Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,115
- 35,128
Mbunge wa CCM wa jimbo la Siha, Mollel ametoa kauli bungeni ya kusema anao ushahidi wote wa CHADEMA kuhusika na tukio la kushambuliwa kwa Tundu Lissu lakini hataweza kuutoa mpaka CHADEMA watoe uthibitisho wa matumizi ya ruzuku zao!!
Ni kauli ya mizaha na yenye mwelekeo wa kipuuzi kwa watu wengi wanaofuatilia mwelekeo wa tukio lile lilipotokea. Haina mantiki yoyote ya kutaka kutambua wahusika wa tukio lile, lakini inaweza kuwa na mantiki hasi kwa rejea ya mijadala katika kupambana kwa hoja kuhusu tukio lile, hususani kutumiwa na Tundu Lissu mwenyewe ambaye ameonekaa ni hodari katika mijadala kwa kuweza kutumia rejea ya maneno, hotuba au kauli mbalimbali za wale wale wapinzani wake.
Kwa kuwa kauli hii imetolewa na mbunge wa CCM tena ndani ya bunge, moja kwa moja inaweza kuchukuliwa kama ndio mwelekeo wa CCM na serikali yake kwa sasa.
Tukumbuke tu, mpaka sasa CCM, serikali na Vyombo vya dola vinakiri kuwa haiwajui wahusika wa tukio lile na hakuna taarifa nyingine yeyote yenye kuonyesha kama kuna uchunguzi au kesi kufunguliwa kuhusu tukio lile.
Kauli hii inafuta hoja zote za CCM, Serikali na vyombo vyote vya dola ya kusema bado haiwajui wahusika wakati huo huo kuna mtu anasema anawajua wahusika na serikali haijamtafuta mtu huyo ili kuutumia uahahidi wake ili kuwatia hatiani wahusika.
Upande mwingine kauli hii inatoa picha kuwa, serikali haina mpango wa kuwatafuta wahusika, maana kauli za kipuuzi za za watu kama Mollel na Msiba zimeachwa hivyo hivyo, hivyo zimechukuliwa kama msimamo wa CCM na serikali yake.
Ni kauli ya mizaha na yenye mwelekeo wa kipuuzi kwa watu wengi wanaofuatilia mwelekeo wa tukio lile lilipotokea. Haina mantiki yoyote ya kutaka kutambua wahusika wa tukio lile, lakini inaweza kuwa na mantiki hasi kwa rejea ya mijadala katika kupambana kwa hoja kuhusu tukio lile, hususani kutumiwa na Tundu Lissu mwenyewe ambaye ameonekaa ni hodari katika mijadala kwa kuweza kutumia rejea ya maneno, hotuba au kauli mbalimbali za wale wale wapinzani wake.
Kwa kuwa kauli hii imetolewa na mbunge wa CCM tena ndani ya bunge, moja kwa moja inaweza kuchukuliwa kama ndio mwelekeo wa CCM na serikali yake kwa sasa.
Tukumbuke tu, mpaka sasa CCM, serikali na Vyombo vya dola vinakiri kuwa haiwajui wahusika wa tukio lile na hakuna taarifa nyingine yeyote yenye kuonyesha kama kuna uchunguzi au kesi kufunguliwa kuhusu tukio lile.
Kauli hii inafuta hoja zote za CCM, Serikali na vyombo vyote vya dola ya kusema bado haiwajui wahusika wakati huo huo kuna mtu anasema anawajua wahusika na serikali haijamtafuta mtu huyo ili kuutumia uahahidi wake ili kuwatia hatiani wahusika.
Upande mwingine kauli hii inatoa picha kuwa, serikali haina mpango wa kuwatafuta wahusika, maana kauli za kipuuzi za za watu kama Mollel na Msiba zimeachwa hivyo hivyo, hivyo zimechukuliwa kama msimamo wa CCM na serikali yake.