CCM na Serikali yake wanavyoicheza ngoma ya Tundu Lissu

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,269
Tukubali tukatae tukio la kupigwa risasi Tundu Lissu litabadilisha siasa za Tanzania na hata Tanzania yenyewe.

Lissu yuko maili zaidi ya elfu 10 kutoka Tanzania lkn akikohoa tu serikali nzima ya Tanzania, Chama tawala, wafuasi wake wote wa mitandaoni wanatetemeka.

Ziara yake inafuatiliwa kuliko hata ziara ya Rais.

Si mawaziri, wabunge, mabalozi, wakuu wa mikoa wanaofuatilia ziara ya Lissu.

Lissu akiongea Lugola anatetemeka.
Lissu akiongea Spika anachanganyikiwa.
Lissu akifanya mahojiano Katibu Mkuu wa CCM anaweweseka.
Lissu akizungumza Polepole anazimia.
Lissu aki post mitandaoni thread zote zinajaa Lissu Lissu.

Hatusikii ya bombardier wala dreamliner siku hizi ni Lissu Lissu tu huku miaka ya awamu ikikatika.


IMG_20190210_124003.jpg
 
Tukubali tukatae tukio la kupigwa risasi Tundu Lissu litabadilisha siasa za Tanzania na hata Tanzania yenyewe.

Lissu yuko maili zaidi ya elfu 10 kutoka Tanzania lkn akikohoa tu serikali ya Tanzania, chama tawala, wafuasi wake hata wa mitandaoni wote wanatetemeka.

Lissu akiongea Lugola anatetemeka.
Lissu akifanya mahojiano Katibu Mkuu wa CCM anaweweseka.
Lissu akizungumza Polepole anazimia.
Lissu aki post mitandaoni thread zote zinajaa Lissu Lissu.

Hatusikii ya bombardier wala dreamliner siku hizi ni Lissu Lissu tu huku miaka ya awamu ikikatika.


View attachment 1023012
Shukrani kubwa sana kwa waratibu wa ziara hii .
 
Maccm Wameingia kichwa kichwa kwenye issue ya Lissu kuomba msaada!
Hawajui wamelengwa subwoofer na bunge lake! Pombe ikiendelea "kuvundikwa"
Kuna mtu aliandika Chadema kina smart people wakati CCM kina intelligent people.

Wao wanafikiri Lissu kuomba msaada kwa wazungu anajidhalilisha kumbe analidhalilisha bunge kwa kutolipa stahiki za mgonjwa.
 
Wao wanafikiri Lissu kuomba msaada kwa wazungu anajidhalilisha kumbe analidhalilisha bunge kwa kutolipa stahiki za mgonjwa.
Then wakija ingia kwenye kesi ndio watajua maana halisi ya kuomba msaada huku kwa Lissu!!!
 
Kuna mtu aliandika Chadema kina smart people wakati CCM kina intelligent people.

Wao wanafikiri Lissu kuomba msaada kwa wazungu anajidhalilisha kumbe analidhalilisha bunge kwa kutolipa stahiki za mgonjwa.
Kufanya maamuzi bila kutambua madhara yake baadae ni hatari sana.

Hawakufikiria madhara yatakayotokea baada ya kuzuia mshahara wake

Haka kataulo cha Bunge kilichokuwa kimebaki nako kanavuliwa..
 
Kufahamu dunia na mahusiano kimataifa ni kitu kikubwa sana katika uongozi. Vinginevyo unaweza kakudanganya kuhusu nguvu zako kumbe hizi nguvu siyo absolute na kuna watu pia wanazifuatilia zinavyotumika.
 
Kufanya maamuzi bila kutambua madhara yake baadae ni hatari sana.

Hawakufikiria madhara yatakayotokea baada ya kuzuia mshahara wake

Haka kataulo cha Bunge kilichokuwa kimebaki nako kanavuliwa..
Kwa sasa dunia nzima inajua bunge letu halina ubinadamu.
 
Back
Top Bottom