Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Hili serikali iweze kuongoza vizuri inahitaji kuwa na wengi wa raia wake nyuma yake. Hivi sasa kila kona ya nchi hii kunasikika vilio vingi vikiilalamikia serikali iliyoko madarakani na chama kilichoiweka pale. Hali hiyo inajenga hisia kwamba, uenda umaarufu wa chama hicho tawala na serikali yake, umeporomoka kiasi cha kushindwa kuongoza nchi bila ya msaada wa vyombo vya dola gandamizi. Kutokana na unyeti wa suala hilo, pengine hivi sasa ni wakati muafaka kwa REDET na Synovate kulifanyia utafiti na kutoa ushauri unaostahili kwa serikali.