CCM na Siasa za Misibani...!

the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Miongoni mwa mambo ambayo wanasiasa wanayatumia katika kujiweka karibu na watu, kwa kuamini katika falsafa ya siasa ni watu na mwanasiasa ni wafuasi, wanasiasa sehemu mbalimbali wamekuwa wakishughulika zaidi na matukio ya kijamii na yenye kuvuta hisia za wengi. Matukio kama ya misiba, michezo na mahafali n.k

Matukio ya kijamii ambayo yanaambatana na huzuni ama maafa yanawavuta wengi zaidi katika kufariji wahanga na waathirika, wanasiasa wengi na walio makini wanatumia zaidi matukio haya kujijenga na kujiimarisha kisiasa. Tukio kama la mafuriko ya jangwani, mabomu ya gongo la mboto, misiba ya wasanii wakubwa kama kanumba na wengineo yalitumika vyema hasa na wanasiasa kutoka upande wa chama tawala katika kufarijiana na kusaidiana na wahanga na waathirika.

Utaratibu huu ambao wanasiasa wa chama cha mapinduzi wamekuwa nao wa kujiweka karibu na wananchi hasa wakati wa shida zao unawaimarisha na kuwasaidia kujijenga kisiasa, jambo hili ni la msingi kisiasa kwa kuzingatia nature ya jamii yetu na tabia tuliyojijengea kama watanzania wenye itikadi ya ujamaa na kujaliana hasa wakati wa shida.

Nimemuona NAPE kwenye mazishi ya John Stephen Maganga, akiwa kama muwakilishi kutoka chama cha mapinduzi na akapewa platform ya kufikisha salamu za rambirambi kutoka kwa mwenyekiti wa chama chake. Lakini nikiri kuwa sijamuona prominent figure yeyote kutoka chadema kwenye mazishi hayo, na nategemea kuwaona tena viongozi wa CCM Tanga kwenye mazishi ya Msanii wa Filamu Shalo-Milionea na pia naweza nisiwaone viongozi wa chadema wakiwakilisha chama chao, ama CUF ama TLP.

Katika midani ya siasa za sasa na mvutano wa kipinzani baina ya vyama vya siasa, hakuna nguvu wanayoitegemea isipokuwa watu wao, wafuasi. Na wafuasi wanapatikana katika mambo kama haya, mitazamo ya watu wetu inaangalia zaidi ni nani yupo karibu yao hasa katika kipindi cha shida, " a friend in needy, is a friend indeed " waswahili wanasema "rafiki wa kweli ni yule anayekujali wakati wa shida".

"...WAPINZANI KUWENI MARAFIKI WA KWELI KWA WATANZANIA..."
 
sasa inakuaje vyama vya siasa navyo vinapeperusha bendela hadi misibani
 
Kwa hiyo misiba ndio maendeleo waliyoyahidi wakina JK:majani7: Kama akili zako zipo hivyo sijajua wanaoi watakuwaje:majani7:Only time will tell and will bring cream mind......
 
Kwa hiyo misiba ndio maendeleo waliyoyahidi wakina JK:majani7: Kama akili zako zipo hivyo sijajua wanaoi watakuwaje:majani7:Only time will tell and will bring cream mind......
Angekuwa ameenda Dr. Slaa(babu). HAPA UNGETANUA MIDOMO MPAKA MAPOVU KUTETEA KUWA KAFANYA JAMBO KUBWA,LAKINI KISA IMEFANYWA NA CCM BASI NI JAMBO LA HOVYO....NYAMBAFU....
 
mwanangu umeandika BOGUSNESS hata sijakuelewa...............!

haya ndiyo majibu mepesi wanayotaka kuyasikia watz kutokana na maswali magumu. Kwani akikupa hiyo hela na barabara zikaendelea kuwa mbovu itasaidia nini? Hospitali mbovu? Shule, vyuo vibovu? Msiba hausaidii chochote zaidi kwa mtu anayetaka kujiosha. Hizo ajali si zimesababishwa na ubovu wa barabara? Endeleeni kuwa wajinga na msiotaka kutafuta suluhu ya ujinga wenu
 
Angekuwa ameenda Dr. Slaa(babu). HAPA UNGETANUA MIDOMO MPAKA MAPOVU KUTETEA KUWA KAFANYA JAMBO KUBWA,LAKINI KISA IMEFANYWA NA CCM BASI NI JAMBO LA HOVYO....NYAMBAFU....
Hiyo Nyambafu nafikiri inakufaa wewe mbona hao unaowashabikia hawakuwa mstari wa mbele kwenye msiba wa Mwangosi au dhamira ilikuwa inawasuta kwa kuuwa? na inatakiwa ujue serikali ya Kisanii ushabikia misiba ya wasanii lakini CCM ingekuwa ni serikali inayozingatia misingi ya usawa isinge bagua
 
huyo NAPE anataka political influence mbona mpaka anatuwekea picha yake kwenye mitandao na si bure hapo kunauwezekano karipia!!
 
Hapo ndipo napochoka na akili za wanasiasa wa Tanzania ambao wanadhani kuhudhuria misiba wataonekana kuwa wako karibu na wananchi. Ni unafiki uliopitiliza kwenda misibani kujidai kuomboleza na wafiwa wakati kwa hali halisi hawajali kabisa maisha ya wananchi. Kushiriki katika misiba itakuwa faraja kwa wachache, lakini kwa Watanzania wengi huo ni unafiki wa hali ya juu. Boresheni kwanza maisha ya walio hai.
 
miongoni mwa mambo ambayo wanasiasa wanayatumia katika kujiweka karibu na watu, kwa kuamini katika falsafa ya siasa ni watu na mwanasiasa ni wafuasi, wanasiasa sehemu mbalimbali wamekuwa wakishughulika zaidi na matukio ya kijamii na yenye kuvuta hisia za wengi. Matukio kama ya misiba, michezo na mahafali n.k

matukio ya kijamii ambayo yanaambatana na huzuni ama maafa yanawavuta wengi zaidi katika kufariji wahanga na waathirika, wanasiasa wengi na walio makini wanatumia zaidi matukio haya kujijenga na kujiimarisha kisiasa. Tukio kama la mafuriko ya jangwani, mabomu ya gongo la mboto, misiba ya wasanii wakubwa kama kanumba na wengineo yalitumika vyema hasa na wanasiasa kutoka upande wa chama tawala katika kufarijiana na kusaidiana na wahanga na waathirika.

Utaratibu huu ambao wanasiasa wa chama cha mapinduzi wamekuwa nao wa kujiweka karibu na wananchi hasa wakati wa shida zao unawaimarisha na kuwasaidia kujijenga kisiasa, jambo hili ni la msingi kisiasa kwa kuzingatia nature ya jamii yetu na tabia tuliyojijengea kama watanzania wenye itikadi ya ujamaa na kujaliana hasa wakati wa shida.

Nimemuona nape kwenye mazishi ya john stephen maganga, akiwa kama muwakilishi kutoka chama cha mapinduzi na akapewa platform ya kufikisha salamu za rambirambi kutoka kwa mwenyekiti wa chama chake. Lakini nikiri kuwa sijamuona prominent figure yeyote kutoka chadema kwenye mazishi hayo, na nategemea kuwaona tena viongozi wa ccm tanga kwenye mazishi ya msanii wa filamu shalo-milionea na pia naweza nisiwaone viongozi wa chadema wakiwakilisha chama chao, ama cuf ama tlp.

Katika midani ya siasa za sasa na mvutano wa kipinzani baina ya vyama vya siasa, hakuna nguvu wanayoitegemea isipokuwa watu wao, wafuasi. Na wafuasi wanapatikana katika mambo kama haya, mitazamo ya watu wetu inaangalia zaidi ni nani yupo karibu yao hasa katika kipindi cha shida, " a friend in needy, is a friend indeed " waswahili wanasema "rafiki wa kweli ni yule anayekujali wakati wa shida".

"...wapinzani kuweni marafiki wa kweli kwa watanzania..."
swala si kuhudhuria misiba, hoja ya msingi ni kutafuta njia ya kuzuia misiba! na hiki ndicho chama makini cha siasa kinajielekeza kufanya! Huo msiba ni matunda ya uzembe wa hao wahudhuriaji misiba ; kwani hawajawapa vitendea kazi madaktari, ila hela za kuhudhuria misiba na kuandaa mikutano ya kampeni wanazo!
 
CCM epukeni kutumia misiba ya watanzania kisiasa,
Nimestushwa na nguvu kubwa ya kipropaganda inayofanywa na ccm ku[itia vyombo vya habari eti eti chadema haijashiriki msiba wa mama yake naZitto.Hii ni aibu na hatari kwa chama tawala nchini kufanya ulaghai wake hata kwenye msiba wa mtanzania,Chadema imeshiriki kumuuguza Bi Shida Salum, akiwa hajazidiwa akiwa hajazidiwa mwenekiti wa Chadema alikuwa ni kiongozi wa kisiasa wa kwanza kumjulia hali na kutoa msaada wa matibabu kwa niaba ya chama.

Pia alipozidiwa na kufikishwa Muhimbili aliendelea kuwa sehemu ya waliomuuguza Bi shida Salum,ambapo viongozi wa juu na wabunge walifika na kumtaka khali pale Muhimbili,huku shughuli za kichama zinaendelea (ziara ya Ukawa) nchini.Taarifa ya msiba wa mama yetu na mjumbe wa kamati kuu,zilitokea wakati viongozi wa juu wakiwa ziarani ambapo Dr Slaa akiwa Singida na Mh Mbowe akiwa Arusha kutokana na mazingira yaliyokuwepo kijiografia kuwa ngumu kuwahi mazishi kule kigoma.

Kutokana na hali hiyo sasa Chama makao makuu kikateua wajumbe wataokiwakilisha chama kwenye msiba ambapo aliteuliwa Wenje,Mdee,Lucy Mukya,Alfi,Mashishanga,Matiko,Anna Mallac,Masishanga na wengine wengi.Sasa binafsi najiuliza hivi ccm hawana utu wala aibu kiasi hiki kutumia msiba wa mama zitto kujinusuru kisiasa? Jana kada mashuhuri wa ccm aliyewahi kushika nyazifa za juu kabisa na ambae kwa sasa ni mbunge Mh Ritha Mlaki amefiwa na mama yake mzazi na msiba umesafilishwa toka Dar kwenda Moshi,lakini hakuna hata kiongozi wa juu aliyefika hata kumpa pole tu Mlaki,siovuvuzera wa ccm (Nape),Muuaji Nchemba,Mg'oaji mashuhuri wa meno ya tembo Kinana wala Kikwete.Inamaana hawakuwa na muda wa kwenda kumhani? Binafsi ninalaani sana kitendo hiki walichokifanya ccm,huu sio uungwana wala utu na sio asili ya siasa za Tanzania kabisa.

Kitu kingine, Uhuni na propaganda ambazo mnazifanya kupitia mitandao ya kijamii kwa kuanza kugombanisha Umoja wa vyama vya upinzani hakika hamtafanikiwa,tutaendelea na mshikamano wetu mpaka kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa hatimaye uchaguzi mkuu 2015.Sasa hivi mala mnasema UKAWA wagombana mara wafanya nini Mnatwanga maji kwenye kinu,Hao vijana mliowanunua kuchafua vyama vya upinzani kwa njia ya mtaandao wanapoteza muda wao tu,2015 ushindi wetu ni Asubuhi sana.Salams kwa mbunge wa Jimbo la Sumve Ndasa pamoja na Mbunge wa jimbo la kwimba Mansour Kama mnaakiri bora muache tu hata kuchukua form kwani majimbo hayo Chadema ushindi ni saa nne tu asubuhi.

Yaliyotokea Malawi yanaenda kutokea Tanzania,Mawaziri waliojipiga Risasi kwa kushindwa ubunge pamoja na chama chao kushindwa hakika hata Tanzania watafanya hivyo kwani watu kama wafuatao sipati picha watajificha wapi Tunapoenda kuchua nchi 2015kama sio kujiua au kwenda uhamishoni.

1.Wasira
2.Kinana
3.Nape
4.Nchemba
5.Lukuvi
6.Werema
7.kingunge
Unaweza ukaongeza wengine.

Mandago 2015 Kwimba@

0765183733
mshulu@yahoo.com


 
Last edited by a moderator:
badala ya kutafuta misiba ilipo kila siku ( KAMA YULE PILI MISIBA WA KEKO ) Naishauri ccm kuangalia namna ya kutimiza hata robo tu ya ahadi zake , kusaka misiba ni uchuro !
 
Back
Top Bottom