Mchungaji,
... Wapigaji wa aina hii wakipewa chakula cha wiki moja na kuambiwa waipigie CCM, watafanya hivyo bila kuwa na mapenzi yoyote kwa CCM. ...
Jasusi,
Sijasahau kuwa CCM ni chama cha Wakulima na Wafanyakazzi, ila ninachoendelea kushangaa ni Upumbavu wa Wana CCM na Watanzania kama BAK anavyouzungumzia na ndiyo maana nikiangalia kwa undani haya mapenzi yasiyo na msingi, ni dhahiri Watanzania wameridhika na CCM.
Si kwamba ni Wajinga, bali ni Upumbavu wa kuridhika na ukipima kuridhika kwao ndiko utaona hayo niliyoyaeleza juu, kuwa ni woga wa mabadiliko.
Hivi mpaka wakati huu, ni vipi mada hii inaelekea? Baada ya CCM kujitangaza kujivua gamba na kuwa karibu zaidi na wananchi, je bado CCM ni mtaji kwa Watanzania?
Jasusi,
Kama ni wajanja wachache, kura zao haziwe kuleta landslide, wao ni kundi dogo sana hata kama ni watoa rushwa. Ukitafakari kwa nini Watanzania ni waoga kukipigia kura chama kingine, si suala la kurubuniwa kwa Pilau bali inabidi tukubali kuwa kuna mengine yanayowafanya Watanzania wawe na mapenzi ya ajabu na CCM
natumaini ni rev. Wa kweli. Waliopiga kura ni 40% ya waliojiandikisha. 61% za rais wa nec ni sawa na kura za waliojiandikisha 24.4% ina maana 75.6% ya wapiga kura hawakumpigia kura rais wa nec. Kwa hesabu ndogo tu hiyo naomba uwatake radhi watanzania.
Kura hizo 61% kwa taarifa sahihi ya matokeo halali zilikuwa ni 27% ikiwa ina maana 34% ziliibwa toka vyama vya "upinzani"/vingene ukirudia hesabu kwa 40% ya wapiga kura alipata 10.8% ya waliojiandikisha. 89.2% ya waliojiandikisha hawakumchagua. Kwa hilo pia tafadhali tutake radhi watanzania.
Vyama vya "upinzani"/vingine viliibiwa 34% za waliopiga kura ukijumlisha na na 39% zilizotangazwa unapata 73% ya waliojiandikisha walichagua vyama vya upinzani ambayo ni sawa na 29.2% kwa 40% yawapiga kura.
Tafadhali utuelewe baadhi yetu watanzania na ujiulize maswali mawili tu.
1. Kwa nini 60% hawakupiga kura? Jibu ni kwa sababu ya uchaguzi dola
2. Kwa nini kura za urais haziwi contested mahakamani? Jibu ni lile lile la hapo juu.
Tufanye
1. Hakuna kukata tamaa kwani kila jambo lina mwisho
2. Mabadiriko ya katiba kama hayatakuwa na mizengwe ya kidola hapo utatuhukumu. Lakini yakienda bila mizengwe ya kikatiba utapata kauli sahihi ya watanzania wote watakaopiga kura
mwisho nakushauri rev. Kuna mabadiriko ya aina mbili:-
- ya uasilia (evolutionery) haya yana nguvu kuliko dola.
nadhani sisi watanzania tunapitia kwenye mchanganyiko wa hayo yote. Mshindi ni tanzania yenye neema
- (revolutionery) ambayo ya msuguano mkali na yana athari.