OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 428
CCM Kutoka madarakani iwe wamependa tu, kila kitu mfumo wote ni wao iweje washindwe? hao wapinzani wameweka matumaini makubwa sana kwa Lowasa kwamba atawasaidia kuchukua nchi lakini wamesahau kwamba tunaongozwa na Katiba ya 1977 baada ya kipigo watageuka kulalamika hakutakua na wa kuwasikiliza.
Hilo moja pia kuna Ushindi wa moja kwa moja ambao CCM wanaweza kupata, kuna watu wengi hawaungi mkono Lowasa kujiunga na CDM swali Iao ni kwamba zile harakati zakuijenga CDM kwa msaada wa Ruzuku ktk vichwa vyao haukutosha mpaka viongozi wanakodi Majeshi tena kwa kumuangukia Lowasa? Uhodari wa michango na Mafisi/kashfa ktk JF ni tofauti na hali halisi.
Dr Slaa alikua chaguo Zuri kwa CDM lakini maamuzi ya dakika za mwisho yanaweza kuididimiza, Risk ina faida kubwa na hasara kubwa tusubiri.
Kenya, Nigeria, Zambia, Malawi ilikuwaje?, hizi ni akili finyu na kukosa maarifa.... Vijana safari hii wanafanya uamuzi mgumu