Ashasembeko
JF-Expert Member
- Dec 14, 2017
- 225
- 910
Nimekua nikijiuliza, hivi kwanini CCM wanashangilia sana kuapa kwa wabunge wa Viti Maalum wa CHADEMA kuliko hata wanaCHADEMA wenyewe?
Jibu lililowazi ni kuwa Uchaguzi wa October umefanya viongozi wateule kukosa uhalali wa uongozi ndani na nje ya nchi (haswa nchi za magharibi). Hili sio tatizo maana tunajua Jiwe hajali kuhusu uhalali wowote, angekua anajali, asingefanya aliyofanya kwenye uchaguzi.
Sababu nyengine yaweza kuwa CCM wamegundua kukaa peke yao bungeni wangeishia kulumabana wao kwa wao. Pia wasingeweza kuwaonyooshea vidole wapinzani kuwa ndo wanakwamisha maendeleo, wakati bunge lote lilikua lao.
Lakini sababu kuu, na yenye msingi ni fedha. Kabla ya hawa wabunge 19 wa CHADEMA, bunge lilikua na wabunge wawili wa kuteuliwa walioapa. Mfumo wa Bunge unahitaji uongozi wa upinzani kwenye baadhi ya kamati kama PAC kwa ajili ya oversight. Wafadhili wasingetoa pesa zao kwenye bunge lisilokuwa na mfumo wa kuchunguza pesa zao zinatumika vipi. Hata hivyo, uteuzi wa wabunge wa Africa Mashariki na Umoja wa Africa unahitaji baadhi ya wabunge watoke upinzani. Hapa pia walikwama.
Yaaani Bunge ilibidi libadilishe kanuni zake ili liweze endesha shuguli zake. Walikua wanawahitaji sana hao wabunge wa CHADEMA ili bunge liweze kuendeswa bila kubadili kanuni na ndio maana nguvu kubwa sana imetumika kuwaconvince kina Mdee.
Hata hivyo, sio siri kuwa nchi yetu kwa sasa inapitia msukomsuko mkubwa wa kidiplomasia. Hawa Viti Maalum wamempa Kabudi "utetezi" akienda kwa wafadhili na vyombo vya habari vya kimataifa. Kila wakimuuliza kama uchaguzi ulikua huru na haki atawajibu kuwa "hao waliosema haukua huru mbona wamepeleka wabunge wa viti maalumu kwa idadi ya kura za uchaguzi huu?"
Kwa namna moja ni habari njema kwa Magufuli, ila bado wanasafari ndefu sana. Kuna plenty of evidence ambazo tayari zimewasilishwa ICC na mabalozi kuhusu mwenendo wa uchaguzi. Bado itawawia vigumu sana kujitetea.
Chazo changu kinachofanya kazi kwenye moja ya hizi balozi kimeniambia kuwa traditional development partners wote, ambao ndio wanamchango mkubwa kwenye bajeti (UK,USA, EU, Cannada, South Korea, Japan na Nordic countries zote) wamekubaliana "informally" kuhusu namna watakavyojihusisha na serikali hii.
Amenihakikishia kuwa kutakua na focus kubwa sana ya kutoa financial support kwa Non government actors (NGOs, CSOs, Activists). Na misaada yao kwenye bajeti ya nchi itapungua mno in fact miradi itakayoendelea ni ile ambayo ipo kwenye utekelezaji, Ila hakuna miradi mipya itakayofadhiliwa na wao. Hii ni changamoto kwa serikali.
Uzuri ni kuwa serikali wataendelea pata support ya Benki ya Dunia na African Development Bank ambazo policies zao zinawakataza kujihisisha na kuingilia mambo ya kisiasa. Japo nchi kama Marekani inaweza tumia nguvu yake katika taasisi hizi kuzuia mikopo. Jua kwamba Marekani na UK ni wanahisani wakubwa zaidi Beni ya Dunia na Africa Development Bank.
Wanaweza wakatumia hiki kigezo washawishi bodi wasipitishe miradi, kama walivyofanya Januari mwaka huu kwenye ule mradi wa elimu wa sekondari (SEQUIP). Hata hivyo Benki ya Dunia haitotoa misaada ya policy support kama wanavyofanyaga.
Huko Zanzibar ndio kabisa, uchumi uko vibaya, na Mwinyi anahangaika sana kuhakikisha Maalim anaingia kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa ili apate uhalali.
Nawaonea huruma sana wafanyabiashara maana wao ndio watakandamizwa sana. Serikali itahitaji kodi zenu kuliko wakati mwengine wowote ule.
Jibu lililowazi ni kuwa Uchaguzi wa October umefanya viongozi wateule kukosa uhalali wa uongozi ndani na nje ya nchi (haswa nchi za magharibi). Hili sio tatizo maana tunajua Jiwe hajali kuhusu uhalali wowote, angekua anajali, asingefanya aliyofanya kwenye uchaguzi.
Sababu nyengine yaweza kuwa CCM wamegundua kukaa peke yao bungeni wangeishia kulumabana wao kwa wao. Pia wasingeweza kuwaonyooshea vidole wapinzani kuwa ndo wanakwamisha maendeleo, wakati bunge lote lilikua lao.
Lakini sababu kuu, na yenye msingi ni fedha. Kabla ya hawa wabunge 19 wa CHADEMA, bunge lilikua na wabunge wawili wa kuteuliwa walioapa. Mfumo wa Bunge unahitaji uongozi wa upinzani kwenye baadhi ya kamati kama PAC kwa ajili ya oversight. Wafadhili wasingetoa pesa zao kwenye bunge lisilokuwa na mfumo wa kuchunguza pesa zao zinatumika vipi. Hata hivyo, uteuzi wa wabunge wa Africa Mashariki na Umoja wa Africa unahitaji baadhi ya wabunge watoke upinzani. Hapa pia walikwama.
Yaaani Bunge ilibidi libadilishe kanuni zake ili liweze endesha shuguli zake. Walikua wanawahitaji sana hao wabunge wa CHADEMA ili bunge liweze kuendeswa bila kubadili kanuni na ndio maana nguvu kubwa sana imetumika kuwaconvince kina Mdee.
Hata hivyo, sio siri kuwa nchi yetu kwa sasa inapitia msukomsuko mkubwa wa kidiplomasia. Hawa Viti Maalum wamempa Kabudi "utetezi" akienda kwa wafadhili na vyombo vya habari vya kimataifa. Kila wakimuuliza kama uchaguzi ulikua huru na haki atawajibu kuwa "hao waliosema haukua huru mbona wamepeleka wabunge wa viti maalumu kwa idadi ya kura za uchaguzi huu?"
Kwa namna moja ni habari njema kwa Magufuli, ila bado wanasafari ndefu sana. Kuna plenty of evidence ambazo tayari zimewasilishwa ICC na mabalozi kuhusu mwenendo wa uchaguzi. Bado itawawia vigumu sana kujitetea.
Chazo changu kinachofanya kazi kwenye moja ya hizi balozi kimeniambia kuwa traditional development partners wote, ambao ndio wanamchango mkubwa kwenye bajeti (UK,USA, EU, Cannada, South Korea, Japan na Nordic countries zote) wamekubaliana "informally" kuhusu namna watakavyojihusisha na serikali hii.
Amenihakikishia kuwa kutakua na focus kubwa sana ya kutoa financial support kwa Non government actors (NGOs, CSOs, Activists). Na misaada yao kwenye bajeti ya nchi itapungua mno in fact miradi itakayoendelea ni ile ambayo ipo kwenye utekelezaji, Ila hakuna miradi mipya itakayofadhiliwa na wao. Hii ni changamoto kwa serikali.
Uzuri ni kuwa serikali wataendelea pata support ya Benki ya Dunia na African Development Bank ambazo policies zao zinawakataza kujihisisha na kuingilia mambo ya kisiasa. Japo nchi kama Marekani inaweza tumia nguvu yake katika taasisi hizi kuzuia mikopo. Jua kwamba Marekani na UK ni wanahisani wakubwa zaidi Beni ya Dunia na Africa Development Bank.
Wanaweza wakatumia hiki kigezo washawishi bodi wasipitishe miradi, kama walivyofanya Januari mwaka huu kwenye ule mradi wa elimu wa sekondari (SEQUIP). Hata hivyo Benki ya Dunia haitotoa misaada ya policy support kama wanavyofanyaga.
Huko Zanzibar ndio kabisa, uchumi uko vibaya, na Mwinyi anahangaika sana kuhakikisha Maalim anaingia kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa ili apate uhalali.
Nawaonea huruma sana wafanyabiashara maana wao ndio watakandamizwa sana. Serikali itahitaji kodi zenu kuliko wakati mwengine wowote ule.