CCM ni Chama Mkombozi au Chama Adui kwa Watanzania?

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,219
40,456
Ili jamii yoyote iweze kupata maendeleo ni lazima iwekeze kiasi kikubwa kuliko inavyotumia. Serikali ya CCM kwa muda mrefu imekuwa ni ya kutumia siyo kuzalisha. JK alikwishawahi kutamka kuwa, 'sisi ni maskini na huko nje kuna pesa nyingi tu, unachotakiwa ni kueleza matatizo yako, wakikuelewa wanakupa pesa'. JK anachojua ni kutumia, wazalishaji wapo nje ya Tanzania. Kwa sasa kila mtanzania ni vema akajua kuwa tupo katika vita, vita ya kuondoa mfumo wa utawala wa ulaji.

Ili ushinde vita yoyote ile ni lazima uwe na makamanda imara, makamanda wenye upeo, makamanda wenye ujasiri, makamanda wenye falsafa moja na wapiganaji wao, makamanda wenye akili na utashi, makamanda watakaowaunganisha wapiganaji wote wawafuate nyuma yao wakiwaongoza kwenye vita vya ushindi. Vita yetu kubwa kwa sasa ni kubadilisha mfumo wa utawala 'ulaji' ili tupate mfumo wa utawala wa 'uzalishaji' LAKINI tunatumia makamanda wanaoamini falsafa ya 'ulaji', hapa hatuwezi kushinda kwa sababu adui yetu namba moja ni makamanda wanaotuongoza. Ndiyo maana nasema adui yetu mkubwa wa maendeleo ni CCM na taasisi zake ambazo zimejengwa katika falsafa ya 'ulaji', hatua yetu ya kwanza kuelekea kwenye maendeleo ni kuiondoa CCM katika uongozi, bila ya hilo kutokea jitihada zetu zote haziwezi kuleta mafanikio makubwa. Japo uchaguzi umekwisha lakini kwa wanaoitakia mema Tanzania ni lazima wahakikishe kila dakika inayopita kuna jitihada za kuhakikisha CCM ipo katika njia ya kutoka katika mamlaka ya kuwatawala watanzania.
 
Kuna maneno mengine yanaudhi sana na kutudhalilisha watanzania,yaani na utajiri wa rasilimali zote hizi tulizonazo halafu mjinga mmoja anatufanya omba omba.Hivi kweli ndio kazi ya raisi hiyo?
 
CCM sio tu inahubiri sera za ulaji na utegemezi, bali pia imeonesha na kujidhihirisha ni chama kisichojihoji wala kuwa na nia ya kujikosoa. Hakina utamaduni wa kusikiliza na mostly importantly, ni mkusanyiko wa watu wanaounganishwa na maslahi na sio dira wala maono.
 
Hili ndio Tatizo lakuwa na kiongozi anayependa kwenda kuombaomba kiongozi asitaka kuumiza kichwa na kufikiria. Kikwete sio kiongozi mpiga kazi. Na tukiachia hivi hili Taifa letu litadhidi kuwa maskini kutokana na kutokuwa na viongozi makini na wenye upendo wa taifa letu
 
Hili ndio Tatizo lakuwa na kiongozi anayependa kwenda kuombaomba kiongozi asitaka kuumiza kichwa na kufikiria. Kikwete sio kiongozi mpiga kazi. Na tukiachia hivi hili Taifa letu litadhidi kuwa maskini kutokana na kutokuwa na viongozi makini na wenye upendo wa taifa letu

CCM imeikataa kwa vitendo siasa ya Ujamaa japo hawataki hilo liondolewe kwenye katiba. Hawa hawa wanaoongoza CCM leo walikuwa wanaimba wimbo sio tu wa Ujamaa, bali pia na KUJITEGEMEA!!!! Whatever happened to the latter policy. Nashangaa, JK kuwaambia WaTZ kama hakwenda nje, wangekufa njaa!!!!

Kama Ujamaa umepitwa na wakati, KUJITEGEMEA je? na hiyo tumeshindwa ama waliokuwa wanaiimba hawakuielewa? Kweli nakubali, WaTZ tuna kumbukumbu finyu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom