Mpira wa kona
JF-Expert Member
- Nov 25, 2016
- 350
- 338
Nimekuwa nafuatilia kauli mbalimbali za viongozi wa CCM Juu ya usaliti wa baadhi ya wanachama wake.Viongozi hao wamekuwa wanajifanya wao ni watiifu lakini wengine ni wasaliti Na kufikia hatua ya kuwafukuza uanachama.Najiuliza hao viongozi wao ni watiifu Kwa ushahidi UPI? Kwa mfano Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita anadiriki Kuwait's wanachama wenzake wasaliti wakati yeye upo ushaidi wa kuwa msaliti.Viongozi wa CCM mnachotakiwa kujua zama za kukipenda chama zimepitwa Na wakati sasa hivi watu wanakipenda chama Kwa maslahi Na baya zaidi anapendwa MTU ambaye wanachama wanajua atawasaidia .Ushahidi huo tumeuona pamoja Na CCM kumfanyia MIZENGWE Na KUMTUKANA Mh.Lowassa bado maelfu ya wanachama walimfuata kiroho Mh.Lowassa Na bado wanaendelea kumwamini.Naamini CCM INA uhakika kuwa robo tatu ya wanachama wake pamoja Na idadi kubwa ya viongozi wake wana imani kubwa Na kamanda Lowassa .Ushahidi ni wakati wa mkutano mkuu wa uchaguzi, mikutano ya kampeni (Akiwa Chadema), mkutano wa ccm wa kukabidhi uenyekiti n.k.Nawashauri CCM wanachama wanampenda Mh.Lowassa KIROHO ni wengi sana hats mkiwafukuza hao mnaidhani wasaliti bado mtawaacha wengine wanaomkubali.Kidumu chama cha Mapinduzi.