CCM ni chama SIASA

kilulu

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
282
57
Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama cha siasa kama vilivyo vyama vingine kama CHADEMA ,CUF , NCCR n.k, CCM wamekuwa wakibeza sana muungano wa hivi vyama 3 vilivyoungana, swali ni je, wao hawawezi kuungana na ACT, TLP kuunda nguvu ya umoja wao?

Kwa kuwa ni chama kinachoshika dola hakiwezi kuwa na umoja wao na ACT na TLP? ama CCM wameishiwa sera ndo maana wanaibeza UKAWA?

Nawasilisha.
 
ngumu kumeza!!

Umoja wa Kutetea Serikali Mbili - UKUSEMBI.

Umoja huu unaundwa na vyama vya CCM, ACT, TLP na UPD.
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama cha siasa kama vilivyo vyama vingine kama CHADEMA ,CUF , NCCR n.k, CCM wamekuwa wakibeza sana muungano wa hivi vyama 3 vilivyoungana, swali ni je, wao hawawezi kuungana na ACT, TLP kuunda nguvu ya umoja wao?

Kwa kuwa ni chama kinachoshika dola hakiwezi kuwa na umoja wao na ACT na TLP? ama CCM wameishiwa sera ndo maana wanaibeza UKAWA?

Nawasilisha.
CCM tumeshaungana na CUF kule Zanzibar
 
Wapi? Kama ni Tanzania CCM bado inakubalika sana.

Sidhani hata wewe kama unaamini hayo maneno. Ukweli ni kwamba kama CCM ingekuwa inakubalika hivyo unavyotaka watu waamini, wala msingekuwa mnahangaika kubeba watu na malori kuhudhuria mikutano. Wala msingekuwa mnaiba kura, ya nini kuiba, si mnapendwa? Subirini wawapigie! Na wala kusingekuwa na haja ya kulazimisha ushindi kwa kutumia Tume ya uchaguzi, polisi, jeshi na Usalama. We unaonaje? Mi naona hata wewe unaona na unajua ni kiasi gani hampendwi.

Kama mnakubalika, acheni kulazimisha watoto wa shule na wafanyakazi wa serikali kwenda kwenye mikutano yenu na msipeleke malori muone ni watu wangapi wanakuja mikutanoni. Na kama kweli mnapendwa na kukubalika, jileteni kwetu kama CCM, acheni kuiba kura wala kubebwa na polisi. Acheni kupiga watu mabomu na risasi halafu muone mnapata kura ngapi! nakuhakikishia kupata kura 5000 kwa nchi nzima itakuwa shida!
 
ccm siipendi sitakujakuipenda kabisa, na wakija na jezi zao ofisini huwa naondoka naenda kunywa chai
 
ngumu kumeza!!

Umoja wa Kutetea Serikali Mbili - UKUSEMBI.

Umoja huu unaundwa na vyama vya CCM, ACT, TLP na UPD.
Taja vyote mbona vingine umeacha kifupi ni kwamba vyama vyote vilivyosajiliwa vinataka serikali mbili ukiacha nccr,cuf na kadima ndiyo wanataka serikali tatu.
 
Sidhani hata wewe kama unaamini hayo maneno. Ukweli ni kwamba kama CCM ingekuwa inakubalika hivyo unavyotaka watu waamini, wala msingekuwa mnahangaika kubeba watu na malori kuhudhuria mikutano. Wala msingekuwa mnaiba kura, ya nini kuiba, si mnapendwa? Subirini wawapigie! Na wala kusingekuwa na haja ya kulazimisha ushindi kwa kutumia Tume ya uchaguzi, polisi, jeshi na Usalama. We unaonaje? Mi naona hata wewe unaona na unajua ni kiasi gani hampendwi.

Kama mnakubalika, acheni kulazimisha watoto wa shule na wafanyakazi wa serikali kwenda kwenye mikutano yenu na msipeleke malori muone ni watu wangapi wanakuja mikutanoni. Na kama kweli mnapendwa na kukubalika, jileteni kwetu kama CCM, acheni kuiba kura wala kubebwa na polisi. Acheni kupiga watu mabomu na risasi halafu muone mnapata kura ngapi! nakuhakikishia kupata kura 5000 kwa nchi nzima itakuwa shida!
Haya maneno yatakutokeeni puani na rafiki zako kaaeni chonjo ccm hii ya kinana mtajuta kuijua watanzania wengi wenye akili wanaiamini sana ccm wewe unaropoka tu.
 
Haya maneno yatakutokeeni puani na rafiki zako kaaeni chonjo ccm hii ya kinana mtajuta kuijua watanzania wengi wenye akili wanaiamini sana ccm wewe unaropoka tu.

Data na ushahidi vingeleta uzito wa hoja yako. Maneno peke yake hapana....bado
 
Haya maneno yatakutokeeni puani na rafiki zako kaaeni chonjo ccm hii ya kinana mtajuta kuijua watanzania wengi wenye akili wanaiamini sana ccm wewe unaropoka tu.

ndugu kivipi tena watajuta au unataka kutuamisha nakudhihirisha kuwa CCM ni chama cha Kigaidi, kikosolewa kinaanza kuhenyesha raia wake walokiweka madarakani.kama ndo hivyo CCM kinakosa mvuto. Raia watakihama si mda mrefu,swali langu ni je, nivibaya kwa CCM kuungana na vyama vingine vya kisiasa wakawa na
muungano wao kama UKAWA?
 
Taja vyote mbona vingine umeacha kifupi ni kwamba vyama vyote vilivyosajiliwa vinataka serikali mbili ukiacha nccr,cuf na kadima ndiyo wanataka serikali tatu.

Vyama hivyo vinawakilisha asilimia ngapi ya wananchi maana serikali 3 ni maoni ya wananchi na sio vyama vya siasa
 
Ofisi yenyewe mnauza bangi na unga mda wote mko juujuu kuhofia kukamatwa.

Mkuu usitoke nje ya mada kanusha hoja kuwa hamtembezi jezi maofisini ikiwezekana weka na ushahidi ili jamaa aumbuke kukimbilia kashfa ni picha ya upeo mdogo wa kulinda hoja
 
Back
Top Bottom