Paul Makonda
Member
- Jul 8, 2011
- 97
- 186
Leo asubuhi nilipokuwa katika kipindi cha Tuongee Asubuhi kinachorushwa katika kituo maarufu cha televisheni cha Star TV ya jijini Mwanza kwenye mada iliyokuwa inahusu uwajibikaji. Nilizungumza juu ya maana halisi na upana wa dhana ya uwajibikaji. Nikaugawa katika maeneo tofauti, kwa mwananchi, kwa chama na kwa serikali. Na Kwamba uwajibika unatokana na wajibu umpasao mtu kuutekeleza na akishindwa kuutekeleza wajibu huo dhana hii inamtaka kujitathimini na kukiri kuwa hana uwezo na ameshindwa kuutekeleza hivyo anawajibika kwa kujiuzulu ama kwa namna nyingine.
Lakini mmoja wa wachangiaji Ndugu Marcus Albano mwanaharakati na mkereketwa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alikishutumu Chama changu, chama makini, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa hakiwajibishi wanachama wake na viongozi wake pale wanapothibitika kuwa wamekosea na wameshindwa kuutekeleza wajibu husika.
Shutuma hii ilinipasa niijibu, na niliijibu kwa sababu na namna mbili:
i) Moja si kweli kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwajibishi wanachama ama viongozi wake, hivyo shutuma hiyo sio ya kweli.
ii) Pili ni wazi kuwa mwanaharakati huyo na mwanachama wa Chadema hafahamu historia ya Chama Cha Mapinduzi, kwa maana hajui kabisa kuwa hata dhana yenyewe ya uwajibikaji imeasisiwa na Mwalimu Nyerere ambae ni muasisi wa CCM na kuiwekea CCM misingi ya uwajibikaji kwa maandiko na mfumo.
Nikaona kulisema hili kwenye TV pekee haitoshi bali nililete hapa ili kama kuna yeyote mwenye ku-challenge hilo ajitokeze, CCM imewahi katika historia yake kumuwajibisha MAKAMU MWENYEKITI wa chama ambae pia alikuwa ni RAIS wa NCHI na chama hakikutingishika wala kupata mpasuko wa aina yeyote, lakini utaratibu huo umeendelea siku zote na hata hivi karibuni kimemvua uanachama mmoja wa makada wake wakubwa walioshika nyadhifa kubwa katika Chama na Serikali kule Zanzibar Ndugu Mansoor.
TOFAUTI iliyopo baina yetu na vyama vingine ni kwamba CCM tunafuata na kuisimamia dhana hii ya UWAJIBIKAJI kwa maslahi mapana ya Chama na Serikali kwa maana ya UTAIFA na wenzetu wa vyama vingine wanajaribu kulifanya hili kwa maslahi ya mtu, ama kikundi cha watu na kwa sababu za madaraka, woga na ubaguzi.
Naomba kuwasilisha.
Lakini mmoja wa wachangiaji Ndugu Marcus Albano mwanaharakati na mkereketwa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alikishutumu Chama changu, chama makini, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa hakiwajibishi wanachama wake na viongozi wake pale wanapothibitika kuwa wamekosea na wameshindwa kuutekeleza wajibu husika.
Shutuma hii ilinipasa niijibu, na niliijibu kwa sababu na namna mbili:
i) Moja si kweli kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwajibishi wanachama ama viongozi wake, hivyo shutuma hiyo sio ya kweli.
ii) Pili ni wazi kuwa mwanaharakati huyo na mwanachama wa Chadema hafahamu historia ya Chama Cha Mapinduzi, kwa maana hajui kabisa kuwa hata dhana yenyewe ya uwajibikaji imeasisiwa na Mwalimu Nyerere ambae ni muasisi wa CCM na kuiwekea CCM misingi ya uwajibikaji kwa maandiko na mfumo.
Nikaona kulisema hili kwenye TV pekee haitoshi bali nililete hapa ili kama kuna yeyote mwenye ku-challenge hilo ajitokeze, CCM imewahi katika historia yake kumuwajibisha MAKAMU MWENYEKITI wa chama ambae pia alikuwa ni RAIS wa NCHI na chama hakikutingishika wala kupata mpasuko wa aina yeyote, lakini utaratibu huo umeendelea siku zote na hata hivi karibuni kimemvua uanachama mmoja wa makada wake wakubwa walioshika nyadhifa kubwa katika Chama na Serikali kule Zanzibar Ndugu Mansoor.
TOFAUTI iliyopo baina yetu na vyama vingine ni kwamba CCM tunafuata na kuisimamia dhana hii ya UWAJIBIKAJI kwa maslahi mapana ya Chama na Serikali kwa maana ya UTAIFA na wenzetu wa vyama vingine wanajaribu kulifanya hili kwa maslahi ya mtu, ama kikundi cha watu na kwa sababu za madaraka, woga na ubaguzi.
Naomba kuwasilisha.