Quinty
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 462
- 74
Nimeona hii picha ukiangalia kwa makini unaona ni jinsi gani CCM wanavyotumia technologia kutengeneza picha ili ionekena wana wingi wa watu katika kampeni/mikutano yao. Hizi ndo siasa uchwara tunaziita maana kama unasera makini wananchi watavutiwa na watajaa kwenye mikutano ila kama sera zako ni za ubabaishaji na ahadi nyingi zisizotimizika kila siku ahadi na hata siku hatujasikia kampeni ya kueleza uteketelezaji hakuna atakaye hudhuria mikutano na matokeo yake kuficha aibu ndo haya mambo ya picha. Ieleweke kwamba watanzania wa sasa wamekuwa na utashi mkubwa sana wa kuelewa mambo tofauti na miaka ya nyuma.