Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA Dr Wilbrod Slaa amesema kumteua Abdulrahman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM ni sawa tu na kumhamisha mgonjwa mahututi-CCM kutoka hospitali ya Mukama na kumhamishia hospitali ya Kinana ambapo mwisho wake ni kifo tu kwa huyo mgonjwa.
Akihutubia maelfu kwa maelfu ya wananchi wa Karagwe jana Dr Slaa anayetambulika kama Rais wa mioyo ya watu alisema kwa sasa CDM imekuja na mkakati mpya ambao ni kuwahamasisha wananchi maeneo ya vijijini na kuepuka kasumba ya kufanya mikutano mijini tu.Amesema ataliongoza jeshi la CDM kujichimbia vijijini ili kazi ya kuizika CCM 2015 iwe nyepesi kabisa.
Katika mkutano huo wanachama 324 walijitoa CCM na kujiunga na CDM.Pia CDM ilitoa kadi kwa wanachama wapya 1836.
Kwa takriban siku tatu sasa Dr Slaa amekuwa gumzo katika wilaya ya Karagwe kutokana na jinsi alivyoiteka wilaya hiyo tangia awasili ambapo kila anapoonekana maelfu ya watu hujipanga na kutamani walau kumshika mkono kama ishara ya kumtakia kila la kheri na kumuunga mkono.
Wachunguzi wa siasa za Karagwe wanasema mikutano ya CDM jimboni humo imevunja rekodi na kwa hakika CCM wilaya imepata hofu kubwa.Katika miji ya Kayanga na Karagwe ilipofanyika mikutano ya CDM wananchi walisimamisha shughuli zote na kuungana na makamanda wa CDM.
Source:Tanzania Daima
Akihutubia maelfu kwa maelfu ya wananchi wa Karagwe jana Dr Slaa anayetambulika kama Rais wa mioyo ya watu alisema kwa sasa CDM imekuja na mkakati mpya ambao ni kuwahamasisha wananchi maeneo ya vijijini na kuepuka kasumba ya kufanya mikutano mijini tu.Amesema ataliongoza jeshi la CDM kujichimbia vijijini ili kazi ya kuizika CCM 2015 iwe nyepesi kabisa.
Katika mkutano huo wanachama 324 walijitoa CCM na kujiunga na CDM.Pia CDM ilitoa kadi kwa wanachama wapya 1836.
Kwa takriban siku tatu sasa Dr Slaa amekuwa gumzo katika wilaya ya Karagwe kutokana na jinsi alivyoiteka wilaya hiyo tangia awasili ambapo kila anapoonekana maelfu ya watu hujipanga na kutamani walau kumshika mkono kama ishara ya kumtakia kila la kheri na kumuunga mkono.
Wachunguzi wa siasa za Karagwe wanasema mikutano ya CDM jimboni humo imevunja rekodi na kwa hakika CCM wilaya imepata hofu kubwa.Katika miji ya Kayanga na Karagwe ilipofanyika mikutano ya CDM wananchi walisimamisha shughuli zote na kuungana na makamanda wa CDM.
Source:Tanzania Daima