Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Tuliambiwa na TANU. ili tuendelee tunahitaji vitu vinne, Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora.
Tukaimba wimbo wa Azimio la Arusha, Azimio la Musoma, madaraka mikoani, vijiji vya ujamaa na zaidi, tukasema kuwa mkoloni, bepari na kaburu ndio maadui wa maendeleo yetu ukiongezea Umasikini, Ujinga na Maradhi.
Leo hii nawatamkieni wazi, ikiwa ni mahubiri yangu ya Jumapili ya Oktoba 19 ya mwaka 2008, kuwa Adui mkubwa wa maendeleo ya Taifa la Tanzania na ustawi wa Maisha ya Watanzania ni Chama Cha Mapinduzi, maarufu kama CCM.
Pamoja na mazuri ya kale yaliyofanywa na TANU hata CCM, lakini ukweli usiopingika kuwa CCM hii si ile mliyokuwa mnaiamini na iliyowaletea Uhuru au Mapinduzi ya kizalendo.
CCM si Chama cha Mapinduzi, bali ni Chama cha Ubabaishaji. Iwe ni uzembe, uvivu, uzururaji, uhujumu, uongozi mbovu, ufisadi, kutokuwajibika au lolote lile ambalo ni kizingiti cha maendeleo ya kweli katika Taifa na Jamii.
CCM ya leo imejenga ubaguzi wa mawazo, imedumaza maendeleo ya Wananchi, inakumbatia hujuma na ufisadi, haina dira au mwelekeo wa kujenga Taifa na Uchumi wake, haina uongozi bora wala siasa safi.
CCM ya leo inatumia vitisho na mabavu kuongoza Taifa na imefikia hatua inalihujumu Taifa ili iendelee kuongoza na kutawala!
CCM ya Kikwete, Msekwa na Makamba zimeishia kuwa Chama cha Wababaishaji, wasio na nidhamu, utu wala aibu. Hakimjali tena yule mkulima au mfanyakazi, bali yamtukuza yule mwenye pesa.
Watu na Ardhi, wapo, Siasa safi ilikuwepo, na hata Uongozi Bora. Lakini watu wameendelea kuwa wanyonge, dhaifu na masikini wa kutupa, ardhi imepoteza rutuba na thamani na kila kitu kinasukumizwa kwa mgeni aliye na fedha akinunue ili Taifa lipate vijisenti vya kujinusuru.
Kwenye Siasa safi na Uongozi bora, huko ndiko kumeoza kabisa! Kwa kipindi cha miaka 13 iliyopita, CCM imepoteza uwezo wa uongozi, imepoteza viongozi safi na wenye uzalendo, imepoteza uwezo wa kuwa na siasa za kujenga Taifa na kupigana vita dhidi ya Umasikini, Maradhi na Ujinga.
Ni kweli takwimu za Kizungu za kiuchumi na maesabu zinaonyesha uchumi ukikua, lakini ni tarakimu kwenye majedwali, na si hali halisi ya Mtanzania kuwa na uhai na tumaini la kuwa na kesho kutwa au mwezi ujao bila kuwa na hofu.
Ikiwa tuliambiwa mapema mwaka huu kuwa asilimia 52 (52%) ya Watanzania wanacheza makidamakida au Umbali Sufuri (Zero Distance)kutoka umasikini, huku wakiwa hawajui leo wataishi vipi, iweje tujitape kuwa uchumi na pato la Taifa limeongezeka?
Ikiwa tunaambiwa 31% ya watu wazima ambao ni miaka 18 na zaidi ni wajinga hawajui kusoma na kuandika, tutasemaje kuwa tunapiga hatua za maendeleo?
Ni maendeleo gani ya kurudi kinyumenyume? NI maendeleo gani ya kutumia na kutumbua bila kuzalisha na kuongeza kipato? Uwiano wa Matumizi na Mapato ni karibu matumizi mara tatu ya mapato!
Sasa tumeingia mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, lakini inabidi tuache woga na kuachana na ile methali ya zimwi likujujalo na tuachane na CCM.
Kauli za Ari, Nguvu na Kasi mpya ni kejeli tupu. Hotuba za Maisha Bora kwa kila Mtanzania ni ujuha na tusi la nguoni!
Nawaasa Watanzania wenzangu, achaneni na CCM, CCM si chama makini tena na hakijali maslahi yenu wala uhai wenu. Thamani yenu kwa CCM ni nyakati za uchaguzi kama tulivyoona huko Tarime majuzi au kule Kiteto!
Ni heri tuwachague CUF, Chadema, TLP, NCCR, UDP au wengine wote nao wajaribu kutuongoza maana umahiri wa CCM tunaohubiriwa kila siku ni uozo mtupu.
Mtanzania mpaka leo anasota kwenda tafuta kuni na maji, kulima kwa kujihemea, hana shule, dawati, daftari, dawa, mshahara mdogo huku gharama za maisha zikipanda na mbaya zaidi, hakuna hata mtu mmoja ambaye anauwezo ndani ya CCM kusema tunahitaji full stop ya ubabaishaji na kuanza kutumikia Watanzania.
Badala yake sababu nyingi zinatolewa kila siku kuhalalisha udhaifu wa Serikali na CCM. mara leo bei za mafuta, kesho jua kali na kiangazi au la sivyo tutaambiwa kuangamia kwa uchumi wa nchi tajiri zilizoendela ni sababu Tanzania inashindwa kupiga hatua za maendeleo.
Iweje Rwanda, Burundi na hata Congo wanaanza kutupita huku sisi tukishabikia Amani, Utulivu, Mshikamano na Umoja lakini ni masikini wa kutupa?
Najua wengi wenu mtadai kuwa CCM kuna wanamapinduzi kina Mwakyembe, Seleli, Kilango na wachache kadhaa ambao eti ni mabingwa wa Wananchi. Lakini watakuwaje mabingwa wa Wananchi ikiwa wao ni wafungwa wa kisiasa ndani ya Chama chao pamoja na kufurukuta kwao?
Tutasemaje eti tuwape CCM miaka mitano mingine ya majaribio huku majaribio ya mwisho yametupa Kiongozi Mkuu ambaye hana hata nguvu ya kuhamasisha umma na kila siku kuishia kulalamika kama Wananchi wanavyolalamika?
Hivi kina Mkukuta, Ilani ya 2005 na visheni 2025 zina maana gani ikiwa anayefaidika ni James Sinclair, Jeetu Patel, Yusuf Manji, Rostam Azizi, Andrew Chenge, Benjamin Mkapa, Daniel Yona, Edward Lowassa, Gray Mgonja, Karmali Juma, Barrick Gold, Rites Corp, IPTL, Richmond na wenginewe katika kikundi hiki kidogo kinachomiliki na kutumbua maslahi ya Taifa na si mkulima, mvuvi, mfanyakazi, mwalimu, mwanafunzi, mzee, kijana na mtoto wa kawaida?
Kuna umuhimu gani kuendela kusema tunaimani na CCM ikiwa CCM haioni umuhimu na umaana wa kuliongoza Taifa kutoka Umasikini, Ujinga na Maradhi?
Ikiwa Nyerere alitishia kujitoa CCM na kusema CCM si Mama yake, iweje sisi tuendelee kuamini kuwa CCM ni Mama na Baba, Alpha na Omega wa kutuletea maendeleo Tanzania?
Sana sana walichokifanya CCM kwa bidii ni kuturudisha nyuma kimaendeleo kwa kukimbilia kuua mihimili ya Uchumi wa Taifa kwa kuiuza ama kwa bei poa au dezo kwa wawekezaji na wao wenyewe.
Mipango ya maendeleo ambayo tuliimba na kuifanya kuwa ndiyo nguzo kuu ya kujitegemea kama Taifa hasa katika nyanja za kilimo, ufugaji, uvuvi na hata ajira, CCM imezitelekeza kwa jina la kujivua majukumu ya Serikali inayofanyia kazi watu kwa kisingizio cha Utandawazi na Soko Huria.
Badala ya kurekebisha makosa na matatizo ya awali yaliyotufikisha hapa tulipo kiuchumi ili kuimarisha Taifa letu na ustawi wetu kama jamii, CCM kupitia Serikali yake imeendelea kuturudisha nyuma kimaendeleo kwa kampeni yake maalum ya kutoa kipaumbele cha kuvuna mali ghafi na rasilimali za Taifa kwa Wawekezaji wanaotuhujumu na kugawanyana wao kwa wao umiliki wa mali na mifumo ya Uchumi wa nchi yetu.
Sasa hivi Tanzania nzima kuna woga wa kutisha wa kutokujua kama kesho itafika kukiwa na chakula mezani au dawa za kutosha. Mgawanyiko wa wale wenye mali na wasio na mali ambau hujenga tabaka la masikini na matajiri ni kubwa mno na asilimia kubwa ya Watanzania wanaegemea kwenye Umasikini uliokubuhu.
Tanzania ya leo, pamoja na kuhamia katika mfumo endelevu wa soko huria, bado haijaweza kujitosheleza hata kwa chakula! Kwa mujibu wa ripoti ya kiuchumi ya Serikali na Benki Kuu iliyotoka mwezi uliopita ambayo inaonyesha ukubwa wa madeni ya Taifa, mapato na matumizi ikiwa ni pamoja na uagizaji, inaonyesha ongezeko kubwa la kuagiza chakula, huku nchi ikiwa imebarikiwa na neema ya ardhi ya kutosha yenye rutuba, vyanzo vingi vya maji na watu wa kutosha kuzalisha chakula.
Badala ya kuja na sera na mipango endelevu kuimarisha uchumi na kusu(Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi) gurudumu la maendeleo kwenda mbele, CCM imekimbilia kutafuta njia fupi na gharama nyepesi kujipatia kipato na kutamba kuwa pato la Taifa linaongezeka.
Ongezeko la uuzaji holela wa mashirika, viwanda, ardhi na vitega uchumi vya Taifa likiandamana na rushwa na uhujumu vimeongezeka.
Badala ya kuongeza ufanisi na gharama ya ubunifu, juhudi na maarifa ili kuinua vipato, CCM imeegemea kubobea katika Rushwa na Takrima na imefanya makusudi makubwa kabisa kuhakikisha kuwa Rushwa na Takrima zinakuwa sehemu halali za maisha ya Mtanzania. Mfano hai ni chaguzi za Serikali za Wabunge na Urais mwaka 2005 na chaguzi ndogo zilizofuatia ambapo CCM ilitumia fedha nyingi kutoa hongo ili ipate kura.
Hata pale penye ushahidi tosha wa Uhujumu wa Taifa iwe ni Ufisadi au kuzorota kwa mahusiano ya Tanganyika na Unguja, bado CCM imeendelea kupuuzia kilio cha Mtanzania na kutuhumu wale wanaopingana nayo kuwa ni wasaliti na si wazalendo au waleta maendeleo.
CCM inajitapa kwa wananchi kuwa yenyewe ina dola na ndiyo iliyo madarakani, lakini inashindwa kumpa Mtanzania uhuru wa kujitegemea kiuchumi. Inashangaza kuwa mpaka leo kuna baadhi ya Watendaji na Viongozi wa CCM ambao wanapita vijijini na mijini wakijitapa kuwa wao ni Dola na wana nguvu. Ni nguvu gani ikiwa raia wako wanateseka?
Kitendo cha Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na Mwenyekiti wa Chama Tawala CCM Bwana Jakaya Kikwete kuzomewa hata kutupiwa mawe ni ishara rasmi kuwa nchi iko njia panda na Watanzania wamechoshwa na mbiu ya mgambo kuisifia CCM kila siku kuwa ni bora kuliko wengine.
Kututisha kuwa eti akija Maalim, Lipumba, Mbowe, Mrema au Cheyo kuwa Taifa litaingia katika vita na vurugu na umwagaji damu mithili ya Zimbabwe na Kenya ni uongo mkubwa!
Yaliyotokea Zimbabwe na Kenya ni yale yale ambayo CCM imeyafanya, kumpuuzia mwananchi wake aendelee kusota huku wao CCM wakibadilishana safari za kwenda kutumbua ndani na nje ya nchi.
Natoa wito huu kwako ndugu Mtanzania kuwa adui wa maendeleo yako ambaye amekomaza Umasikini, Ujinga na Maradhi si mkoloni, bepari, beberu au kaburu tena, bali ni CCM.
Waswahili wanasema kikulacho ki nguoni mwako, jihadharini na CCM!
Tukaimba wimbo wa Azimio la Arusha, Azimio la Musoma, madaraka mikoani, vijiji vya ujamaa na zaidi, tukasema kuwa mkoloni, bepari na kaburu ndio maadui wa maendeleo yetu ukiongezea Umasikini, Ujinga na Maradhi.
Leo hii nawatamkieni wazi, ikiwa ni mahubiri yangu ya Jumapili ya Oktoba 19 ya mwaka 2008, kuwa Adui mkubwa wa maendeleo ya Taifa la Tanzania na ustawi wa Maisha ya Watanzania ni Chama Cha Mapinduzi, maarufu kama CCM.
Pamoja na mazuri ya kale yaliyofanywa na TANU hata CCM, lakini ukweli usiopingika kuwa CCM hii si ile mliyokuwa mnaiamini na iliyowaletea Uhuru au Mapinduzi ya kizalendo.
CCM si Chama cha Mapinduzi, bali ni Chama cha Ubabaishaji. Iwe ni uzembe, uvivu, uzururaji, uhujumu, uongozi mbovu, ufisadi, kutokuwajibika au lolote lile ambalo ni kizingiti cha maendeleo ya kweli katika Taifa na Jamii.
CCM ya leo imejenga ubaguzi wa mawazo, imedumaza maendeleo ya Wananchi, inakumbatia hujuma na ufisadi, haina dira au mwelekeo wa kujenga Taifa na Uchumi wake, haina uongozi bora wala siasa safi.
CCM ya leo inatumia vitisho na mabavu kuongoza Taifa na imefikia hatua inalihujumu Taifa ili iendelee kuongoza na kutawala!
CCM ya Kikwete, Msekwa na Makamba zimeishia kuwa Chama cha Wababaishaji, wasio na nidhamu, utu wala aibu. Hakimjali tena yule mkulima au mfanyakazi, bali yamtukuza yule mwenye pesa.
Watu na Ardhi, wapo, Siasa safi ilikuwepo, na hata Uongozi Bora. Lakini watu wameendelea kuwa wanyonge, dhaifu na masikini wa kutupa, ardhi imepoteza rutuba na thamani na kila kitu kinasukumizwa kwa mgeni aliye na fedha akinunue ili Taifa lipate vijisenti vya kujinusuru.
Kwenye Siasa safi na Uongozi bora, huko ndiko kumeoza kabisa! Kwa kipindi cha miaka 13 iliyopita, CCM imepoteza uwezo wa uongozi, imepoteza viongozi safi na wenye uzalendo, imepoteza uwezo wa kuwa na siasa za kujenga Taifa na kupigana vita dhidi ya Umasikini, Maradhi na Ujinga.
Ni kweli takwimu za Kizungu za kiuchumi na maesabu zinaonyesha uchumi ukikua, lakini ni tarakimu kwenye majedwali, na si hali halisi ya Mtanzania kuwa na uhai na tumaini la kuwa na kesho kutwa au mwezi ujao bila kuwa na hofu.
Ikiwa tuliambiwa mapema mwaka huu kuwa asilimia 52 (52%) ya Watanzania wanacheza makidamakida au Umbali Sufuri (Zero Distance)kutoka umasikini, huku wakiwa hawajui leo wataishi vipi, iweje tujitape kuwa uchumi na pato la Taifa limeongezeka?
Ikiwa tunaambiwa 31% ya watu wazima ambao ni miaka 18 na zaidi ni wajinga hawajui kusoma na kuandika, tutasemaje kuwa tunapiga hatua za maendeleo?
Ni maendeleo gani ya kurudi kinyumenyume? NI maendeleo gani ya kutumia na kutumbua bila kuzalisha na kuongeza kipato? Uwiano wa Matumizi na Mapato ni karibu matumizi mara tatu ya mapato!
Sasa tumeingia mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, lakini inabidi tuache woga na kuachana na ile methali ya zimwi likujujalo na tuachane na CCM.
Kauli za Ari, Nguvu na Kasi mpya ni kejeli tupu. Hotuba za Maisha Bora kwa kila Mtanzania ni ujuha na tusi la nguoni!
Nawaasa Watanzania wenzangu, achaneni na CCM, CCM si chama makini tena na hakijali maslahi yenu wala uhai wenu. Thamani yenu kwa CCM ni nyakati za uchaguzi kama tulivyoona huko Tarime majuzi au kule Kiteto!
Ni heri tuwachague CUF, Chadema, TLP, NCCR, UDP au wengine wote nao wajaribu kutuongoza maana umahiri wa CCM tunaohubiriwa kila siku ni uozo mtupu.
Mtanzania mpaka leo anasota kwenda tafuta kuni na maji, kulima kwa kujihemea, hana shule, dawati, daftari, dawa, mshahara mdogo huku gharama za maisha zikipanda na mbaya zaidi, hakuna hata mtu mmoja ambaye anauwezo ndani ya CCM kusema tunahitaji full stop ya ubabaishaji na kuanza kutumikia Watanzania.
Badala yake sababu nyingi zinatolewa kila siku kuhalalisha udhaifu wa Serikali na CCM. mara leo bei za mafuta, kesho jua kali na kiangazi au la sivyo tutaambiwa kuangamia kwa uchumi wa nchi tajiri zilizoendela ni sababu Tanzania inashindwa kupiga hatua za maendeleo.
Iweje Rwanda, Burundi na hata Congo wanaanza kutupita huku sisi tukishabikia Amani, Utulivu, Mshikamano na Umoja lakini ni masikini wa kutupa?
Najua wengi wenu mtadai kuwa CCM kuna wanamapinduzi kina Mwakyembe, Seleli, Kilango na wachache kadhaa ambao eti ni mabingwa wa Wananchi. Lakini watakuwaje mabingwa wa Wananchi ikiwa wao ni wafungwa wa kisiasa ndani ya Chama chao pamoja na kufurukuta kwao?
Tutasemaje eti tuwape CCM miaka mitano mingine ya majaribio huku majaribio ya mwisho yametupa Kiongozi Mkuu ambaye hana hata nguvu ya kuhamasisha umma na kila siku kuishia kulalamika kama Wananchi wanavyolalamika?
Hivi kina Mkukuta, Ilani ya 2005 na visheni 2025 zina maana gani ikiwa anayefaidika ni James Sinclair, Jeetu Patel, Yusuf Manji, Rostam Azizi, Andrew Chenge, Benjamin Mkapa, Daniel Yona, Edward Lowassa, Gray Mgonja, Karmali Juma, Barrick Gold, Rites Corp, IPTL, Richmond na wenginewe katika kikundi hiki kidogo kinachomiliki na kutumbua maslahi ya Taifa na si mkulima, mvuvi, mfanyakazi, mwalimu, mwanafunzi, mzee, kijana na mtoto wa kawaida?
Kuna umuhimu gani kuendela kusema tunaimani na CCM ikiwa CCM haioni umuhimu na umaana wa kuliongoza Taifa kutoka Umasikini, Ujinga na Maradhi?
Ikiwa Nyerere alitishia kujitoa CCM na kusema CCM si Mama yake, iweje sisi tuendelee kuamini kuwa CCM ni Mama na Baba, Alpha na Omega wa kutuletea maendeleo Tanzania?
Sana sana walichokifanya CCM kwa bidii ni kuturudisha nyuma kimaendeleo kwa kukimbilia kuua mihimili ya Uchumi wa Taifa kwa kuiuza ama kwa bei poa au dezo kwa wawekezaji na wao wenyewe.
Mipango ya maendeleo ambayo tuliimba na kuifanya kuwa ndiyo nguzo kuu ya kujitegemea kama Taifa hasa katika nyanja za kilimo, ufugaji, uvuvi na hata ajira, CCM imezitelekeza kwa jina la kujivua majukumu ya Serikali inayofanyia kazi watu kwa kisingizio cha Utandawazi na Soko Huria.
Badala ya kurekebisha makosa na matatizo ya awali yaliyotufikisha hapa tulipo kiuchumi ili kuimarisha Taifa letu na ustawi wetu kama jamii, CCM kupitia Serikali yake imeendelea kuturudisha nyuma kimaendeleo kwa kampeni yake maalum ya kutoa kipaumbele cha kuvuna mali ghafi na rasilimali za Taifa kwa Wawekezaji wanaotuhujumu na kugawanyana wao kwa wao umiliki wa mali na mifumo ya Uchumi wa nchi yetu.
Sasa hivi Tanzania nzima kuna woga wa kutisha wa kutokujua kama kesho itafika kukiwa na chakula mezani au dawa za kutosha. Mgawanyiko wa wale wenye mali na wasio na mali ambau hujenga tabaka la masikini na matajiri ni kubwa mno na asilimia kubwa ya Watanzania wanaegemea kwenye Umasikini uliokubuhu.
Tanzania ya leo, pamoja na kuhamia katika mfumo endelevu wa soko huria, bado haijaweza kujitosheleza hata kwa chakula! Kwa mujibu wa ripoti ya kiuchumi ya Serikali na Benki Kuu iliyotoka mwezi uliopita ambayo inaonyesha ukubwa wa madeni ya Taifa, mapato na matumizi ikiwa ni pamoja na uagizaji, inaonyesha ongezeko kubwa la kuagiza chakula, huku nchi ikiwa imebarikiwa na neema ya ardhi ya kutosha yenye rutuba, vyanzo vingi vya maji na watu wa kutosha kuzalisha chakula.
Badala ya kuja na sera na mipango endelevu kuimarisha uchumi na kusu(Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi) gurudumu la maendeleo kwenda mbele, CCM imekimbilia kutafuta njia fupi na gharama nyepesi kujipatia kipato na kutamba kuwa pato la Taifa linaongezeka.
Ongezeko la uuzaji holela wa mashirika, viwanda, ardhi na vitega uchumi vya Taifa likiandamana na rushwa na uhujumu vimeongezeka.
Badala ya kuongeza ufanisi na gharama ya ubunifu, juhudi na maarifa ili kuinua vipato, CCM imeegemea kubobea katika Rushwa na Takrima na imefanya makusudi makubwa kabisa kuhakikisha kuwa Rushwa na Takrima zinakuwa sehemu halali za maisha ya Mtanzania. Mfano hai ni chaguzi za Serikali za Wabunge na Urais mwaka 2005 na chaguzi ndogo zilizofuatia ambapo CCM ilitumia fedha nyingi kutoa hongo ili ipate kura.
Hata pale penye ushahidi tosha wa Uhujumu wa Taifa iwe ni Ufisadi au kuzorota kwa mahusiano ya Tanganyika na Unguja, bado CCM imeendelea kupuuzia kilio cha Mtanzania na kutuhumu wale wanaopingana nayo kuwa ni wasaliti na si wazalendo au waleta maendeleo.
CCM inajitapa kwa wananchi kuwa yenyewe ina dola na ndiyo iliyo madarakani, lakini inashindwa kumpa Mtanzania uhuru wa kujitegemea kiuchumi. Inashangaza kuwa mpaka leo kuna baadhi ya Watendaji na Viongozi wa CCM ambao wanapita vijijini na mijini wakijitapa kuwa wao ni Dola na wana nguvu. Ni nguvu gani ikiwa raia wako wanateseka?
Kitendo cha Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na Mwenyekiti wa Chama Tawala CCM Bwana Jakaya Kikwete kuzomewa hata kutupiwa mawe ni ishara rasmi kuwa nchi iko njia panda na Watanzania wamechoshwa na mbiu ya mgambo kuisifia CCM kila siku kuwa ni bora kuliko wengine.
Kututisha kuwa eti akija Maalim, Lipumba, Mbowe, Mrema au Cheyo kuwa Taifa litaingia katika vita na vurugu na umwagaji damu mithili ya Zimbabwe na Kenya ni uongo mkubwa!
Yaliyotokea Zimbabwe na Kenya ni yale yale ambayo CCM imeyafanya, kumpuuzia mwananchi wake aendelee kusota huku wao CCM wakibadilishana safari za kwenda kutumbua ndani na nje ya nchi.
Natoa wito huu kwako ndugu Mtanzania kuwa adui wa maendeleo yako ambaye amekomaza Umasikini, Ujinga na Maradhi si mkoloni, bepari, beberu au kaburu tena, bali ni CCM.
Waswahili wanasema kikulacho ki nguoni mwako, jihadharini na CCM!