CCM: Nafasi ya Makamu Mwenyekiti yageuka gumzo

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
803
CCM: Nafasi ya Makamu Mwenyekiti yageuka gumzo

ZIKIWA zimebakia wiki mbili kufikia uchaguzi Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ngazi ya taifa joto limeanza kupanda kwa baadhi ya makada wanaotajwa kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa.

Kwa mujibu wa taratibu na kanuni za CCM nafasi hiyo haigombewi bali jina la atakayependekezwa na Kamati Kuu kushika wadhifa huo, litajadiliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na baadaye kupelekwa katika Mkutano Mkuu ili lipigiwe kura.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti kwa sasa inashikiliwa na John Malecela ambaye kwa mujibu wa Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete, ana nafasi sawa na makada wengine katika kutetea kiti hicho kufuatia muda wake kumalizika.

Malecela amekalia kiti hicho tangu awamu ya pili iliyokuwa chini ya Ali Hassan Mwinyi, kisha awamu ya tatu chini ya Benjamin Mkapa na sasa awamu ya nne iliyoanza chini ya Kikwete.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanaeleza kuwepo ugumu wa Malecela kubakiza kiti hicho kufuatia wimbi linalohitaji wazee kupumzika, ili kupisha damu changa.

Lakini hali ikiwa hivyo kwa Malecela, mkongwe mwingine kutoka awamu ya kwanza hadi sasa Kingunge Ngombale-Mwiru, naye anatajwa na baadhi ya wanachama wa CCM kuwa anaweza kuteuliwa kushika nafasi hiyo.

Wanaomtaja Kingunge wanaeleza kuwa kiongozi huyo amekuwa karibu na Mwenyekiti wa CCM kwa kipindi kirefu na ndiye pekee anayeweza kuzima harakati za makundi yanayoongozwa na wana CCM wakongwe ili kufanya uongozi wa Kikwete kufanikiwa bila mawimbi.

Jina lingine linalozungumzwa ni la Katibu wa sasa wa CCM, Yusuf Makamba. Makamba anatajwa kuwepo kwenye orodha ya kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti, ikiwa ni mpango wa Mwenyekiti Kikwete kumuengua kiustaarabu kutoka katika nafasi ya utendaji ambayo anaonekana kupwaya.

Katika siku za hivi karibuni Makamba amehusishwa na migogoro mingi katika sehemu mbalimbali anazotembelea, hasa kufuatia tabia yake ya kuwafokea viongozi wa chama hadharani na kuwapigia debe baadhi ya makada anaowataka kushinda nafasi za uongozi.

Katika orodha hiyo, pia limo jina la Spika Mstaafu wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdulrahman Kinana. Kinana anaelezwa kuwa karibu na Kikwete kuanzia wakati wa harakati zake za kuwania urais.

Baadhi ya makada wa CCM wanasema Kinana ni mmoja wa vigogo walio karibu na rais ambaye hajapewa nafasi ya juu ya uongozi katika serikali na chama, huku pia akionekana kutumika katika matukio ya kusuluhisha migogoro kadhaa ndani ya CCM hasa mkoani Mbeya.

Kazi hizo za usuluhishi zinaelezwa kupewa kwake moja kwa moja na Kikwete kama harakati za kumuandaa kwa wadhifa wa Makamu Mwenyekiti.

Kinana pia anaonekana kukubalika na kundi la vijana, ambalo linamtazama kama kiongozi anayeweza kukubaliana na mabadiliko yatakayowawezesha baadhi ya wakongwe kukaa kando na kubakia na kazi ya ushauri.

Pia kunatajwa jina la Edward Lowassa, Waziri Mkuu wa sasa, huyu baadhi ya watu wamekuwa wakimtaja kuwa ana harakati za kuwania urais siku zijazo.

Watu walio karibu na Lowassa ambao walipata fursa ya kuzungumza na gazeti hili, walieleza kusikitishwa kwao kuhusu fikra hizo huku wakifafanua kuwa, Lowassa hana nia ya kusaka nafasi hiyo.

"Kazi aliyonayo katika serikali ni kubwa na inayomtaka kuwajibika kila siku. Hawezi kuwa na nia tena ya kutaka nafasi ya Makamu Mwenyekiti.

"Tena wanaozungumzia suala la yeye kutamani urais wanapoteza muda kwa kuwa muda wa Kikwete utakapomalizika atakuwa na umri zaidi ya miaka 60.

"Yeye alikuwepo katika kundi linalopinga wakongwe kung'ang'ania madaraka sasa iweje kesho ajitokeze kupingana na falsafa yake? Ni wazi wanaozungumza hivi wanakosea," mmoja wa watu wa karibu na Lowassa aliliambia gazeti hili hivi karibuni.

Uchaguzi Mkuu wa CCM unatarajiwa kufanyika wiki ya kwanza ya Mwezi Novemba.

Source: Mwananchi
 
Kusema kweli, kinyang'anyiro ni kigumu sana, kwani kubaki kwa Malecela katika nafasi hii kunatokana moja kwa moja na huruma ya mwenyekiti wa sisiemu kwa namna moja ama nyingine, kama ilivyokuwa katika awamu mbili zilizopita. Mzee Tingatinga ni muhimu sana katika chama.
Sina uhakika kama muungwana *Kingwendu* atamtupa Mzee Malecela, ukizingatia kuwa ni mmoja wa wazee tegemeo la chama katika kuweka mambo sawa. Kumbuka kuwa ni mzee huyu huyu ametumika 'Kukomboa' majimbo kadhaa yaliyoachwa wazi, hadi akaitwa "Tingatinga". Mfano ni hivi karibuni aliposhiriki moja kwa moja katika kampezi za uchaguzi mdogo wa jimbo la Tunduru, lililoachwa wazi baada ya mbunge wake kuaga dunia.
Pia, huenda mwenyekiti akamwacha mzee ili 'kufuta' uvumi kuwa wanamtandao hawawataki 'wazee' madarakani, kwa hiyo akiondolewa katika nafasi hii huenda mashabiki wa siasa ya falsafa ya vijana wakashangilia utabiri wao. Hii huenda ni moja ya sababu zitakazombakisha mzee huyu, si tunaona kwa Kingunge?
Nina uhakika huenda mzee "Tinga tinga" akabaki madarakani mwaka huu, 'hadi kifo kitakapomchukua', ili kulinda utengano ulioletwa na kundi la wanamtandao. Kuondolewa kwake huenda kukazua chuki toka kwa wazee wa chama hiki.
Tusubiri matokeo!
 
Huko CCM kutakuwa vichekesho vitupu maanake hao kina JK na EL wameonyesha wazi kuwa bado kabisa hawajapata somo la Utawala bora. Hekima na Busara ni vitu vipya kabisa ktk bongo zao leo wanataka kuwaondoa wazee ili washike vijana?...
Hivi tu ktk kuongoza nchi wakitumia nguvu ya dola wanashindwa itakuwa chama bila wazee kutakalika kweli huko?
 
Mzee MMJ,

Umesahau katibu, Kinana!

Makamba, maji ya shingo baada ya kumuudhi Muungwana, kuhusiana na uchaguzi wa Kigoda, NEC huko Tanga........!

Lowassa, anautaka lakini kitendo cha mtoto wake kununua nyumba ya Shillingi Millioni 800, nyumba ambayo Muungwana alienda kuiona kwa macho yake saa za usiku, na maneno ya Lowassa kuhusu wazee kujiondoa uongozini, mkono wake kwenye kesi ya wabunge, kumempunguzia sana uwezekano wa kupata hiyo nafasi,

So far Muungwana, amekataa kumwambia mtu yoyote atampa nani, lakini we will soon find out kabla ya ya wiki ijayo, tutaiweka hapa hapa JF, it is coming!
 
Mwaka huu tutaona viroja. Hivi ni kwa mshahara gani anaweza kununua nyumba ya millioni 800. Kodi amelipa kiasi gani? Je, hiyo pesa kama ni halali ililipiwa kodi. Haya mambo ya mishen town hayatatusaidia kuendelea wanaopenda biashara wakae kwenye biashara waache mambo ya siasa.

Siasa isiwe kigezo cha kujitajirisha.
 
Nyumba ya sh. million 800? Tanzania yetu ile? Pale Dar es Salaam au sio?

Bila ya soni wala nini? Mchana kweupeee, kila mlalahoi akishangilia kijana akijitutumua na sh. millioni 800!
Kazipata wapi?

Anayo miradi gani huyo kijana! Amekopa benki? Ni mradi wa kikundi cha watu?

Jama eeeh, tuelezane ukweli; tusije tukaanza kupotezeana kuaminiana katika vita hii inayotukabili.

Kada Mpi... na viburudisho vyako vya kila Ijumaa, nasi tuwekee hapa tuburudishe macho basi.
 
mnataka kuniambia JK hana kazi zaidi ya kwenda kuchungulia nyumba ya mtoto wa lowassa, je yeye kafanya hivyo kama nani ? polisi, PCCB? cid? au nani ? hizi habari nyingine ni za kweli au maneno tu ? tuweni makini jamani huyu ni rais na sio kama mnavyodhani !

Jamani hapa mie sitomuonea mtu yoyote yule aibu lakini panapostahili kusema lazima tuseme, huu mchezo wa kuongea vitu ambavyo watu wanavitoa vijiweni na kuja kuandika hapa ni kupotezana big time ukizingatia mnasema JF ni ukataji ishu, sasa credi. inaenda wapi ? maana sasa hii itakuwa kama magazeti ya globalpublishers ya akina shigongo !
Ninaamini kwamba kama kweli hizi habari ni za kweli ingeanzishwa thread na sio kama maneno tu ya juu juu ambayo mtu unasema mara moja then watu wanapick up na kuweka chuki kwa viongozi wetu kitu ambacho si cha kiungwana na si cha kimaadili mema !

haya maneno ya kusema JK kaenda kuona nyumba ya mtoto wa lowassa usiku ni serious na hatutaki kupakaza matope viongozi wetu na itabidi tueleweshwe hapa otherwise itakuwa ni yale yale kwamba MENGI YANAYOZUNGUZWA HAPA NI UDAKU.... hadi sasa hivi naona ni 65% udaku na kuna uhakika udaku ukaongezeka hadi 85% iwapo watu hawatojibu walichoandika !
 
Nyumba ya sh. million 800? Tanzania yetu ile? Pale Dar es Salaam au sio?

Bila ya soni wala nini? Mchana kweupeee, kila mlalahoi akishangilia kijana akijitutumua na sh. millioni 800!
Kazipata wapi?

Anayo miradi gani huyo kijana! Amekopa benki? Ni mradi wa kikundi cha watu?

Jama eeeh, tuelezane ukweli; tusije tukaanza kupotezeana kuaminiana katika vita hii inayotukabili.

Kada Mpi... na viburudisho vyako vya kila Ijumaa, nasi tuwekee hapa tuburudishe macho basi.

mzee hayo mambo nimewaachia watu wengine sasa wawe wanaburudisha bana si unajua tena, nilikuwa kwenye limelight kipindi kile na inabidi niache wengine waendeleze mambo ! lakini tutakuwa wote katika kuendeleza shughuli za ijumaa kama kawa !
 
Kusema kweli, kinyang'anyiro ni kigumu sana, kwani kubaki kwa Malecela katika nafasi hii kunatokana moja kwa moja na huruma ya mwenyekiti wa sisiemu kwa namna moja ama nyingine, kama ilivyokuwa katika awamu mbili zilizopita. Mzee Tingatinga ni muhimu sana katika chama.
Sina uhakika kama muungwana *Kingwendu* atamtupa Mzee Malecela, ukizingatia kuwa ni mmoja wa wazee tegemeo la chama katika kuweka mambo sawa. Kumbuka kuwa ni mzee huyu huyu ametumika 'Kukomboa' majimbo kadhaa yaliyoachwa wazi, hadi akaitwa "Tingatinga". Mfano ni hivi karibuni aliposhiriki moja kwa moja katika kampezi za uchaguzi mdogo wa jimbo la Tunduru, lililoachwa wazi baada ya mbunge wake kuaga dunia.
Pia, huenda mwenyekiti akamwacha mzee ili 'kufuta' uvumi kuwa wanamtandao hawawataki 'wazee' madarakani, kwa hiyo akiondolewa katika nafasi hii huenda mashabiki wa siasa ya falsafa ya vijana wakashangilia utabiri wao. Hii huenda ni moja ya sababu zitakazombakisha mzee huyu, si tunaona kwa Kingunge?
Nina uhakika huenda mzee "Tinga tinga" akabaki madarakani mwaka huu, 'hadi kifo kitakapomchukua', ili kulinda utengano ulioletwa na kundi la wanamtandao. Kuondolewa kwake huenda kukazua chuki toka kwa wazee wa chama hiki.
Tusubiri matokeo!


mtu pori.....

kwi kiw kwi,mzee TINGA TINGA sio duh sio utani. by the way Dr Malecela mie naona ni muhimi sana ktk chama kwa sasa,unajua wazee kama yeye muhimu sana.

ES...hebu tuwekeeni hiyo nyumba ya miliioni 800 tuione jamani.
 
Kada,
Muda si mrefu kule BCSTIME halafu hata hapa tulimbishia mambo mengi sana Mzee ES, kuwa outspoken, malicious lies etc etc; lakini baadaye naweza kusema, 90 percent ya yale aliyoyasema yamekuwa ni kweli. Mojawapo ni mtandao, Mkapa alivyoiba/ufisadi, etc etc! Kwa Tanzania ya leo everything/anything is possible!
 
Tatizo kubwa ambalo naliona hapa ni kwamba badala ya kujadili nini kimeandikwa, baadhi ya JF members wanaangalia jina la aliyeandika issue ...................................

Teh teh teh........
 
Mnaoweza si mshaurini mzee Malecela aachane na hayo mambo ya umakamu wa Mwenyekiti? Inatakiwa sasa awe mzee wa chama kama akina Mwinyi, Kawawa, Mkapa na wengine na atoe ushauri toka pembeni.

Ila CCM kweli sasa imekwisha maana kama hata Makamba anahesabiwa kuwa makamu Mwenyekiti, hapo kazi ipo kweli kweli.

Wacha tusubiri na tutayasikia kwanza hapa JF kupitia kwa wakuu mbalimbali.
 
Wote hawafai Malecela, Kinana, Lowassa, Kingunge, Makamba, Jaka Mwambi, Aggrey Mwanri na Sumaye.

CCM wanahitaji somebody mpya kabisa na msiniulize kutoka wapi...

Hapo ndio namkumbuka mzee BWM anakuibulia mtu, virtually from no-where!
 
Lisemwalo lipo kama halipo laja.unaoitwa udaku mara nyingi hutokea ukaw kweli.Hebu tufanyeni utafiti tuwe na data kamili
 
mtu pori.....

kwi kiw kwi,mzee TINGA TINGA sio duh sio utani. by the way Dr Malecela mie naona ni muhimi sana ktk chama kwa sasa,unajua wazee kama yeye muhimu sana.

ES...hebu tuwekeeni hiyo nyumba ya miliioni 800 tuione jamani.
Reply With Quote

Ni kweli Mzee Malecela anajulikana kwa jina hilo kisiasa. Huyu 'inasemekana' ni makamu wa chama aliyeshika madaraka kwa muda mrefu sana na katika awamu tatu tofauti. Hakuna makamu mwingine mwenye sifa hizi kwa sasa.
 
Interested Observer
--------------------------------------------------------------------------------

Kada,
Muda si mrefu kule BCSTIME halafu hata hapa tulimbishia mambo mengi sana Mzee ES, kuwa outspoken, malicious lies etc etc; lakini baadaye naweza kusema, 90 percent ya yale aliyoyasema yamekuwa ni kweli. Mojawapo ni mtandao, Mkapa alivyoiba/ufisadi, etc etc! Kwa Tanzania ya leo everything/anything is possible!


Mkuu IO,

Heshima mbele mkuu, muda wa kubishana na mtu yoyote kuhusiana na dataz, sina tena siku hizi, BCS niliposema kuhusu barua ya Butiku, kwa Mkapa nafikiri unakumbuka yale matusi, halafu nilipotabiri kuhusu uwezo mdogo wa Mtandao kisiasa, licha ya uwezo mkubwa kipesa, nafikiri unakumbuka yale matusi niliyorushiwa, niliposema seriklai ya Muungwana, itakuwa ya kishikaji sana unakumbuka yale matusi niliyoporomoshewa,

Sasa what do we do? As long as tunaamini tunayosema ni ya kweli na tulishajifunza siku nyingi kuwa wananchi wengi hapa huwa hawana hizo info, ingawa ni mashujaa wa kujifanya wanajaua kama kawaida yetu wabongo, sisi ni kuendelea kumwaga vitu, kuna wenye common sense hufuatilia na kuzipata hatimaye, na kuna wenzangu na mimi,

Ninasema kuwa tutaendelea kutoa dataz hapa forum, bila uoga wala wasi wasi, Unajua Admin, ana maneno yake chini yanayosema "Ficha Upumbavu Wako" huwa ninayaheshimu, sina mpango wowote wa kumlazimisha kuamini dataz, maana tumeona ya kutosha hapa forum, ndio maana Mchambuzi, kidogo aiteke hii forum na kutuaminisha kuwa Lowassa anafaaa kuwa next president, kuna walioanza mpaka kukubali kuwa ansema ukweli, mpaka wenye dataz tulipoanza kumkaba koo ndio akajiondokea, kwa ustaarabu!

Kuwepo hapa forum kwetu wengine ni committment, na sio kuja ku-hang out tu, na kusindikiza wengine, kwa wale tunaojua safari za maisha, ni kwamba siku zote ni lazima bin-adam uanzie somewhere, na hapa forum ni one of the places pia,

dataz tutaendelea kuzitoa regardless of what, hakuna anyelazimishwa kuamini, nafikiri uliiona ile article against Dr. Slaa ambayo juzi almost kwa kauli moja hapa forum tuliikataa kuwa ni ujinga mtupu, WHY? Ni kwa sababu huwezi kuzipikz dataz zikaonekana kuwa ni kweli, hapana uongo huonekana toka asubuhi kuwa ni uongo, ingawa kuipinga kwangu ile article so far kunaniletea mashambulizi sana hapa forum maana kuna niliowaudhi kwa kuikataa ile article ya uzushi against DR. Slaa, mimi sina noma maana ninaujua mchezo wa siasa kwa kina, na ni mchezo ninaoupenda tena sana,

Kwa hiyo wakuu tutaendelea bila ya wasi kukata ishus na kumwaga dataz, asiyetaka ni kubadili channel tu! Now lets get on with more dataz....

....The dataz, ni kwamba Makamba hamtaki Kigoda, kwa hiyo akaenda Tanga na kuzunguka mkoa mzima, akiwataka wenyeviti wa CCM wa mikoa na wilaya, kutomsaidia na kwamba Muungwana, ndiye aliyemtuma wampigie mgombea mwingine, kwenye kikao cha juzi cha siri Dar cha CC, ni ishu iliyoleta mzozo ndani huko mpaka ikabidi Muungwana, kumpigia simu huyo mgombea anayepingana na Kigoda, na kumtukana mbele ya wajumbe kuwa aache mara moja huo ujinga maana the last thing Muungwana alisema hataki ni ugomvi na Kigoda, na akamuonya Makamba mbele ya wajumbe hao kuwa he is fed up na ujinga wake na kwamba he can't wait kumg'oa..!

Ahsante wakuu na we will never stop!
 
Ninasema kuwa tutaendelea kutoa dataz hapa forum, bila uoga wala wasi wasi, Unajua Admin, ana maneno yake chini yanayosema "Ficha Upumbavu Wako" huwa ninayaheshimu, sina mpango wowote wa kumlazimisha kuamini dataz, maana tumeona ya kutosha hapa forum, ndio maana Mchambuzi, kidogo aiteke hii forum na kutuaminisha kuwa Lowassa anafaaa kuwa next president, kuna walioanza mpaka kukubali kuwa ansema ukweli, mpaka wenye dataz tulipoanza kumkaba koo ndio akajiondokea, kwa ustaarabu!

Ahsante wakuu na we will never stop!

Heshima mbele Mukulu!
Endelea kutumwagia mavitu.Anayetaka ataamini asiyetaka atajiju! Haujamlazimisha mtu kusoma data zako kisha aziamini. Tanzania ninaijua vizuri is just the matter of common sense. Mtu kama anasubiri JK aje atangaze kuwa alikwenda kuiangalia nyumba ya 800Mil ya mtoto wa EL usiku ndo aamini asubiri hiyo kauli. Mie ninayejua unafiki wa viongozi wa Tanzania hilo sizani kama haliwezekani.
Wale wanaong'ang'nia ushahidi inawezekana na JK kwenda usiku ilikuwa ni kupata ushahidi ili ajionee jinsi familia ya waziri wake inavyokula nchi.
 
Heshima mbele Mukulu!
Endelea kutumwagia mavitu.Anayetaka ataamini asiyetaka atajiju! Haujamlazimisha mtu kusoma data zako kisha aziamini.

Mkuu hakuna maneno, heshima mbele tunaendelea kuzifukua dataz tu, zingine zinasema kuwa mkuu Lowassa, kumbe ana mtu wake ndani ya Tanzania Daima, ambaye humbonyeza in advance kama kuna article ya kumkosoa, kwa mfano hivi majuzi ilitakiwa itolewe article kali ya kumlima kutokana na yeye Lowassa, kutukanwa na mkuu mmoja wa wilaya, kule alikoulizwa na mtoto mdogo maswali yasiyojibika, majibu ya wananchi kutoka mkoa wa Lindi, ambayo waliyatuma kwa gazeti hilo, waliomchagua mwenyekiti wao wa CCM mpya hivi karibuni mwenye umri wa miaka 76, na jinsi alivyotukanwa na Muungwana, kuhusiana na maneno aliyoyasema kuhusu viongozi wazee, na maswali ya yule mtoto,

Tunasikia the night before the arctile itolewe, mkuu akwamwagia mapesa na hasa huyu mtu wake, article ikazimwa, ujumbe wangu huko ni kwamba huwa tunaamini sana Tanzania Daima, sasa kama na nyinyi mmekuwa penetrated na hawa wakulu sasa tutamuamini nani?
 
Back
Top Bottom