Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,502
- 4,408
Waswahili wanasema wasiwasi ndio akili. Leo nami nina wasiwasi mkubwa juu ya Chama changu. Naamini CCM ni chama kikubwa sana naweza kukifananisha na mbuyu, unaweza usikatwe na shoka lakini ikipatikana zana nzuri unakatwa.
Nyakati za sasa wanaCCM wanaamini katika ukubwa wa chama kuliko uwezo wa ushawishi. Unakuta mtu anasema nitajiunga CCM ili nishinde kirahisi kwa sababu CCM itanibeba, hawa ni maslahi na ni aibu kwa mustakabali wa CCM.
Ifike mahali ili MTU aweze kugombea uongozi iwe ndani ya CCM au kupitia CCM awe amepitia mafunzo fulani yanayotolewa na chama hii itasaidia chama kutengeneza viongozi imara.
Mustkali wa Chama upo mikononi mwa Mwenyekiti wetu Ndg.Samia, ninakusihi na kukuomba ufanye mabadiliko kwenye uongozi wa Chama hususani kwa nafasi ya Ukatibu mkuu na katibu mwenezi.
Nafasi hizo zinahitaji wenye ushawishi kama Mzee Mangula au Comred Kinana, watu kwenye uwezo mkubwa wa kisiasa. Kwa kipindi cha mwaka sasa naona kuwa ombwe kubwa kwenye nafasi hizo.
Viongozi wenye ushawishi ni chachu ya kujenga CCM imara licha ya sasa inaweza isionekane kwa sababu ya ukubwa wa CCM lakini kwa baadae ni muhimu. Viongozi wenye ushawishi wanasaidia kujenga taasisi yenye ushawishi na nguvu ya ushawishi.
Nyakati za sasa wanaCCM wanaamini katika ukubwa wa chama kuliko uwezo wa ushawishi. Unakuta mtu anasema nitajiunga CCM ili nishinde kirahisi kwa sababu CCM itanibeba, hawa ni maslahi na ni aibu kwa mustakabali wa CCM.
Ifike mahali ili MTU aweze kugombea uongozi iwe ndani ya CCM au kupitia CCM awe amepitia mafunzo fulani yanayotolewa na chama hii itasaidia chama kutengeneza viongozi imara.
Mustkali wa Chama upo mikononi mwa Mwenyekiti wetu Ndg.Samia, ninakusihi na kukuomba ufanye mabadiliko kwenye uongozi wa Chama hususani kwa nafasi ya Ukatibu mkuu na katibu mwenezi.
Nafasi hizo zinahitaji wenye ushawishi kama Mzee Mangula au Comred Kinana, watu kwenye uwezo mkubwa wa kisiasa. Kwa kipindi cha mwaka sasa naona kuwa ombwe kubwa kwenye nafasi hizo.
Viongozi wenye ushawishi ni chachu ya kujenga CCM imara licha ya sasa inaweza isionekane kwa sababu ya ukubwa wa CCM lakini kwa baadae ni muhimu. Viongozi wenye ushawishi wanasaidia kujenga taasisi yenye ushawishi na nguvu ya ushawishi.