Azarel
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 26,056
- 33,915
Habarini Wadau,
Ninasema wazi kabisa ninachokishuhudia katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura katika kuchagua viongozi wa serikali za mitaa, yaani Wenyeviti wa Kijiji, wenyeviti wa Kitongoji na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya vijiji.
Kwakweli katika Wilaya nyingi wananchi HAWAJIANDIKISHI KABISA, kwa anayebisha apite katika vitongoji karibu vyote, Wananchi hawataki kujiandikisha.
SABABU WANAZOTOA :- Wengi wa wananchi wanalalamika kwa kubanwa kwa wagombea wao wa vyama vya upinzani ambao walikuwa tayari kuwachagua.
Unakutana na wananchi wanakuambia wazi kabisa ''Sina muda mchafu'' wa kujiandikisha na kupiga kura kwasababu watakaoshinda kwa hila na nguvu wanajulikana.
Nailaumu CCM, hususan Mwenyekiti wao aliyewanyima wapinzani haki yao ya kujieleza kwa Wananchi wao.
Sasa naona wanaoweweseka sana ni haohao viongozi wa CCM, kwa kulaumu mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara kuwa ndio hawajafanya uhamasishaji kwa wananchi ili wajiandikishe.
Mh. Suleiman Jaffo, Waziri wa Nchi O.R TAMISEMI amewashitaki kwa Rais wasimamizi wote wa mikoa hii ya Kaskazini kwamba uandikishaji ni hafifu Mnoo kwakuwa hawajahamasisha. Haijatosha ametoa agizo kuwa sasa ni lazima wananchi waandikishwe kwa zaidi ya 50%
Kingine tena, Leo wasimamizi wameagiza tena waandikishaji wapite nyumba kwa nyumba kuandikisha.
Waandikishaji nao wanagoma kwenda mpaka walipwe kwasababu sehemu nyingi zipo remoted na mbali...na pia ni kazi ngumu kwakuwa mwanzoni walikubaliana kukaa katika vituo rasmi vya kuandikishia.
SWALI LA MSINGI : Kwanini mnalazimisha watu kujiandikisha?
Hata sehemu isiyo na Upinzani kabisa kama Same na tambarare ya Mwanga ambapo CCM inatawala siku zote pia wananchi wengine hawajiandikishi.
TATIZO NI NINI?
Siku zote ''Mshahara wa Dhambi ni Mauti''
Haya ni Mauti kwa upande wa kaskazini.
Ninasema wazi kabisa ninachokishuhudia katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura katika kuchagua viongozi wa serikali za mitaa, yaani Wenyeviti wa Kijiji, wenyeviti wa Kitongoji na Wajumbe wa Halmashauri kuu ya vijiji.
Kwakweli katika Wilaya nyingi wananchi HAWAJIANDIKISHI KABISA, kwa anayebisha apite katika vitongoji karibu vyote, Wananchi hawataki kujiandikisha.
SABABU WANAZOTOA :- Wengi wa wananchi wanalalamika kwa kubanwa kwa wagombea wao wa vyama vya upinzani ambao walikuwa tayari kuwachagua.
Unakutana na wananchi wanakuambia wazi kabisa ''Sina muda mchafu'' wa kujiandikisha na kupiga kura kwasababu watakaoshinda kwa hila na nguvu wanajulikana.
Nailaumu CCM, hususan Mwenyekiti wao aliyewanyima wapinzani haki yao ya kujieleza kwa Wananchi wao.
Sasa naona wanaoweweseka sana ni haohao viongozi wa CCM, kwa kulaumu mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara kuwa ndio hawajafanya uhamasishaji kwa wananchi ili wajiandikishe.
Mh. Suleiman Jaffo, Waziri wa Nchi O.R TAMISEMI amewashitaki kwa Rais wasimamizi wote wa mikoa hii ya Kaskazini kwamba uandikishaji ni hafifu Mnoo kwakuwa hawajahamasisha. Haijatosha ametoa agizo kuwa sasa ni lazima wananchi waandikishwe kwa zaidi ya 50%
Kingine tena, Leo wasimamizi wameagiza tena waandikishaji wapite nyumba kwa nyumba kuandikisha.
Waandikishaji nao wanagoma kwenda mpaka walipwe kwasababu sehemu nyingi zipo remoted na mbali...na pia ni kazi ngumu kwakuwa mwanzoni walikubaliana kukaa katika vituo rasmi vya kuandikishia.
SWALI LA MSINGI : Kwanini mnalazimisha watu kujiandikisha?
Hata sehemu isiyo na Upinzani kabisa kama Same na tambarare ya Mwanga ambapo CCM inatawala siku zote pia wananchi wengine hawajiandikishi.
TATIZO NI NINI?
Siku zote ''Mshahara wa Dhambi ni Mauti''
Haya ni Mauti kwa upande wa kaskazini.