Pamoja na kwamba maneno yake yana ukweli fulani lakini kuna jambo amelisema kwa mafumbo,anaposema "CDM inafanya operation sangara uvccm na ccm wakiangalia tu'' hapa sijaelewa anamaanisha nini,nadhani anataka wawadhibiti au anataka nao wapite mitaa na vitongoji kujinadi?Tumeshuhudia vyombo vyote vya dola vikiwaandama wapinzani na kuwawekea vipingamizi wasifanikishe malengo yao na sehemu nyingine wamesababisha vifo.Je hayo hayajamridhisha Kingunge? je anataka Tendwa avifungie vyama hivi ndo ataona wanafanya kazi? Siamini kama mzee huyu kazeeka bali anahamasisha vurugu,anaposema ccm anamaanisha polisi na wengineo na anaposema uvccm anamaanisha green guard ambapo tumeshuhudia vikundi hivi vikitenda kinyume cha sheria dhidi ya vyama vya upinzani.
Mimi naamini kiongozi yeyote mstaafu anayetoa mawazo natamani azungumze juu ya kuijenga tanzania na siyo chama fulani maana hakuna chama chochote kitakachotawala milele katika zama hizi za demokrasia.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.