Mdaiwa-Sugu
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 284
- 910
Kati ya makosa yaliyofanywa na Serikali yangu ya CCM ni kushindwa kutoa ajira kwa vijana na kuacha wazagae mitaani bila kazi.
Ni kosa kubwa sana kwa sababu vijana hawa ni bomu tulojitegea wenyewe kutumaliza.
Maelfu ya vijana wanaojitokeza kwa wingi kwenye hadhara za bw. Tundu Antipas Lissu ni sababu yetu sisi.
Kwa miaka minne tumewatelekeza mitaani kama kuku wa videri; tumeua future zao; tumewaua kisaikolojia; tumewatoa kwenye reli hadi baadhi wamekata tamaa wameamua kuwa walevi wa gongo na wavuta bangi.
Uchaguzi umefika tutawaeleza nini hawa vijana watuelewe na watuchague?
Tutawashawishi vipi wazazi wao waliowasomesha kwa shida ili watuamini na watuchague?
Tutawambia tumenunua ndege?
Tutawambia tunajenga SGR?
Tutawambia tunajenga daraja la Busisi?
Tutawambia tumejenga flyover?
Wana CCM wenzangu; 'maendeleo ya vitu bila kuboresha maendeleo ya watu ni sawa na kazi bure'
Kwakuwa tumelikoroga kwa miaka minne sasa muda wa kulinywa umewadia.
Ni kosa kubwa sana kwa sababu vijana hawa ni bomu tulojitegea wenyewe kutumaliza.
Maelfu ya vijana wanaojitokeza kwa wingi kwenye hadhara za bw. Tundu Antipas Lissu ni sababu yetu sisi.
Kwa miaka minne tumewatelekeza mitaani kama kuku wa videri; tumeua future zao; tumewaua kisaikolojia; tumewatoa kwenye reli hadi baadhi wamekata tamaa wameamua kuwa walevi wa gongo na wavuta bangi.
Uchaguzi umefika tutawaeleza nini hawa vijana watuelewe na watuchague?
Tutawashawishi vipi wazazi wao waliowasomesha kwa shida ili watuamini na watuchague?
Tutawambia tumenunua ndege?
Tutawambia tunajenga SGR?
Tutawambia tunajenga daraja la Busisi?
Tutawambia tumejenga flyover?
Wana CCM wenzangu; 'maendeleo ya vitu bila kuboresha maendeleo ya watu ni sawa na kazi bure'
Kwakuwa tumelikoroga kwa miaka minne sasa muda wa kulinywa umewadia.