu JF. Umeongea lugha ya wengi humu.
Mkubwa umenena tatizo hatutaki kuambiwa ukweli waungwana!!
 
Huyu fisadi mzee naye anatafuta pa kufia, anafikiri tumesahau ile ishu yake ya Mwananchi Gold? Akafie mbali huyo kikongwe.

Ama Kweli Chadema mnaonesha ni jinsi gani heshima Huyo unaye mtukana na Sawa na baba yako na pia aliwahi kuwa kiongozi Wa nchi hii. Hivi nikweli hakuna alichokifanya alipokuwa madarakani? Au umezaliwa juzi hujuwi tulikotoka? Achani siasa za chuki
 
Nilkuwa namuheshimu sana Warioba lakini sasa naona anakoelekea atapoteza heshima yake,anazeeka vibaya na hiyo mipombe na umri wake inabidi anywe Casstle lite.
 
Wimbi laja na tufani hakuna wa kulizuia. Hao wanaotumiwa sasa ndio waliotufikisha hapa kwenye lindi la umaskini. WEacha waongee tu baragumu la mabadiliko limelia na watu wanajifunga kibwebwe kjusonga mbele. Wakijiingiza katika siasa basi walipuliwe hadharani na kukitokea mabadiliko mali zao zitaifishwe. Mungu yupo na waja wake katika mpambano huu. Tuwapuuze hao wanaozuia kusonga mbele,
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom